Monday, February 23, 2009

UJAMBAZI ULIOKITHIRI DAR ES SALAAM

From  Sara  Mrema (machomrema@yahoo.com)
Tarehe: Februari 20, 2009, 7.30am.saa za Afrika Mashariki.

Kwa kweli Bwana Afande AGP Saidi Mwema ana kazi nzito.

Napenda kuwataatharisha kuwa muwe makini zaidi mkiwa barabarani hasa
 kwenye  foleni.Kuna kundi la vijana zaidi ya 30 wanavamia magari
 wakiwa na mapanga,nondo na visu kwa lengo la kupora chochote
ulichonacho na halikadhalika wanauwa ama kujeruhi.
 
 Maeneo hatari ni maeneo ya Jangwani- Morogoro Road ,Ocean
 Road, Seaview, Salender Bridge , Bonde la Kigogo ukitokea
Ilala kuja Magomeni, Daraja la Ubungo karibu na njia panda ya kwenda UDSM na
barabara ya Mandela Road ukitokea Tazara kuja Ubungo (NDIPO ALIPOVAMIWA
RAFIKI YANGU)
 
 His Case. Akiwa kwenye folen majira ya saa mbili
usiku, ghafla lilitokea kundi la vijana kama kumi na mapanga na kuanza kupiga vioo vya gari wakitaka kuvunja, aidha waliongezeka ghafla na wakafunga
 barabara kama kwa dakika  7 hivi wakiendelea kumshambulia (kwenye gari
 walikuwa watatu), kumbuka kwenye foleni huwezi kukimbia popote, Mungu
 aliwasaidia sana kwani milango ya gari ilikuwa imefungwa/locked, na vioo
 vilikuwa vimefungwa kasoro kimoja kilikuwa wazi nusu. Baada ya
 mapambano na  kelele za kuomba msaada,ndipo msamalia mwema aliyekuwa na
 silaha aliingilia kati na ndipo alipowatawanya. Kwa mujibu wa Taarifa mbalimbali, haya matukio yamekuwa
 yakiongezeka sana katika siku za usoni, kwa hilo nawatahadharisha
 msinunue vitu ovyo kwenye traffic light, vioo msishushe ovyo na lock za
 milango ya magari mfunge, muwe makini.Ujambazi huu unafanyika kila siku
 sehemu tofauti kuanzia saa 12 jioni kuendelea.
 
 Namshukuru Mungu hakuna aliyeumizwa sana , japo walifanikiwa kupata
 baadhi ya vitu ikiwemo simu ya mwenye gari.
 
 Natambua unaweza kuona kama sinema,ila haya ndio yanayotokea katika
jiji la Dar kwenye foleni za magari.


Mwatawala, Zainab M.
P O Box 453
Morogoro, Tanzania
East Africa
Tel. 255 023 260 3583
Cell: 202 427 4413
5167 Fulton Str. NW
Washington, DC., 20016
USA

1 comment:

  1. Many thanks for the exciting blog! I really enjoyed reading it. Great Job,Keep it up..
    best mhe leasing companies in qatar

    ReplyDelete