Saturday, March 30, 2013

MAONI YA C U F KWA TUME YA KATIBA TANZANIA

IMETUNDIKWA HAPA LEO HII  30  Machi, 2013. 


 THE CIVIC UNITED FRONT
(CUF - Chama Cha Wananchi)

 MAONI YA THE CIVIC UNITED FRONT (CUF- CHAMA CHA WANANCHI) KWA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA-  07 JANUARI,  2013

 UTANGULIZI;

Kwa niaba ya The Civic United Fronf (CUF-Chama Cha wananchi), na kwa niaba
 yangu binafsi napenda kuchukua fursa hii kukushukuru wewe Mwenyekiti wa
 Tume ya Mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na
  wajumbe  wako kwa kutualika rasmi Chama Cha CUF mbele ya Tume yako kutusikiliza na
 kupata maoni ya chama chetu juu ya mchakato huu muhimu kwa mustakbali mwema
 wa Taifa letu la Tanzania pamoja na watu wake.

 Aidha, tunampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Jakaya  Mrisho Kikwete kwa kuanzisha mchakato huu wa mapitio makubwa na kukusanya
 maoni ya katiba ya nchi yetu ili ikidhi matakwa ya wakati wa sasa na
 kutupeleka mbele zaidi kwa ustawi wa Taifa letu na watu wake. Madai haya ya
 kuandaa mchakato wa kuwa na katiba mpya inayokidhi matakwa ya wakati
 tulionao ni madai ya msingi ambayo chama chetu cha CUF kimekuwa
 kikiyasisitiza tangu kurejeshwa tena kwa mfumo wa demokrasia ya vyama vingi
 vya siasa nchini mwaka 1992 na mara zote kuainisha suala hili katika
 manifesto zake za uchaguzi.

 Kutokana na muongozo wa Tume ya Mabadiliko ya katiba maoni yetu yamejikita
 katika maeneo yafuatayo:

(i)     Misingi na Maadili ya Kitaifa, Madaraka ya
(ii)    Wananchi, Muundo wa Nchi na Taifa ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
(iii)    Haki za Binadamu na Wajibu wa Wananchi,
(iv)    Ardhi, Maliasili na Mazingira
 (v)    Mihimili ya Nchi (Ardhi, Watu na Utawala),
(vi)    Mihimili ya Utawala (Serikali,
(vii)    Bunge na Mahakama),
(viii)   Muundo na Mamlaka ya Serikali za Mitaa, na
(ix)    Vyombo vya Ulinzi na Usalama.

 Kwa muhtasari maudhui haya Chama Cha Wananchi CUF kinapendekeza yafuatayo
 katika mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya Mwaka 1977;

 1. Muundo wa serikali tatu za muungano; yaani serikali ya Zanzibar, serikali
 ya Tanganyika na Serikali ya Mungano.

2. Uanzishwaji wa Tume huru za uchaguzi mapema iwezekanavyo. Kwa kuwa Tume
 ya uchaguzi inapaswa kuanza kazi zake mapema ili kufanikisha uchaguzi wa
 mwaka 2014/15, Tume haiwezi kusubiri mabadiliko ya katiba yakamilike ndio
 ianze kazi zake kwa Muundo mpya utakaopendekezwa.

3. Katiba yenye misingi ya mfumo wa uwajibikaji kwa watendaji wote wa umma
 na uainishwaji wa wazi wa Dira ya Taifa.

 4. Katiba itakayotoa haki kwa wagombea binafsi kushiriki katika uchaguzi.

5. Katiba itakayotoa uhuru wa vyama vya siasa kuungana muda wowote
 vitakapoona inafaa bila kupoteza usajili wa kawaida wa vyama hivyo.

6. Katiba itakayoweka muundo wa kuwa na Rais mtendaji "Executive President"
mwenye madaraka yanayopimika na kukubalika yasiyobana wala kuingilia au
 kuondoa uhuru wa utendaji kazi wa mihimili mingine ya dola. Rais achaguliwe
 kwa kupata asilimia 50+1 au zaidi ya kura zilizopigwa.

 7. Katiba yenye kuweka mfumo sahihi wa kulinda rasilimali za Taifa na
 kuhakikisha zinawanufaisha Watanzania wote kwa haki na usawa.

