Sunday, February 28, 2010

K U Z E E K A

KUZEEKA - imechangiwa na dr. Wilbert Bunini Manyilizu wa Chuo Kikuu, Mzumbe, Tanzania.

* Kila mmoja anazeeka/ataazeeka

* Kuna tabia za kimwili na kiakili zinazoambatana na mchakato huu usioepukika wa kuzeeka

* Kasi ya kuzeeka hutofautiana kutoka mtu hadi mtu kutokana na sababu mbalimbali za kimaisha, mazingira, tabia, vyakula na kadhalika.


MABADILIKO YA KIMWILI WAKATI WA MKCHAKTO WA KUZEEKA

Tabia za kuzeeka Mwili huonekana mapema zaidi kuliko zile za kisaikolojia.
Uzee huanza lini?
Unapozaliwa tu unaanza kuzeeka. Japo kuzeeka halisi ni pale kukua kunapokoma.
Mchakato wa kuzeeka haraka au taratibu hutegemea mtu binafsi.
Uzee huja kwa kasi tofauti kati ya mtu na mtu na kwa viwango tofauti kati ya kiungo na kiungo katika mtu huyo huyo.
Kwa nini mtu anazeeka?
Nadharia za sayansi za mchakato wa kuzeeka zinaeleza kuwa:

1. Kadiri siku zinavyopita kuna upotevu wa chembe chembe zinazotengeneza mwili hasa mtu anapokuwa ametoka kwenye utoto au ujana na anaposimama kukua. Hii ni hali ya kurithi ambayo kila mtu ameumbwa nayo.

2. Baadhi ya chembe chembe kama vile zile za damu za ngozi, ubongo nakadhalika hazigawanyiki tena ili kuongezeka (yaani hakuna kukua tena).Kukua maana yake ni kuongezeka wingi wa chembe chembe za mwili na ubongo kunakotokana na kugawinyika kwake.

3. Chembe chembe kama za neva za fahamu, misuli nakadhalika zinapopotea kwa kuzeeka na kufa kunakotokana na kushindwa kugawanyika, hupotea milele.

4. Viunganishi ( ni kama jointi za matofali ya nyumba= matofali ni chembe chembe) vya chembe chembe za mwili katika viungo vyote kama vile kwenye ngozi, misuli, ubongo nakadhalika. Tishu hizi ambazo ni viunganishi vya chembe chembe hukakamaa na kupoteza uwezo wake wa asili na kukatika kwa kukomaa, hivyo kubakia jointi dhaifu kwa kuunganisha chEmbe chembe. Hii huonekana wazi sana kwenye ngozi inapozeeka na kubakia tepetepe.

Pia tukumbuke kuwa takataka au makapi yanayotokana na michakato mbalimbali ndani ya mwili huharakisha kuzeeka kwa chembe chembe kwa kuwa na sumu na kemikali ambazo hazikutolewa kwa wakati na hivyo huchangia kuzeesha na kuchosha chembe chembe na kuzifanya zife kwa kukosa huduma bora zikilinganishwa na zile chembe chembe zisizozeeka.

MABADILIKO YA KAWAIDA YA MCHAKATO WA KUZEEKA

MACHO

1. Macho huanza kuonesha dalili za kushindwa kuona vizuri kati ya umri wa miaka 30 mwishoni na 40 mwanzoni. Macho huendelea kupungua nguvu zaidi na zaidi kadiri mtu anavyoendelea kuzeeka. Mtu hulazimika kukunja uso au kuweka ukurasa wa maandishi mbali akijitahidi kuona vizuri.

2. Kadiri mtu anavyozeeka lensi ya jicho hupoteza uwezo wake wa kulengesha mwanga unaotoka nje ya jicho kwenda kwenye retina ambako ndiko kuliko mlango unaoenda kwenye ubongo kunakotoa tafsiri ya kitu kilichopo mbele ya macho kama ni mtu, gari, mti na kadhalika.

3. Ukubwa wa tundu dogo linaloonekana jeusi kwenye jicho (pupil) hupungua kwa kukakamaa sababu hupoteza mnyambuliko (flexibility) kadiri mtu anavyozeeka hivyo kuruhusu mwanga kidogo sana kupitia lensi kwenda kwenye retina. Hivyo mtu hujaribu kukodoa macho na kukunja uso ili kuruhusu mwanga mwingi bila mafanikio kwani uzee ndio ulioleta matatizo hayo. Tatizo hili mtu huliona zaidi anapokuwa akiangalia kwenye mazingira ya mwanga mdogo sana kama vile anapoendesha gari usiku. Macho huchoka sana na uso huanza kuzoea kukaa katika mkazo huo na hatimae huanza kubadilika uso na kuwa na makunyanzi tofauti na wakati wa ujana wakati hapakuwa na ulazimishaji wa kuona.

