Friday, October 22, 2010

MAMLAKA YA BUNGE YA KUMUONDOA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA CHINI YA IBARA YA 46A ya KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, 1977.

Ibara ya 46A YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, 1977; INAYOHUSU KUMUONDOA MADARAKANI (IMPEACHMENT) RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA. katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 [Cap. 2 R.E. 2002.] Leo hii Ijumaa 22/10/2010) - Somo la Katiba [Constitutional Law]

ZOEZI HILI HUCHUKUA JUMLA {KAMA KILA KITU KINAKWENDA SAWA - ceteris paribus} YA SIKU 150 au miezi mitano.

Rais (Mhimili wa Utawala) anaweza kuondolewa madarakani chini ya Ibara hii kwa tuhuma za aina nne:
- kuvunja katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.
- Kukiuka Sheria ya Maadili ya Viongozi [Leadership Code]
- Kukiuka vipengele vilivyomo katika maadili yanayohusu uandikishwaji wa vyama vya Siasa yaliyotajwa katika Ibara ya 20 (2) ya Katiba, au
- Amekuwa na mwenendo unaodhalilisha kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

1. Ili kuanzisha mchakato huo inahitaji idadi ya asilimia 20 (20%) ya Wabunge waliopo wafikishe Notisi ya maandishi na kuiwasilisha kwa Spika. Siku 30 zipite kabla ya kikao cha kujadili hizo tuhuma:

2. Baada ya kupita hizo siku 30, MTOA HOJA ATAIWASILISHA BUNGENI.

-Aidha tuhuma zitupwe au
- Wapendekeze kuunda Kamati ya Kuchunguza tuhuma hizo.

3. Bunge litapiga kura ili iundwe Kamati ya Kuchunguza tuhuma hizo; lakini kura hizo lazima zifikie au zizidi theluthi mbili ya kura zote. Kama ndio,

4. Spika anatakiwa kutaja majina ya Kamati ya Uchunguzi chini ya Ibara ya 46A(4) ambao ni:
(a) Jaji Mkuu (Mwenyekiti)
(b) Jaji Mkuu wa Zanzibar
(c) Wajumbe saba wanaoteuliwa na Spika; kwa kuzingatia Kanuni za Bunge na Uwakilishi wa Vyama vya Siasa Bungeni.

Matokea ya No. 3 hapo juu chini ya Ibara 46A (5) ni kwamba

- RAis anasimamishwa kazi
- Vivyo Ibara ya 37 (3) inafanya kazi. (Edapo Rais hatakuwepo madarakani wakati huo)

Jambo hili la kumsimamisha kazi Rais litaendelea hadi hapo Spika atakapomfahamisha Rais juu ya matokeo ya uchunguzi uliofanywa [Ibara ya 46A (5)]

Na. 4 hapo juu Kamati inapewa siku 7 kukamilisha uchunguzi wake na kumpa fursa Rais ya kujieleza [Ibara ya 46A (6)]

Kamati ya uchunguzi inapewa siku 90 kukamilisha ripoti yake na kuiwasilisha kwa Spika.

Ibara ya 46A (8) - Spika anawasilisha Ripoti ya Uchunguzi kwa Bunge

Ibara ya 46A (9) - Bunge lenye idadi isiyopungua theluthi mbili litajadili Ripoti hiyo na kumpa Rais fursa ya kujieleza.

Bunge linatakiwa liibuke na aidha ya majibu yafuatayo:

(i) Kwamba tuhuma zimethibitishwa.
(ii) Kwamba Rais hafai kuendelea kufanya kazi
(iii) Kwamba Rais hafai kuwa Rais
(iv) Kwamba tuhuma hazikuthibitishwa.

Ibara 46A(10) - Baada ya hilo kufanyika, endapo ni (i) Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatakiwa kuachia ngazi (resign) ndani ya siku tatu.

MCHAKATO HUO WOOOOTE ULIOTAJWA HAPO JUU UKIFUATAWA KAMA UNAVYOTOLEWA kisheria unatakiwa kumalizika ndani ya siku 150 sawa sawa na miezi 5 kamili.

JAMANI, HILI KWELI LINAWEZEKANA AU IBARA YA 46(A) ya Jamhuri ya Muungano wa TAnzania imewekwa kiini macho tu kwa sisi walalahoi wa Tanzania tuendelee kuota kwamba tukifanyikwa kinyume na Ibara hii basi rais ataendelea kupeta tu???????? Nasema hivi kwa sababu mchakato mzima ni mgumu na hauna mwelekea wa kufanikiwa hasa ikingatiwa idadi ya wabunge husika wa mchakato huu!!!!!!

TUANGALIE UTARATIBU WA MAMLAKA YA BUNGE KUMUONDOA MADARAKANI (REMOVAL) RAIS, PIA KWA SABABU HIZO HIZO HUKO KATIKA NCHI YA JAMHURI YA AFRIKA YA KUSINI (REPUBLIC OF SOUTH AFRICA)
Ifahamike wazi hapa kwamba Kumuondoa Rais kwa Katiba ya Jamhuri ya Tanzania ni "impeachment" wakati katika Jamhuri ya Afrika ya Kusini ni "Removal". Haya ni maneno mawili tofauti japokuwa matokeo au hatima ya michakato yake ni moja; ya kumuondoa mtu madarakani.

Chini ya Katiba yao ya mwaka 1996; Sheria Na. 108 ya Jamhuri ya Afrika ya Kusini; Ibara ya 89 (1) inasema hivi Kiingereza:

"The National Assembly by a resolution adopted with a supporting vote of at least two thirds of its members, may remove the President from office only on the grounds of -

(a) a serious violation of the Constitution or the law;
(b) serious misconduct; or
(c) inability to perform the functions of office.

Tafsiri ya Kiswahili ya Ibara hiyo ni hii hapa:

"Bunge linaweza kumuondoa rais madarakani kwa kutoa Azimio litakayokubaliwa kwa kupigiwa kura na angalau theluthi mbili ya wabunge wote. Rais anaweza kuondolewa madarakani kwa sababu zifuatazo tu:
(a) Kosa kubwa la Kuvunja katiba ya nchi au sheria;
(b) Mwenendo unaodhalilisha [serious misconduct]
(c) Kushindwa kutekeleza majukumu yake ya kazi ya ofisi hiyo.