 8. Katiba itakayompa kila Mtanzania kwa nafasi yake kushiriki katika
 maendeleo ya nchi yake kwa kuwa na muundo wa serikali itakayoshirikisha
 kila   Mtanzania mwenye uzalendo wa kweli na uwezo wa kutoa mchango wake kwa ajili
 ya maendeleo na ustawi wa taifa.

 9. Katiba itakayoweka muundo wa uwakilishi wa uwiano (propotional
 representation) ili kila kura itakayopigwa kuwa na thamani tofauti na
 utaratibu wa sasa wa mshindi kuchukua vyote (winner takes all) hata kama ameshinda kwa kura moja.

 10. Katiba itakayo hakikisha uwepo wa mgawanyo wa madaraka kati ya serikali
 kuu na serikali za mitaa kwa kuondoa mfumo wa kuziburuza serikali hizo
 zilizokaribu na wananchi. Wilaya zisianzishwe kiholela. Vigezo vya
 halmashauri ya wilaya, miji, manispaa na majiji vitawekwa na sheria.
 Utawala wa mikoa uondolewe.

 11. Katiba itakayoweka msingi wa kuzuia ufisadi mkubwa wa rasilimali za
 nchi  hasa kwa njia ya uingiaji wa mikataba, Bunge likiwa ni chombo cha
 uwakilishi  wa wananchi lazima lishirikishwe.

 12. Katiba itakayoweka Muundo wa Tume huru za Taifa za uchaguzi tangu ngazi
ya uteuzi wake kuanzia ngazi ya Taifa hadi ngazi ya chini. Katiba
 itakayoto fursa matokeo ya uchaguzi kwa ngazi zote kuhojiwa mahakamani ikiwemo
  matoke ya uchaguzi wa Rais.

13. Katiba itakayopambanua mgawanyo wa madaraka na mamlaka ya mihimili yote
 mikuu katika nchi kwa maana ya Bunge, Serikali na Mahakama.

 14. Katiba itakayoeleza wazi kuhusu haki na wajibu wa dola kuhakikisha
 elimu ya watoto wetu, matumizi ya rasilimali za taifa, huduma za msingi za afya,
 ulinzi wa nchi yetu na sera za ardhi na kilimo zinasimamiwa na kutekelezwa
 kwa manufaa ya wananchi wote. Katiba ndiyo yenye nafasi ya kulinda haki hizi
za mwananchi na si huruma ya mtawala atakaye kuwepo kwa wakati huo au chama
 cha siasa. Sera za kitaifa lazima zifuate na kuheshimu haki zilizoainishwa
 ndani ya katiba.

15. Kuhakikisha kwamba wananchi wana madaraka ya kujiamulia wenyewe masuala
 ya maendeleo yao kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.;

16. Katiba yenye kulinda haki za binaadamu, na kupinga aina zote za ubadhilifu, ukandamizaji, ubaguzi wa aina yeyote iwe wa kidini, kikabila, kijinsia au kikanda.

17. Katiba yenye kuweka misingi endelevu ya kulinda amani ya nchi yetu.

 18. Masuala ya Ardhi yawe na sura kamili katika katiba mpya. Ardhi ni mali
 ya Watanzania wote. Mtanzania peke yake ndiye anayeweza kumiliki ardhi moja
 kwa moja.

 19. Katiba inayohakikisha kuwa haki za msingi za makundi maalum, wanawake,
 watoto, wazee wasiojiweza na walemavu zinalindwa kwa kuanishwa ndani ya
katiba.

Chama cha CUF kipo tayari kutoa ushirikiano unaostahiki kwa Tume katika
 kipindi chote cha mchakato huu pamoja na kushirikiana na Watanzania wote
 bila kujali itikadi za kisiasa na tofauti nyinginezo, kuhakikisha kuwa kwa
 pamoja nchi yetu inakuwa na katiba bora yenye kukidhi haja na matakwa ya
 hali ya kisiasa, kiuchumi na ustawi mwema wa jamii ya Watanzania.
 Ni matarajio ya Chama Cha Wananchi CUF kuwa maoni haya yatazingatiwa na
 kuingizwa katika rasimu ya mabadiliko ya katiba kwa mjadala na hatimaye
 kufanyiwa maamuzi yanayofaa kwa mustakbali mwema wa Taifa letu la Tanzania.