4. Ulengaji wa kuona na kulenga (focusing) hupungua mtu anapozeeka na usahihi wa kuona kitu kwa mipaka, rangi na sura kwa uzuri hupungua. Uwezo wa kuona vitu vya pembeni vya jicho pia hupungua na kumlazimisha mtu huyu kugeuza shingo ili kuona kitu ambacho angeona bila kugeuza shingo, hasa wakati wa giza.

5. Uwezo wa kuona rangi pia hupotea kidogo kidogo kadiri ya umri unavyosonga mbele.

MASIKIO

1. Hupoteza uwezo wa kusikia sauti kali bali nafuu huwepo kama sauti zikiwa kubwa lakini za pichi ya chini.

2. Sauti ambayo wazee husikia vizuri wakati mwingine huonekana kero kwa vijana walio na masikio yanayosikia vizuri.

3. Maneno yakichanganywa na muziki na sauti zingine kidogo husababisha tatizo la kutokuelewa ujumbe kwa kadiri mtu anavyozeeka. Huwapo nafuu ya kuelewa na kufuata maongezi kama vyombo vya sauti zingine tofauti na maongezi vitazimwa kwa ajili ya mzee. Vyombo hivyo ni kama redio, runinga, ngoma au maongezi pembeni.

4. Vitu hivi kama vitaendelea kusikika huleta ghadhabu ya haraka na tafsiri tofauti kwa mzee kama vile huonesha kumdharau, kutokumheshimu na kadhalika.

5. Matokeo yanayojitokeza kwa mzee kwa kutokuzingatia haya ni pamoja na mzee huyo kutofurahia maongezi, kuzira (Kususa), malalamiko, kujitenga na kujenga dunia ya upweke. Hamu ya chakula hupotea na afya hudhoofu zaidi. Mzee huyu huendelea kuumia ndani kwa ndani na hivyo kinga yake dhidi ya maradhi huporomoka kwa kasi kutokana na msongo wa mawazo ambayo ni matatizo ya akili. Vyote hivi huongeza kasi ya kuzeeka na hatimaye kupoteza maisha.


LADHA YA CHAKULA NA HARUFU

1. Milango ya kupokea Ladha ya chakula hudhoofika na kushindwa kupeleka taarifa za ladha ya chakula kwenye ubongo kwa kadri mtu anavyozeeka. Hii hujitokeza mtu anapofikia miaka ya hamsini, hii huendelea hivyo hadi miaka sabini ambapo wazee wengi hupoteza sehemu kubwa ya milango hii na hivyo kuwa na matatizo ya kula.

2. Tatizo kubwa la wakati wa uzee ni ulaji wa tabu ambao husababisha afya kudhoofika sana hasa wasipokuwa na wasimamizi wa utaratibu wa chakula na aina za vyakula wapendavyo wazee wenyewe.

3. Matatizo ya ulaji yanaweza kuwa makubwa sana kama kuna tatizo la upendo na huduma hafifu anazoona mzee. Wazee huzira kwa urahisi wanapoona hawathaminiwi na kujiona hawana faida na kuona heri wafe badala ya kuendelea kusumbua watu. Hulalamika, hukata tamaa na kupoteza hamu ya kula. Hali hii pia huathiri milango ya ladha ya chakula.

4. Uwezo wa (kunusa) milango ya kupokea harufu nzuri na mbaya ya chakula kudhoofika na kushindwa kugundua chakula kizuri cha kutia hamu ya chakula.

FOUR LIFESTYLE STEPS TO A HEATHY HEART

4 Lifestyle Steps to a Healthy Heart
Tip of the Day 2/28/2010 by Dr. Weil (www.drweil.com)


Maintaining the right mix of healthy lifestyle habits is the best way to achieve optimal cardiovascular function. Incorporate the following into your daily routine to help promote the health of your heart:

1. Exercise. Regular exercise helps maintain the health of blood vessels, strengthens the heart muscle itself, and can help reduce heart disease risk factors including high cholesterol, high blood pressure, insulin resistance, and stress. Aim for 30 minutes a day of moderate aerobic activity on most days of the week. For individual guidance, consult a personal trainer.
2. Lose weight. If you are overweight or obese, even modest weight loss can significantly lower cardiovascular risks.
3. Don't smoke. Smoking is the major preventable risk factor for heart disease, and has negative health consequences for your entire body, from your taste buds to your energy levels to your skin. Seek support and guidance in quitting.
4. Manage stress. Uncontrolled stress can raise blood pressure, cholesterol levels, and homocysteine levels. Practice breath work, meditation, guided imagery, visualization or another relaxation technique, and participate in regular moderate exercise (including yoga and T'ai chi), stay social, and laugh often.