Ibara ya 89 (2) inasema kwamba yeyote atakayeondolewa chini ya Ibara ya 89 (1) kutokana na sababu (a) au (b) anaweza kunyimwa mafao yote yaendanayo na ofisi hiyo; na pia anaweza kupoteza sifa ya kufanya kazi katika wadhifa mwingine wowote ya umma.

Vipengele hivi katika Katiba ya Jamhuri ya Afrika ya Kusini havitaji muda wowote kutoka kutolewa Azimio hadi kumuondoa madarakani. Kwa maneno mengine, jambo hilo linaweza kufanyika ndani ya muda mfupi iwezekanavyo.

Ibara ya 35 (3) ya Katiba ya Jamhuri ya Afrika Kusini, inayozungumzia haki za mshitakiwa inasema kila mtuhumiwa ana haki ya kupata kuhukumiwa ipasavyo; inayojumlisha haki ya:

(a) Kufahamishwa kosa lake kikamilifu ili aweze kujitetea
(b) Kupewa muda wa kutosha na nyenzo za kuweza kujitetea.
(d) Kupata haki ya kusikilizwa kwa wakati bila kucheleweshwa(zote hizi ni sehemu ya haki ya Kusikilizwa kikamilifu)

Kwa hiyo vipengele hivi vitatu vikifuatwa barabara, hata hivyo, nina hakika haitachukua siku 150 kwa shauri hilo kufikia tamati. Yawezekana pegine kuchukua mwezi mmoja au miwili, bila shaka kutegemea na shutuma zenyewe na uendeshaji wa kesi hiyo.

TAMKO LA FEM-ACT KUHUSU TISHIO LA SERIKALI DHIDI YA TAMWA NA VYOMBO VYA HABARI TANZANIA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Posted here on 23/10/2010

TAMKO LA FEMACT KUHUSU TISHIO LA SERIKALI DHIDI YA TAMWA NA VYOMBO VYA HABARI 21/10/2010

Sisi Mashirika yapatayo 50 yanayotetea Usawa wa Kijinsia, Haki za Binadamu, Maendeleo na Ukombozi wa Mwanamke Kimapinduzi (FemAct) tunalaani kauli ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo, kuwatishia wanaharakati kuwa wasizungumzie masuala ya uchaguzi. Katika kipindi hiki kuelekea Uchaguzi Mkuu 2010, tumebaini dhamira na hatua za makusudi za Serikali kukiuka haki za binadamu kwa kutishia na hatimaye kunyamazisha sauti za vyombo vya habari na raia; mtu mmoja mmoja, wanafunzi wa elimu ya juu, asasi za kiraia, na makundi mengine ya kijamii yanayotoa elimu ya uraia kwa lengo la kuhakikisha Tanzania inapata viongozi bora na kuendelea kuongozwa kidemokrasia, na kujihakikishia mabadiliko chanya wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 31, 2010.



Kwa kuzingatia haki na wajibu wetu kama kiraia chini ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya 1977, kunako Oktoba 6, 2010 tulitoa tamko kwa vyombo vya habari tukilaani kitendo cha vyombo vya usalama vikiongozwa na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) kuingilia mchakato wa uchaguzi jambo ambalo lingeweza kusababisha vitisho dhidi ya wananchi, vurugu na hatimaye kuchafua hali ya amani na usalama ambayo ni tunu ya Tanzania.



Vyombo vya habari, kwa kuzingatia maslahi ya umma, vilichapisha na/au kutagangaza Tamko la FemAct. Tumeshangazwa kusikia Serikali kupitia kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamadauni na Michezo Ndugu Seth Kamuhanda akikishambulia Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA), ni mwanachama wa mashirika ya FemAct, kwamba kwa kutoa tamko hilo TAMWA imeacha malengo yake na inajihusisha na siasa. Tunaona kuwa kitendo cha Serikali kutishia na kuishambulia TAMWA ni sawa na kutishia na kushambulia FemAct na watanzania wote kwa ujumla. Huu ni uonevu usiostahili kuvumiliwa. Ni jambo la kushangaza zaidi kuona Serikali inajiingiza katika masuala ya kampeni za uchaguzi wakati washiriki rasmi wa kampeni za uchaguzi, kwa mujibu wa sheria, ni vyama vya siasa.



Kadhalika tumesikitishwa na kitendo cha Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo kutishia kuyafungia magazeti ya Mwananchi na Mwanahalisi, ambayo yamekuwa yakitoa taarifa za matukio ya uchaguzi kama vyombo vingine vya habari, kwa kwa madai kwamba yanaandika habari za uchochezi dhidi ya serikali iliyoko madarakani. Aidha tunalaani hatua ya Serikali kukifungia kituo cha Redio SAUT FM cha Mwanza.



Tunapenda serikali ifahamu kuwa FemAct tunaendelea kufuatilia na watanzania wako macho dhidi ya hujuma yoyote itakayotokea kufifisha sauti za wananchi zinazochagiza na kuhimiza kupanua uelewa, uhuru na ushiriki wa wananchi katika kampeni za Uchaguzi Mkuu na hatimaye kupata uangavu wa kutosha kuchagua viongozi wanaojali na kusimamia maslahi ya wananchi na taifa kwa ujumla. Tunatoa wito kwa wananchi kuunganisha nguvu zao na kudai uwajibikaji kutoka serikalini na kwa viongozi tuliowaweka madarakani.



Ibara ya 18 na Ibara ya 20 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatamka na kusimamia uhuru wa kutoa maoni na uhuru wa kujumuika. Haki hizi zimetolewa ufafanuzi katika kesi mbali mbali ikiwamo kesi maarufu ya BAWATA. Katika kesi hii, uhuru wa kujumika umefafanuliwa na tabia ya viongozi kufungia mashirika ya kiraia bila kufata taratibu vimekemewa hata na mahakama kuu ambayo nayo ni chombo cha Katiba kilichopewa jukumu la kusimamia haki kwa wananchi.



Madai yetu:-

1. Serikali iache kutishia mashirika ya kijamii na mtu mmoja mmoja katika kipindi hiki cha uchaguzi kwa madai kuwa wanaingilia masuala ya kisiasa. Wananchi wana haki ya kutoa maoni na mawazo mbadala kwa maslahi ya Taifa.

2. Serikali irejee maamuzi ya Kesi ya “BAWATA” juu ya haki ya wananchi kujumuika na izingatie sheria za nchi kabla ya kufanya maamuzi ya kutoa karipio au vitisho kwa taasisi za kiraia na vyombo vya Habari. Utawala bora unahimiza watanzania wote wakiwemo viongozi wetu tunaowapata kwa demokrasia kuzingatia sheria za nchi.