 Mungu Ibariki Tanzania na watu wake.

 HAKI SAWA KWA WOTE

 Prof Ibrahim Haruna Lipumba,
 Mwenyekiti wa CUF Taifa

 Contact;
 P.O.Box 10979
 Dar es salaam, Tanzania.
 lipumba@yahoo.com

Tuesday, March 26, 2013

SHEIKH BILAL REHANI WAIKELA ATINGA MAHAKAMANI KISUTU, DAR ES SALAAM, TANZANIA.


Imetundikwa hapa leo hii tarehe 26/3/2013.

Kutoka:  tz_muslim_community@yahoogroups.com, 25/3/2013.

Asalaam aleikum warahmatullah wa barakatuh,


Haya ndio yaliyojiri mahakama ya Kisutu pale Sheikh Bilal Rehani Waikela ambae alipanda kizimbani kutoa ushahidi wake upande wa washtakiwa.

Sheikh Waikela alikuja kutoka Tabora.

Hakika mahakama jana walisikia ambayo si wengi wamepata kuyasikia katika maisha yao yote.

Sheikh Waikela ameanza kwa kutaja umri wake wa miaka 87 na akaieleza mahakama kuwa ameanza kuutumikia Uislam mwaka 1940 akiwa katika Anjuman Muslim na ilipokuja East African Muslim Society ( EAMWS) akawa kiongozi.

Akaeleza pia yeye ni muasisi wa Mabaraza ya Misikiti Duniani makao makuu yake Makka.

Akasema yeye Tabora ni mtu wa tatu kujiunga na TANU na katika Tanganyika ni mtu wa 264.

Sheikh Waikela akaeleza kuwa yeye alikuwa bega kwa bega na Nyerere katika kuipigania uhuru wa Tanganyika na akimchukua Nyerere ndani ya gari yake Tabora na wakila chakula nyumbani kwake.

Waikela aliichekesha mahakama aliposema wakati ule alikuwa kijana ana fedha na akicheza tennis.

Akaeleza kuwa Gavana Edward Twinning aliingiza fitna nchini kuhusu Waislam kutaka kuwachonganisha na Wakristo katika suala la elimu ili avunje juhudi za TANU kudai uhuru.

Nyerere alimsihi Waikela kuwa katika hutuba zake ajitahidi sana kuliweka suala hilo vyema ili pasiingie mtafaruku na nchi ikawa kama India na Pakistani Waislam na Wahindu wakagawana nchi katika misingi ya dini.

Waikela akasema hilo walilifanyia kazi na hali ikabaki shwari hadi uhuru ukapatikana.

Matatizo yakaja baada ya uhuru kupatikana.

Waikela akaieleza Mahakama jinsi Sheikh Hassan bin Amir alivyomtahadharisha kuhusu njama zilizokuwa zinapikwa serikali dhidi ya EAMWS na akamweleza kuwa wanafiki ndiyo wanaotumiwa.

Sheikh Waikela aliwataja Mahakamani wanafiki hao kwa majina mmoja baada ya mwingine.

Akaeleza mkutano wa EAMWS katika Ukumbi wa Aga Khan Girls mwaka 1963 alipomsomea Nyerere risala ya Waislam kuhusu fitna iliyokuwa ikienezwa nchini dhidi ya Waislam na Uislam.

(Risala hii kwa sasa ni maarufu inajulikana kama ''Moto wa Waislam Ukiwaka.'')

Anasema hotuba hii ndiyo iliyosabaisha yeye kuwekwa kizuizini mwaka uliofuatia 1964 na alipotoka jela alipewa hati ya kifungo ambayo Sheikh Waikela aliieleza Mahakama kuwa ameitundika nyumbani kwake ukutani kama pambo.

Mahakama ilifahamishwa kuwa mmoja wa washitakiwa ni binti yake aitwae Dentation Waikela ambae alizaliwa baba yake ikiwa jela.