Thursday, February 25, 2010

MGOMBEA BINAFSI CHAGUZINI TANZANIA

25/2/2010

MAZOWEYA YA MHIMILI WA UTAWALA TANZANIA KUKEJELI, KUDHARAU, KUBEZA NA KUDHIHAKI MHIMILI WA UTOAJI HAKI (MAHAKAMA)

1. Katika Kitabu kiitwacho LAW AND JUSTICE IN TANZANIA: QUARTER OF A CENTURY OF THE COURT OF APPEAL, kilichohaririwa na Peter, C.M. na Kijo-Bisimba, H. (2007), aliyekuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa [CAT] na ambaye sasa ndiye Jaji Mkuu wa Tanzania, Mheshimiwa Augustino Ramadhani aliandika makala iitwayo “Twenty Five Years of the Court of Appeal of Tanzania and the Establishment of the East African Court of Justice” [Miaka 25 ya Mahakama ya Rufaa Tanzania na Uanzishwaji wa Mahakama ya Afrika Mashariki] ianziayo ukurasa 223 wa kitabu hicho.

Katika Ukurasa wa 227 ametoa maeneo matatu ya Maagizo ambayo Mhimili wa Utawala (The Executive) nchini Tanzania umeshindwa kutekeleza kutokana na tabia yake ya kudharau, kubeza, na kudhihaki Mhimili wa Utoaji haki kama ifuatavyo:

1. Malipo ya Mafao kwa Majaji Waondolewao Madarakani

Katika hili Mahakama ya Rufaa ilishauri kuwepo na Orodha ya Makosa yanayomnyima Mafao Jaji atiwaye hatiani au Chombo kinachotoa hukumu hiyo (tribunal) kitamke endapo Jaji Mkosaji anastahili au hastahili malipo ya mafao (terminal benefits) katika kesi ya MOSES J. MWAKIBETE V THE PRINCIPAL SECRETARY (Estab.) AND THE ATTORNEY GENERAL, Court of Appeal of Tanzania at Arusha, Civil Appeal No. 27 ya 1992 (haikuripotiwa).

Hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa na Serikali hadi wakati wa kuchapishwa kitabu hicho mwaka 2007 toka mwaka 1992.

2. Malipo ya Mawakili wa Kujitegemea Wateteapo Wahalifu Kwa Mujibu wa Sheria

Mahakama ya Rufaa ilipendekeza mwaka 1991 kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali [AG] (Andrew Change – Bwana Vijisenti) kupitia upya malipo haya yaliyolipwa kati ya Tshs.120/= na Tshs.500/=; wakati huo ikilinganishwa na kiasi cha chini ya nusu dola ya Kimarekani ($).

AG hakuwahi kutekeleza agizo hili hadi miaka mitano (5) baadaye wakati CAT ilipoamua yenyewe kuongeza kiasi hicho hadi kufikia Tshs.100,000/= kwa kutumia fursa iliyojitokeza katika kesi ya THE ATTORNEY GENERAL V N.I.N. MUNUO NG’UNI [1998] TLR 464.

3. Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984

CAT ilipendekeza masuala ya kutafsiri Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 na masuala mengine nyeti ya Kikatiba yasiyofikishwa CAT kwa uamuzi yatazamwe na yafikiriwe kubadilishwa katika kesi ya SEIF SHARIFF HAMAD V SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR (SMZ) [1998] TLR 48.

Jambo hili halikufanyiwa kazi na miaka mitano (5) baadaye CAT ikalikumbusha pendekezo lake kwamba Mamlaka zinazohusika pande mbili za Muungano zichukue hatua za makusudi kuoanisha vipengele viletavyo migongano ndani ya Katiba zote mbili; ile ya Zanzibar ya mwaka 1984 na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977. HAYA HAYAJATEKELEZWA.
[mwisho wa sehemu iliyoandikwa na Jaji Mkuu)



4. MTAFARUKU ULIOPO SASA WA MGOMBEA BINAFSI
Ijumaa, Februari 12, 2010, Bw. Philip Marmo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, alisema kuwa katika uchaguzi mkuu ujao suala la kuwepo Mgombea binafsi kama ilivyoamuliwa na Mahakama Kuu tarehe 5 Mei, 2006 na kufafanuliwa na CAT tarehe 20 Februari, 2010, haliwezi kupata nafasi kwa kuwa muda wa maandalizi hautoshi.

Kauli hiyo ililenga kukejeli, kupinga, kudharau, kuasi na kubeza tamko la Mahakama ya Rufaa la Feruari 10, 2010 lililobariki amri iliyotolewa na Mahakama Kuu tarehe 5 Mei, 2006.