3. Tunahimiza wananchi kuwa macho na viongozi wanaotaka kutumia nguvu nyingi kuziba midomo wananchi na kuendelea kuwa macho kulinda na kutetea maslahi ya taifa wakati wote.

4. Sisi kama mashirika yasiyo ya kiserikali tutaendelea kufanya kazi ya kutoa elimu ya uraia kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi bila kuogopa wala kupendelea mtu yeyote wala chama chochote cha siasa.



MUNGU IBARIKI TANZANIA

.












Ananilea Nkya
Executive Director
Tanzania Media Women's Association (TAMWA)
P. O. Box 8981, Sinza-Mori
Dar es Salaam, TANZANIA
Tel: +255-22 2772681 Fax +255 22 2772681 E-mail:ananilea_nkya@yahoo.com
Cellphone:+255-754-464-368

UFUNGAJI WA RADIO YA ST. AUGUSTINE UNIVERSITY (saut) TANZANIA

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA - 23/10/2010.

TANZANIA COMMUNICATIONS REGULATORY AUTHORITY

PUBLIC NOTICE

CLOSURE OF RADIO SAUT FM IN MWANZA FOR INTERFERING WITH

AERONAUTICAL COMMUNICATIONS.

The Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA) would like to inform the

general public that on 23rd August, 2010 ordered Radio SAUT FM in mwanza to close

down due to harmful interference with aeronautical communications to levels that

threaten the safety of aircrafts. The order to close the station was not due to political

reasons as alleged by Majira Newspaper of September 23rd, 2010 a story carried on

page 4 headlined “TCRA yaifungia Radio SAUT”.

The closure of the Radio Station was done after a technical investigation was carried

out by experts from TCRA, Tanzania Civil Aviation Authority (TCAA) and Radio SAUT FM

who found that the Radio was broadcasting on frequency 118.2 to 119.3 instead of

frequency 96.2 MHz assigned to them by TCRA. The frequency 118.2MHz to 119.3MHz

were giving out superous emissions interfering with aeronautical communications.

It should be NOTED that TCRA, cannot compromise the safety of aircrafts using

Tanzania airspace in conformity with national and international standards that when

interference occurs between other forms of communications like the radio station and

aeronautical communications, the immediate action is to close down the radio station

for safety reasons.

Radio SAUT FM, was directed to rectify this anomaly by installing filters to eliminate

unwanted signals, tuning its broadcasting equipments to operate within its assigned

frequencies and avail the station to the Authority for inspection before reopening the

radio station.

Issued by

DIRECTOR GENERAL
TANZANIA COMMUNICATIONS REGULATORY AUTHORITY

MUUJIZA WA UOKOAJI WA WACHIMBA MADINI WALIOFUNIKWA NCHINI CHILE

Miner Miracle

Date: 14/10/2010
By MICHAEL WARREN The Associated Press

SAN JOSE MINE, Chile — The last of the Chilean miners, the foreman who held them together when they were feared lost, was raised from the depths of the earth Wednesday night — a joyous ending to a 69-day ordeal that riveted the world. No one has ever been trapped so long and survived.
Luis Urzua ascended smoothly through 2,000 feet of rock, completing a 221/2- hour rescue operation that unfolded with remarkable speed and flawless execution. Before a jubilant crowd of about 2,000 people, he became the 33rd miner to be rescued.
The rescue exceeded expectations every step of the way. Officials first said it might be four months before they could get the men out.
It turned out to be 69 days and about 8 hours.
Once the escape tunnel was finished, they estimated it would take 36 to 48 hours to get all the miners to the surface. That got faster as the operation went along, and all the men were safely above ground in 22 hours, 37 minutes.
The rescue workers who talked the men through the final hours were being hoisted one at time to the surface.
The crowd in “Camp Hope,” down a hill from the escape shaft, set off confetti, released balloons and sprayed champagne as Urzua’s capsule surfaced, joining in a rousing miners’ cheer. In Chile’s capital of Santiago, hundreds gathered in Plaza Italia, waving flags and chanting victory slogans in the miners’ honor.
In nearby Copiapo, about 3,000 people gathered in the town square, where a huge screen broadcast live footage of the rescue. The exuberant crowd waved Chilean flags of all sizes and blew on red vuvuzelas as cars drove around the plaza honking their horns, their drivers yelling, “Long live Chile!”
“The miners are our heroes,” said teary-eyed Copiapo resident Maria Guzman, 45.
One by one through- out the day, the men had emerged to the cheers of exuberant Chileans and before the eyes of a trans- fixed globe. While the opera- tion picked up speed as the day went on, each miner was greeted with the same boisterous applause from rescuers.
‘Welcome to life’
“Welcome to life,” Chilean President Sebastian Pinera told Victor Segovia, the 15th miner out. On a day of superlatives, it seemed no overstatement.
They rejoined a world intensely curious about their ordeal and certain to offer fame and jobs. Previously unimaginable riches awaited men who had risked their lives going into the unstable gold and copper mine for about $1,600 a month.
The miners made the smooth ascent inside a cap- sule called Phoenix — 13 feet tall, barely wider than their shoulders and painted in the white, blue and red of the Chilean flag. It had a door that stuck occasion- ally, and some wheels had to be replaced, but it worked exactly as planned.
Beginning at midnight Tuesday, and sometimes as quickly as every 25 minutes, the pod was lowered the nearly half-mile to where 700,000 tons of rock collapsed on Aug. 5, 2010 and entombed the men.
Then, after a quick pep talk from rescue workers who had descended into the mine, a miner would climb in, make the journey upward and emerge from a manhole into the blinding sun.
The rescue was planned with extreme care. The miners were monitored by video on the way up for any sign of panic. They had oxygen masks, dark glasses to pro- tect their eyes from the unfamiliar sunlight and sweaters for the jarring transition from subterranean swelter to chilly desert air.
As they neared the surface, a camera attached to the top of the capsule showed a brilliant white piercing the darkness not unlike what accident sur- vivors describe when they have near-death experiences.
The miners emerged look- ing healthier than many had expected. Several thrust their fists upwards like prizefighters, and Mario Sepulveda, the second to taste freedom, bounded
out and led his rescuers in a rousing cheer. Franklin Lobos, who played for the Chilean national soccer team in the 1980s, briefly bounced a soccer ball on his foot and knee.
“We have prayed to San Lorenzo, the patron saint of miners, and to many other saints so that my brothers Florencio and Renan would come out of the mine all right. It is as if they had been born again,” said Priscila Avalos. One of her brothers was the first miner rescued, and the other was due out later in the evening.
Healthy — or not
Health Minister Jaime Manalich said some of the miners probably will be able to leave the hospital today — earlier than pro- jected — but many had been unable to sleep, wanted to talk with families and were anxious. One was treated for pneumonia, and two needed dental work.
“They are not ready to have a moment’s rest until the last of their colleagues is out,” he said.
As it traveled down and up, down and up, the rescue capsule was not rotating as much inside the 2,041-foot escape shaft as officials expected, allowing for faster trips.
The first man out was Florencio Avalos, who emerged from the missile- like chamber and hugged his sobbing 7-year-old son, his wife and the Chilean president.
No one in recorded his- tory has survived as long trapped underground. For the first 17 days, no one even knew whether they were alive. In the weeks that followed, the world was captivated by their endurance and unity.
Worldwide attention
News channels from North America to Europe and the Middle East carried live coverage of the rescue. Pope Benedict XVI said in Spanish that he “continues with hope to entrust to God’s goodness” the fate of the men. Iran’s state Eng- lish-language Press TV fol- lowed events live for a time. Crews from Russia and Japan and North Korean state TV were at the mine.
The images beamed to the world were extraordi- nary: Grainy footage from beneath the earth showed each miner climbing into the capsule, then disap- pearing upward through an opening. Then a camera showed the pod steadily rising through the dark, smooth-walled tunnel.
Among the first rescued was the youngest miner, Jimmy Sanchez, at 19 the father of a months-old baby. Two hours later came the oldest, Mario Gomez, 63, who suffers from a lung disease common to miners and had been on antibiot- ics inside the mine. He dropped to his knees after he emerged, bowed his head in prayer and clutched the Chilean flag.
Gomez’s wife, Lilia- nett Ramirez, pulled him up from the ground and embraced him. The couple had talked over video chat once a week, and she said that he had repeated the promise he made to her in his initial letter from inside the mine: He would marry her properly in a church wedding, followed by the honeymoon they never had.
The lone foreigner among them, Carlos Mamani of Bolivia, was visited at a nearby clinic by Pinera
and Bolivian President Evo Morales. The miner could be heard telling the Chilean president how nice it was to breathe fresh air and see the stars.
Carrier ‘palomas’
Most of the men emerged clean-shaven. More than 300 people at the mine alone had worked on the rescue or to sustain them during their long wait by lowering rocket-shaped tubes dubbed “palomas,” Spanish for car- rier pigeons. Along with the food and medicine came razors and shaving cream.
Estimates for the rescue operation alone have soared beyond $22 million, though the government has repeat- edly insisted that money is not a concern.
The men emerged in good health. But at the hospital in Copiapo, where miner after miner walked from the ambulance to a waiting wheelchair, it became clear that psychological issues would be as important to treat as physical ones.
Dr. Guillermo Swett said Sepulveda told him about an internal “fight with the devil” that he had inside the mine. He said Sanchez appeared to be having a hard time adjusting, and seemed depressed.
“He spoke very little and didn’t seem to connect,” the doctor said.
Chile has promised that its care of the miners won’t end for six months at least — not until they can be sure that each man has readjusted.