Sheikh Waikela akaeleza jinsi Nyerere alivyowawezesha kundi la Adam Nasib kwa fedha na ushirikiano wa serikali kupita majimboni kuwashawishi Waislam kujitoa EAMWS lakini hawakufanikiwa.

Katika majimbo 20 ni majimbo 8 tu ndiyo yaliyokubali kujitoa.

Hata hivyo serikali ilikatumia nguvu na kuitisha mkutano wa wanasiasa Waislam Iringa na Bakwata ikaanzishwa na serikali ikaweka askari wenye silaha katika ofisi zote za EAMWS na kuzifunga na makufuli na minyororo.

Binafsi Sheikh Waikela akaeleza Mahakama kuwa alihongwa shs: 40, 000 na Geoffrey Sawaya aliyekuwa Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai, hongo ambayo aliikataa.

Hao waliokubali hongo ile ndiyo walioshirikiana na serikali katika kuiweka BAKWATA madarakani.

Kuhusu kiwanja cha Markaz Chang'ombe anasema kile kiwanja ni mali ya EAMWS na madhumuni yake ilikuwa ni kujenga Chuo Kikuu.

Kwa hakika alisema mengi na mwisho alimuomba hakimu awape Waislam haki yao



Tuesday, March 19, 2013

HOW GRANDCHILDREN PERCEIVE THEIR GRANDPARENTS !!!!

Posted here on 19/3/2013.

How children perceive their Grandparents……



1. She was in the bathroom, putting on her makeup, under the watchful eyes of her young granddaughter, as she’d done many times before. After she applied her lipstick and started to leave, the little one said, “But Grandma, you forgot to kiss the toilet paper good-bye!” I will probably never put lipstick on again without thinking about kissing the toilet paper good-bye….

2. My young grandson called the other day to wish me Happy Birthday. He asked me how old I was, and I told him, 80. My grandson was quiet for a moment, and then he asked, “Did you start at 1?”

3. A grandmother was telling her little granddaughter what her own childhood was like. “We used to skate outside on a pond. I had a swing made from a tire; it hung from a tree in our front yard. We rode our pony. We picked wild raspberries in the woods.”

The little girl was wide-eyed, taking this all in. At last she said, “I sure wish I’d gotten to know you sooner!”

4. When my grandson Billy and I entered our vacation cabin, we kept the lights off until we were inside to keep from attracting pesky insects. Still, a few fireflies followed us in. Noticing them before I did, Billy whispered, “It’s no use Grandpa. Now the mosquitoes are coming after us with flashlights.”

5. A second grader came home from school and said to her grandmother, “Grandma, guess what? We learned how to make babies today.” The grandmother, more than a little surprised, tried to keep her cool. “That’s interesting.” she said… “How do you make babies?”

“It’s simple,” replied the girl. “You just change ‘y’ to ‘i’ and add ‘es’.”

6. Children’s Logic: “Give me a sentence about a public servant,” said a teacher. The small boy wrote: “The fireman came down the ladder pregnant.” The teacher took the lad aside to correct him. “Don’t you know what pregnant means?” she asked.

“Sure,” said the young boy confidently. ‘It means carrying a child.”

7. A grandfather was delivering his grandchildren to their home one day when a fire truck zoomed past. Sitting in the front seat of the fire truck was a Dalmatian dog. The children started discussing the dog’s duties.

“They use him to keep crowds back,” said one child.

“No,” said another. “He’s just for good luck..”

A third child brought the argument to a close. “They use the dogs,” she said firmly, “to find the fire hydrants.”

8. A 6-year-old was asked where his grandma lived. “Oh,” he said, “she lives at the airport, and when we want her, we just go get her. Then, when we’re done having her visit, we take her back to the airport.”

9. Grandpa is the smartest man on earth! He teaches me good things, but I don’t get to see him enough to get as smart as him!

10. After putting her grandchildren to bed, a grandmother changed into old slacks and a droopy blouse, took her teeth out and proceeded to wash her hair. As she heard the children getting more and more rambunctious, her patience grew thin. Finally, she threw a towel around her head and stormed into their room, putting them back to bed with stern warnings. As she left the room, she heard the three-year-old say with a trembling voice,

“Who was THAT?”