Friday, February 20, 2009

Thursday, February 19, 2009 3:16:46 PM GMT -05:00 US/Canada Eastern
Subject: Re: [tanzanet] HIZI NDIO ELIMU ZA VIONGOZI WAKO - Imechangiwa na Mwalimu Joseph Mbele (mbele@stolaf.edu)

Ndugu

Jakaya Kikwete tulisoma wote Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Alikuwa mwaka moja mbele yangu. Tulimchangua kuwa rais wa jumuia yetu ya wanafunzi, Dar es Salaam University Students' Organization (DUSO). Alipata shahada yake pale, mwaka 1975.

Nilikuwepo siku alipotunukiwa shahada ya heshima ya udaktari na chuo kikuu cha St. Thomas, hapa Minnesota. Hiki ni chuo maarufu. It is not a joke kama joke zingine tunazozisikiaga. Na citation ambayo uongozi wa chuo ulitoa kama msingi wa kumtunuku Jakaya Kikwete shahada hiyo ilikuwa nzito. Sio jokes kama hizi za wabunge.

Na baada ya kutunikiwa hii shahada, Rais Jakaya Kikwete alitoa hotuba nzito, iliyoacha gumzo. He really and effectively spelled out the condition of Tanzania and Africa, challenges and opportunities. Having outlined our potential, he argued, very effectively, that what we need is partnerships, sio handouts.

Sijawahi kusikia mtu huku Marekani akihoji uhalali wa JK kutunukiwa hili digirii. Sana sana watakaokuwa wanahoji ni wateja wa vijiwe vya Bongo :-)


No comments:

Post a Comment