UTAJIRI WA LUGHA YA KISWAHILI

From: Chris Mwasambili
To: list@tanzanet.org
Sent: Thu, Oct 21, 2010 3:19 pm
Subject: [tanzanet] UTAJIRI WA KISWAHILI:Maneno ni mengi, kuyatumia tunashindwa

Imeandikwa na Barnabas Maro; Tarehe: 21st October 2010 Habari Leo

LUGHA ya Kiswahili ina maneno mengi lakini wengi wetu hatuyajui, kwa hiyo tunashindwa kuyatumia.

Matokeo yake tunachanganya maneno ya Kiingereza katikati ya Kiswahili na kufanya kile nikiitacho ’Kiswangereza.’ Sababu hiyo imewafanya baadhi ya watu kusema, kwa mfano, ”wanasiasa ’wanaboa’ kwa maneno yao” badala ya chusha, chukiza, sunza, udhi.

”Wasiasa wanachusha/wanachosha/ wanasunza/wanaudhi.” Hata kuomba radhi siku hizi watu husema ’sore’ (sorry) badala ya ’samahani’ ’kumradhi’ au ’niwie radhi.’ Wengine husema ”tukutane ’hom’ (home)” badala ya nyumbani.

Majuzi nikiwa ndani ya daladala, kijana fulani akiongea na mwenziye kwa simu alimwambia: ”Jana ’nimemwambia’ mkuu kuwa leo napitia benki kuangalia kama fedha zangu za kwenda chuoni zimeingia.”

Kila alipokuwa akielezea mambo yaliyopita alitumia neno ’nime ... ” badala ya ’nili ... .’ Hata nilipomwambia aseme ’nilimwambia’ badala ya ’nimemwambia’ kwa kuwa ni wakati uliopita (jana, juzi, n.k.) hakunielewa ila aliniangalia tu kwa dharau kama sanamu.

Alirudia kosa hilo kila alipozungumza. Kama mwanafunzi wa Chuo Kikuu anakosea na anaposahihishwa haoni wala kujutia kosa lake, itakuwaje kwa mwanafunzi wa msingi?

Kumbe ndio maana wanafunzi hushindwa mitihani ya Kiswahili ingawa ni lugha ya taifa! Kosa kama hili hufanywa na wazungumzaji wengine na waandishi kama ilivyo katika habari ifuatayo: ”Wakati Poulsen akisema hayo, wapinzani wake timu ya taifa ya Morocco ”Atlas Lions” wamewasili juzi usiku ... .”

Ingekuwa: ”Wakati Poulsen akisema hayo, timu ya taifa ya Morocco, Atlas Lions, iliwasili juzi usiku ... .”

Angalizo: Timu iliwasili juzi, jana (wakati uliopita). Kama ujio wake ni siku hiyohiyo, basi husemwa imewasili leo. Naomba wazungumzaji na waandishi wazingatie mambo ya wakati uliopita, uliopo na ujao.

Wengi husema, kwa mfano, ”mimi ’naamkaga’, ’nalalaga’, ’nakulaga’, ’nakwendaga’, ’namwambiaga’, ’nasemaga’.” Kwa ufasaha wa lugha husemwa huamka badala ya ’naamkaga’, hulala badala ya ’nalalaga’, hula badala ya ’nakulaga’, huenda badala ya ’nakwendaga’, humwambia badala ya ’namwambiaga’, na husema badala ya ’nasemaga’.