Maelezo kama hayo pia yameshatolewa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dk. Werema, na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (National Electoral Commission [NEC]).

Saturday, February 20, 2010

MTOTO ALELEWA NA NYANI TANZANIA !!!

Date: Thursday, 20 November, 2008, 11:43 M MAJIRA NEWSPAPER, TANZANIA.

Mtoto Baraka Rose (11) aliyelelewa na nyani akiandika majina yake mbele ya waandishi wa habari Dar es Salaam jana. Kulia akionesha kovu la risasi mguuni alilojlipata katika harakati za kuachanishwa na nyani mlezi wake mwaka 2005. (Picha na Richard Mwaikenda)

Na Gladness Mboma

WATANZANIA wameombwa kujitokeza kumsaidia kielimu mtoto Bahati Baraka Rose (11) ambaye anadaiwa kulelewa na nyani baada ya kutupwa porini akiwa mchanga wilayani Bukombe, Shinyanga.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kimanga, Tabata, Bw. Pastory Kyombya, alisema mtoto huyo kwa sasa analelewa na Bibi Rose Mbwambo wa Kimanga.

Alisema Bibi Mbwambo alikabidhiwa mtoto huyo na Serikali wilayani Bukombe baada ya kufuata taratibu zote za kiserikali.

Alisema Katibu Tawala wa Wilaya ya Bukombe, Bw. Richard Nhende, ndiye aliyemkabidhi Bibi Mbwambo mtoto huyo ili amlee baada ya kumwomba.

Bw. Kyombya alisema mtoto huyo anaomba kupelekwa shule kama anavyoshuhudia wenzake wakienda shule na kuwaomba wasamaria wema wajitokeze kumsaidia ili aanze shule mwakani.

Naye Bibi Mbwambo alisema alimchukua mtoto huyo Agosti mwaka huu akiwa kwenye biashara zake Bukombe.

"Nilikuwa nimepanga kwenye nyumba ya kulala wageni ya Neema, nikiwa na wenzangu, mama mmoja (hakumtaja jina) ambaye alikuwa akitupikia chakula alitujia na kutueleza matatizo aliyonayo mtoto Baraka.

"Nilimwonea huruma sana Baraka, baada ya mama huyo kutuelezea historia yake nzima na kwamba hana ndugu na maisha yake ni ya kutangatanga na kututaka tumsaidie," alisema.

Alisema yeye binafsi aliingiwa na huruma ndipo alipofuata taratibu zote za kumchukua mtoto huyo na kuja naye Dar es Salaam kumlea.

Bibi Mbwambo alisema atamtunza mtoto huyo kama anavyotunza watoto wake ila aliomba wasamaria wema kujitokeza kumsaidia ili aanze masomo mwakani ikiwezekana shule ya bweni.

Alisema mtoto huyo alilelewa na nyani miaka kadhaa porini kabla ya kuchukuliwa tena na binadamu baada ya nyani huyo mlezi kuuawa kwa risasi.

Bibi Mbwambo alisema inadaiwa mtoto huyo aliokotwa na nyani akiwa kwenye mfuko wa 'rambo' akiwa mchanga na kumlea kwa miaka mitano.

"Askari wa wanyamapori wa Ushirombo, Bukombe, ndio waliofanikisha kupatikana kwa mtoto huyo baada ya siku moja kumwona nyani akimnyonyesha.

"Hata hivyo, inadaiwa askari hao walipata shida kumchukua mtoto huyo baada ya nyani mlezi kukimbia naye mara zote kila alipokuwa akiwaona, hivyo kuchukua muda mrefu kumpata," alisema.

Alisema mtoto huyo aliendelea kulelewa na nyani huyo hadi alipofikisha umri wa miaka mitano na baadaye askari hao kumvamia tena ili kumnyang'anya mtoto huyo na kusababisha vurugu kubwa kati yao na nyani mlezi.

Bibi Mbwambo alisema katika vurugu hizo, askari walimfyatulia risasi nyani huyo na kumuua huku risasi moja ikimpata mtoto huyo kwenye kidole cha mguu wa kushoto.

Alisema askari hao walimchukua mtoto huyo na kumpeleka katika hospitali ya Bukombe ambako aliendelea kulelewa hospitalini hapo.

Bibi Mbwambo alisema watu mbalimbali walikuwa wakimchukua mtoto huyo na kumlea na walioshindwa walikuwa wakimrudisha hospitalini hapo, lakini msamaria mwema alimchukua, lakini mtoto huyo alimtoroka na kuingia mitaani na kuishi maisha ya shida.

Alisema Baraka alikwishazoea kuishi maisha ya porini, akiparamia miti na kusababisha wasamaria wema waliokuwa wakimlea kulazimika kumfunga minyororo ili asitoroke.