Baadhi yetu hutumia maneno bila kujua maana yake kama ilivyo katika sentensi ifuatayo: ”Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Deodatus Kinawiro amenusurika kupigwa mawe na wananchi wenye hasira katika kijiji cha Mtanila, baada ya gari lake alilokuwamo lenye namba za usajili STK 3770 kukoswakoswa kuvunjwa vioo kwa madai ya kujihusisha na kampeni za uchaguzi mkuu dhidi ya Chama Cha Mapinduzi.”

Moja kwa moja sentensi hii inaonesha kuwa mkuu wa wilaya ya Chunya, Deodatus Kinawiro alinusurika kupigwa na wananchi kwa kujihusisha na kampeni zinazokwenda kinyume na Chama Cha Mapinduzi.

Hata hivyo, sentensi inayofuatia inaeleza tofauti ingawa mwandishi ni yuleyule! ”Habari ambazo ... (jina la gazeti) imezipata jana zinadai kuwa DC huyo amekuwa akifanya kampeni katika kata na vijiji kadhaa kwa kofia ya serikali ili kuhakikisha kuwa mgombea wa CCM katika jimbo la Lupa, Victor Mwambalaswa, anapita kwa kishindo.”

Kosa kubwa la mwandishi huyu ni kutumia neno ’dhidi’ ambalo bila shaka haelewi maana yake. Kwa kumsaidia, maana ya ’dhidi’ (kivumishi) ni –enye kinyume na; -enye kupingana na; kushindana na; mbalimbali na.

Mwandishi ameandika: ”Habari ambazo (jina la gazeti) imezipata jana ...” si sahihi kwani ingekuwa ” ... ilizipata jana ... ” au ” habari ilizopata gazeti hili jana ... .”

Maneno mengine yanayotumiwa kuunda sentensi huleta maana potofu au sentensi kutokamilika ingawa huwa na nukta mwisho kuashiria sentensi imekamilika.

Tusome sentensi ifuatayo: ”Inashangaza katika uwanja huu ambao mimi ndio msimamizi mkuu na mwenye jukumu la kuhakikisha kwamba mambo yanakwenda vyema kama ilivyopangwa.”

Mwandishi ametumia maneno mengi na hivyo kupoteza nafasi na kuharibu sentensi. Ifuatayo ni sentensi iliyofanyiwa marekebisho:
”Katika uwanja huu mimi ndio mwenye jukumu la kuhakikisha mambo yanakwenda kama ilivyopangwa.”

Ni sentensi yenye maneno 13 dhidi ya 20 aliyotumia mwandishi. Hebu sasa tuingie kwenye methali. “Kanga hazai utumwani” maana yake kanga hatagi ugenini. Methali hii huweza kutumiwa kwa mtu anayeshindwa kufanya jambo lolote anapokuwa katika mazingira mageni.

Tunafunzwa kuwa ugeni una shida. Kangaja simle, mchuzi kitoweo. Kangaja ni aina ya samaki ambaye huwa na harufu mbaya lakini mchuzi wake huwa kitoweo kizuri.

Methali hii hutumiwa katika mazingira ambapo mtu fulani hampendi mwengine ingawa anafaidika na matendo yake. Huweza kumshauri mtu anayekataa kitu kizuri kinachotokana na mtu m-baya au mwenye sifa mbaya.

Msi chembe wala uta si muwani. Muwani ni anayepigana au anayepambana. Chembe ni kigumba cha mshale. Maana yake mtu asiye na chembe au uta si mpiganaji. Methali hii hutumiwa kutukumbusha kwamba lazima tujiandae vizuri tunapotaka kufanya jambo fulani.

Kwa kawaida kila jambo huwa na masharti yake ya kimsingi ambayo hatuna budi kuyatosheleza. Mathalan mwanasiasa mzuri lazima awe stadi (mtu aliye na uhodari au ufundi mkubwa wa kutenda jambo fulani; bingwa, farisi, galacha) wa kusema.

Kitendawili: Ngozi ndani nyama n-nje – Firigisi ya kuku. marobarnabas@yahoo.com

Sunday, October 17, 2010

USAFIRI MPYA WA MAHUJAJI KUANZIA 2010

30-day test run for Makkah metro

http://arabnews.com/saudiarabia/article152577.ece/REPRESENTATIONS/large_620x350/sau_train.jpg

A Makkah metro train during a test run. (AN photo)

By P.K. ABDUL GHAFOUR | ARAB NEWS

Published: Oct 2, 2010 23:44 Updated: Oct 3, 2010 00:33

JEDDAH: The newly established Mashair Railway, which links the holy sites of Mina, Arafat and Muzdalifa with Makkah, will have a 30-day test run before opening to transport domestic and GCC pilgrims during the upcoming Haj season.

Municipal and Rural Affairs Minister Prince Mansour bin Miteb will inspect the railway (also known as the Makkah Metro) on Tuesday to make sure the facility is ready to transport the guests of God. The railway will bring about a dramatic change in pilgrim transportation between the holy sites.

Established at a cost of SR6.5 billion, the new railway will have a capacity to transport 72,000 pilgrims in an hour. Nine stations have been constructed in Arafat, Mina and Muzdalifa, each having three stations. This is the second largest project implemented by the Ministry of Municipal and Rural Affairs after the SR4.5 billion high-tech Jamrat Bridge project in Mina.

Habib Zain Al-Abidine, deputy minister of municipal and rural affairs, said the railway will have 10 trains in the first phase, each with a length of 300 meters. “Each train will carry 3,000 passengers.”

He said Saudi authorities have not yet fixed the fare. “The matter is in the hands of Second Deputy Premier and Minister of Interior Prince Naif, chairman of the Supreme Haj Committee. Once the prince gives his directives, we’ll announce the fare,” he said.

The time for transporting pilgrims from Arafat to Muzdalifa will be reduced to five minutes on the 9th of Dul Hijjah when the faithful will move together from the plain of Arafat to Muzdalifa. And another five minutes will take them from Muzdalifa to Mina on the 10th.

Zain Al-Abidine said the railway would operate throughout the year.

The second phase of the project will link Mashair Railway with the Grand Mosque in Makkah with a station on Umm Al-Qura Road. It will also be linked with the Haramain Railway that connects Makkah with Madinah and Jeddah.

The trains will have a test run covering 6,000 km each before starting regular operations. The first test run took place last Thursday. The railway will have 20 trains in the next stage, each with 12 carriages and each carriage holding 250 passengers. About 20 percent of passengers will be seated while 80 percent will be standing. Trains will have a speed of 80 to 120 km/hour.

RASILIMALI ADIMU ZA TANZANIA NA DUNIANI

Imeandikwa na Beda Msimbe; Tarehe: 14th October 2010 Habari Leo

MSITU WA MAZUMBAI WA LUSHOTO, TANZANIA

Eneo la kupumzikia wageni wa SUA ndani ya msitu wa Mazumbai.

NDANI ya milima ya Usambara kuna misitu miwili mikubwa inayotumika kwa utafiti.

Misitu hiyo ni ya Amani na Mazumbai. Msitu wa Amani upo Muheza na ule wa Mazumbai upo Lushoto. Nilifika msitu wa Mazumbai wenye
ua linalopatikana kiasili Tanzania pekee, ‘African Violet’.

Nilikuwa sijawahi kuona ua la African Violet, lakini nilipata kulisoma sana katika mtandao na nilipofika Mazumbai kitu cha kwanza kuuliza na kutaka kuoneshwa ni ua hilo, Meneja wa Hifadhi ya Msitu wa Mazumbai, Said Kiparu alikuwa zaidi ya tayari kunionesha, yalikuwa yamepandwa nje ya nyumba ya kupumzikia iliyo hapo.

Nyumba hiyo hutumika na watu wanaozuru msitu huo pamoja na watafiti na siku ambayo nilifika kulikuwa na wazungu kadhaa waliofika
kutalii na walitarajiwa kuwapo hapo kwa siku nne au zaidi walikuwa msituni wakivinjari.

Kuwapo kwa ua hilo si tu fahari ya Tanzania, lakini ua hilo lenyeugumu mkubwa wa kuota na kumea lililopewa jina na Mjerumani mmoja aliyepeleka taarifa kwao kuhusu kuwapo kwa ua hilo la urujuani wakati akivinjari milima ya Usambara.

African Violet au tuseme Ua la Usambara ambalo wenyeji wa Usambaani huliita ‘Dughulishi’, lilijulikana kwa Wazungu mwaka 1892 kupitia Baron Walter von St. Paul na tangu wakati huo mpaka leo zaidi ya aina 20 za maua haya zimebainika.

Kusema kweli pamoja na kutawanyika kwa African violet duniani, Wazungu wanatambua kwamba makao yake makuu yapo Usambara wakati wakielezea historia ya maua hayo ambayo watu wengi wa Ulaya hupenda kuyaweka majumbani kwao kutokana na uzuri wake.

Kwa historia, Baron huyu ambaye alikuwa na hisia za masuala ya mimea ya bustani (unaweza kumuita botania) ndiye aliyewezesha mimea hii kufika Ulaya kwa kumtumia baba yake Baron Ulrich von Saint Paul-Illare, ambaye wakati huo alikuwa ni Rais wa chama cha miti nchini Ujerumani (Dendrological Society of Germany).

Juhudi hizo zilifanya kuanzia mwaka 1893 ua hilo kupatikana nje ya usambara na watu kuanza kulizalisha kwa wingi kwa kutumia mbegu hizo zilizotoka Tanzania.

Sehemu kubwa ya maua ya African Violet katika bara la Ulaya na Marekani si orijino ni haibridi. Kimsingi ua hilo lilitawanyika dunia kupitia Ujerumani na pamoja na kupendwa sana Marekani yalifika huko mwaka 1926 yakitokea Ujerumani.

Sasa hivi nchini Marekani kuna jumuia nyingi zinazojihusisha na African Violet. Botani huyu Baron Walter von Saint Paul, alikuwa ni Gavana wa Kijerumani jimbo la Kaskazini Mashariki la Tanganyika na aliyaona maua hayo yakijiotea katika vipenyo vya majabali.

Ndani ya Msitu wa Mazumbai ambao kimsingi unamilikiwa na Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) na kutumiwa nadra na watalii lakini sana na watafiti kuna zaidi ya maua, ipo miti aina tofauti zaidi ya 100 ambayo inamea vyema ikiangaliwa isifanyiwe
uharibifu.

Watu wa SUA walikabidhiwa msitu huo na mzungu anayeitwa John Tanner ambaye alikuwa na mashamba yake ya chai katika eneo hilo na aliitunza misitu ya asili aliyopukuta kwa sababu za shughuli yake aliyokuwa akiifanya.

Mzungu huyo aliyezaliwa Tanga mwaka 1918 aliishi Mazumbai kuanzia mwaka 1946 hadi mwaka 1982, kwa sasa yupo nchini kwao Uswisi na habari zinasema yungali hai.

Kuwapo mashamba ya chai kunaonesha kwa nini kulikuwa na misitu kwani utengenezaji wa chai hutumia miti mingi kwa hiyo kulikuwa na haja ya kuwa na miti ya kutosha (misitu) kwa ajili ya kazi hiyo.

Ndani ya msitu huo pia mzungu huyo alikuwa ametengeneza mfumo wa kufua umeme ambao ndio unaotumiwa hadi sasa na nyumba ya SUA kupata nishati. Umeme huo wa maji unaofuliwa katika nyumba kuukuu ni moja ya vivutio ambavyo vinaweza kutoa taswira ya neema katika harufu nzuri ya misitu na maua yake.

Ndani ya msitu huo mnene yapo magogo makubwa ambayo yamechomoza kwa namna inayopendeza zaidi, ingawa huwezi kuona kila kitu kilichopo katika msitu huo pamoja na nyoka wa aina mbalimbali, ndege, kuna mandhari inayokonga moyo hasa kwa wale wanaopenda asili na vitu vinavyofuatana navyo.

Kuna miti ambayo mizizi yake iliyojitokeza nje ina urefu wa zaidi ya futi tano ikitengeneza mandhari ya kustaajabisha zaidi. Ni kama jengo lililofumwa. "Hii ni hifadhi, inasaidia vitu vingi sana na watu hawaruhusiwi kuingia ndani ya msitu na kuvuna," anasema Meneja Kiparu.

Akaongeza kwamba, pamoja na kuwatembeza watalii ni kazi yao kutoa nafasi ya watu kujifunza masuala ya misitu na namna hifadhi
inavyoweza kuokoa misitu na katika hilo watafiti wa ndani na nje hufika kujifunza kwenye msitu huu ambao kimsingi ulikuwa binafsi.

Katikati ya msitu huu wa hifadhi wa hekta 300 kuna mbega na ndege mbalimbali ambao hupendezesha sauti katika msitu unaozizima kwa utulivu.

Thursday, October 14, 2010

HABARI ZA UHALIFU WA KIMAFIA TANZANIA HIZI HAPA

Mengi awalipua polisi



• ABAINI NJAMA ZA KUMBAMBIKIA MWANAE DAWA ZA KULEVYA DAR

TANZANIA DAIMA LA Jumatano, 13 Oktoba 2010

na Mwandishi wetu



MWENYEKITI Mtendaji wa makampuni ya IPP, Reginald Mengi, amedai kubaini njama chafu za kutaka kumbambikia mwanae dawa za kulevya.

Mengi alifichua njama hiyo jana katika mkutano wake na waandishi wa habari, uliofanyika ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

Akifafanua kisa hicho cha kusikitisha, Mengi alisema mpango huo umefadhiliwa na mmoja wa watu aliopata kuwataja siku za nyuma kwamba ni mafisadi papa, kutokana na kujihusisha na matukio ya ufisadi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT).



Waliotajwa na Mengi katika sakata hilo lililotikisa nchi ni pamoja na mfanyabiashara mwenye asili ya Kiasia, Yusuf Manji, Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, Jeetu Patel, ambaye kwa sasa anakabiliwa na kesi ya EPA mahakamani na Tonil Sumaiya.



Huku akizungumza kwa kutulia na kujiamini, Mengi alisema mfanyabiashara huyo ambaye hakumtaja jina, amefadhili mkakati huo kwa kuwahusisha baadhi ya maofisa wa polisi wa ngazi ya juu nchini na Polisi wa Kimataifa (Interpool) ambao kila mmoja angelipwa dola za Marekani 40,000, sawa na sh milioni 47.



Kwa mujibu wa Mengi, mpango huo ambao umegharimiwa kwa sh bilioni tatu, pia umewahusisha maofisa wawili ambao hakuwataja majina kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere na maofisa kutoka kampuni moja ya simu za mkononi nchini.

Akisimulia mpango mzima wa mkakati huo, Mengi alidai kuwa siku ya tukio, mwanae akiongozana na watu wengine wanne, walitarajiwa kusafiri hadi nchini India kwa shughuli za kikazi.

Alisema walipofika katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere, alipambana na mazingira ya ajabu na hatimaye kujinasua kwenye mtego uliosukwa ili wamnase na dawa za kulevya.



“Kwa mapenzi ya Mungu, kijana wangu alibaini mbinu hiyo chafu na kwa mapenzi ya Mungu aliahirisha safari. Tulipofanya uchunguzi, tukabaini mpango huo na kuwajua wahusika ambao nitawataja pamoja na kiasi cha fedha walichoahidiwa na walichokwisha kuchukua kama malipo ya awali kwa kazi hiyo haramu,” alisema Mengi.



Mfanyabiashara huyo maarufu nchini, aliwataja aliodai kuhusika katika mpango huo kuwa ni pamoja na Kamishna wa Polisi Msaidizi wa kitengo cha kukabiliana na dawa za kulevya, Godfrey Nzowa, aliyeahidiwa dola za Marekani 40,000, sawa na sh milioni 47 na kulipwa dola za Marekani 20,000, sawa na sh milioni 23.5.



Mwingine ni ofisa wa polisi, Charles Mkumbo na polisi wa Interpool, aliyemtaja kwa jina moja la Henry. Wote waliahidiwa kiasi kama hicho cha Nzowa na kupata malipo ya awali yanayofanana.



“Mkumbo alionekana kwenye ofisi za mfanyabiashara huyo akiwa anaendesha gari lake aina ya Rav4, lenye rangi ya silver, siku hiyo ya Septemba 26, majira ya saa nne asubuhi na alikwenda kuchukua malipo yake ya awali,” alisema Mengi.

Watuhumiwa wengine katika mpango huo ni maofisa wawili wa Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere na ofisa kutoka kampuni moja ya simu za mkononi ambao hata hivyo hakuwataja kwa majina. Hao wanadaiwa kuahidiwa sh milioni 15 na wote walilipwa malipo ya awali ya sh milioni saba kila mmoja.



Mengi alisisitiza kuwa anajua anachokisema na amejiandaa kutoa ushahidi wa kutosha, hivyo aliwataka wahusika waende mahakamani ili akatoe ushahidi zaidi juu ya mpango huo aliouita kuwa ni wa kigaidi.



“Huu ni unyama, maisha ya mwanangu na heshima yangu ingekwisha, kwani kila mmoja angesema Mengi ni muuzaji wa dawa za kulevya. Namfamu mwanangu, hana tabia hiyo na hawezi kujihusisha na biashara hiyo haramu na kama mtego huo usingegunduliwa, huo ungekuwa mwisho wa maisha ya mwanangu,” alisisitiza Mengi.



Mengi alisema Jeshi la Polisi linafanya kazi nzuri na analiheshimu, lakini alidai kuna watu wachache wanaotaka kuharibu heshima ya jeshi hilo.

“Ndani ya Jeshi letu la Polisi, kuna viongozi wazuri, waadilifu, ukianzia na IGP Mwema, wasaidizi wake, kina Kamanda Venance Tossi, Suleiman Kova, Elias Kalinga, Chilogile na wengine, ni wachapa kazi wazuri, waadilifu, lakini wapo wachache kwa sababu ya tamaa ya fedha, wanataka kuliharibu jeshi letu,” alisema Mengi.



Akijibu tuhuma hizo, Nzowa, kwanza alishangaa kusikia taarifa hizo na kuongeza kuwa katika kipindi alichotaja Mengi alikuwa nje ya nchi kikazi.

“Kwanza mimi katika kipindi anachotaja Mengi sikuwepo nchini. Lakini pia sijui kama Mengi au huyo mwanae wananijua. Binafsi huyo mwanae wala simjui, sasa sijui nimehusikaje hapa,” alisema Nzowa.

Kamanda huyo wa kikosi cha kudhibiti dawa za kulevya nchini alisema kauli ya Mengi ina lengo la kumchafulia, kwani kiasi anachokitaja ili kumhujumu mwanae ni kidogo sana ikilinganishwa na ahadi alizowahi kupewa na wahalifu, lakini alizikataa na kusimamia misingi ya sheria.



Kwa upande wake, Kamanda Mkumbo, naye aliruka ‘kimanga’ kwamba hajawahi wala hawezi kuthubutu kumbambikia dawa za kulevya mtu, kwa sababu ya kulipwa pesa.



“Mimi kwanza huyo mtoto wa Mengi simjui na hata sasa sijui tuhuma hizi zinatokea wapi. Hata mbele ya Mwenyezi Mungu niko tayari kukana kuhusika na mpango huo,” alisema.



Kamanda huyo alisema anashangazwa zaidi kuhusishwa na Nzowa kwenye mpango huo, kwani vitengo vyao havihusiani kikazi.



Chanzo: Gazeti la TanzaniaDaima

Wednesday, October 13, 2010

UCHAGUZI TANZANIA 2010 MAMBO!

PIMAJOTO INAZIDI KUPANDA KWA KUSINGIZIWA WAPINZANI ETI WATAMWAGA DAMU? KWA KUTUMIA NINI?
WAMWAGAJI DAMU NI CCM TOKA KILOMBERO, MWEMBECHAI, PEMBA, etc.

Kwa nini wanatisha wananchi na wakati vyombo vyote vya mitulinga viko mikononi mwao? Someone is afraid - really afraid!!

By the way, ni utawala gani wanaofanya ambao Watanzania wengine hawawezi?
Kugawiana nyumba za serikali?
Kuiba fedha zetu BOT?
Kugawa mashirika yetu kwa wageni?
Kutumia bilioni 150 kwa mwaka kwenye usafiri wa Presidency?
Kujipangia mishahara ya milioni 10 kwa viongozi?
Kupeana sitting allowance za board meetings za 1 million per day?
Kuachia boda boda na mabasi kufanya barabara zetu ni machinjoni?
Kusinzia bungeni na kupiga piga makofi kwenye kila kikao?
Kuruhusu magogo na pembe za ndovu kupitishwa barabara zetu na kupakiwa melini na kupelekwa nje mchana mchana?
Kuhakikisha Tanzania na haswa Zanzibar imekuwa key transhipment ya drugs from the middle and far east to South Africa, Europe and US? Kuuziwa radar ya million 28 kwa 40?
Kushindwa kumaliza kesi yoyote ya EPA ambao ushahidi uko wazi tangu 2006?
Kuwaachia wageni kuendeleza kila sekta ya uchumi na kujisifu ndio maendeleo?
Kuwagawia watoto wa mfalme wa Saudia ekari mamilioni ya ardhi yetu kulima?
Kudumisha mgawo wa umeme tangu wakati wa Mkapa hadi leo?
Kuagiza kampuni feki (Richmond) ya kuuza vitabu kutununulia injini la ndege bovu feki eti kufua umeme?
Kwenda kununua mvua Thailand?
Rais kujiuzia mgodi wa mkaa wa mawe na mtambo wa kufua umeme Kiwira?
Kusimamia uchumi bei ya mchele toka 600 hadi 1500 in 4 years
Sukari toka 800 hadi 1600 (3000 Mbambabay) in 4 years?
Petroli toka 750 hadi 1800?
Shilingi toka 1000 hadi 1500 kwa dola moja?
Kununua magari ya viongozi ya milioni 200+?
Kufelisha karibu nusu ya wanafunzi wa kidato cha nne?
Kuzalishia mama zetu sakafuni na wagonjwa 3 kuchangia kitanda kimoja?
Kupeleka watoto India au Afrika Kusini kufanyiwa dialysis wakati machine zinauzwa dola 10,000?
Kuua Air Tanzania?
Kuwepo kwa foleni ya masaa 3 toka Kimara kwenda mjini?
Give me a freakin break!! Kujijengea makasri hapo Migombani Street sio kuongoza nchi.

Kwa utawala wa namna hiyo heri vijana wa Chuo Kikuu wangeweza kuongoza nchi hii kuliko hii serikali ya sasa. Kukopa hela na kuweka barabara kadhaa lami na nyingine changarawe ndio ingemshinda Lipumba?

Sunday, October 10, 2010

MATATIZO YA ELIMU KATIKA NCHI ZINAZOENDELEA

UNIVERSITIES IN EAST AFRICA HAVE UNQUALIFIED LECTURERS ! Daily News, Tanzania 10/10/2010

From MARC NKWAME in Arusha, 9th October 2010 @ 12:00, Total Comments: 0, Hits: 247

The Executive Secretary of the Inter-University Council for East Africa, Prof Chacha Nyaigotti-Chacha is worried over the mushrooming of universities not corresponding with the available number of qualified lecturers.

A university lecturer must qualify to the top; anybody teaching at higher institute of learning needs to be a PhD holder, but at the moment our universities seem to have just one doctorate lecturer in every 40 dons.

"As a result our colleges keep churning out half-baked graduates," Prof Chacha maintained. The professor expressed this worry in Arusha over the weekend at a press conference held in the threshold of the forthcoming celebrations to mark the 10th Anniversary of the Revitalization of the Inter-University Council for East Africa, to be held in the Ugandan Capital of Kampala between the 19th and 21st October 2010.

Following the dissolution of the University of East Africa and the establishment of the University of Dar es Salaam, Makerere University and the University of Nairobi in 1970, an Inter-University Committee for East Africa was created under the East African Community (EAC), to facilitate collaboration among the three national universities.

"By then there were only three universities in the region. Now the number is staggering. Yet we keep having fewer and fewer trained professors to correspond with the trainers' demand," said Mr Chacha.

The committee functioned very well under the aegis of the Community and after the collapse of the latter body in 1977, in 1980, the three Vice-Chancellors agreed to maintain the committee through signing a Memorandum of Understanding (MoU), which led to the birth of the Inter-University Council for East Africa (IUCEA).

The MoU set out the objectives, functions, membership and governance of the Council. In 1999 the Partner States recognized the Inter-University Council as one of the surviving institutions of the former East African Community (EAC).

It was agreed to establish a corporate body to be known as the Inter-University Council for East Africa. At that time IUCEA was not a legal entity.

Following the revitalization and recruitment of a new set of staff in 2000, the Governing Board embarked on the development of legal instruments to make IUCEA a legal body corporate.
In 2002 the protocol for the establishment of the IUCEA was signed by the three partner States with the aim of harmonizing and providing a legal framework within which to undertake activities of the IUCEA.

Source:
http://www.dailynews.co.tz/home/?n=13685&cat=home