Tuesday, August 21, 2012

MAONI YA KATIBA KWA TUME YA KATIBA NA. 1MAONI YA KATIBA NA. MOJA – 20/8/2012 Ibara Na. 1 ya Katiba ya 1977: Napendekeza Tanzania iwe nchi ya mfumo wa “Federation” rasmi ili kuondoa kero na manunng’uniko yote ya pande zote mbili za Muungano. Kwamba nchi ya Tanganyika ipatikane kama ilivyokuwa zamani kabla ya tarehe 26/4/1964, na iwe nchi kamili. Zanzibar tayari ipo na iendelee kuwa nchi kamili. Nchi hizi mbili zipige kura ya Maoni [Referendum] ili watu wake waseme endapo wanataka waendelee kuwa katika Muungano au waachane na mfumo huo. Ili endapo zitakubaliana kuwa na Muungano, nchi hizi zikutane katika Federation ya Tanzania [TZ] (au jina lolote litakaloamuliwa na wananchi). Binafsi napendekeza jina hilo hilo libaki lakini tukiwa katika Federation. Kwa hiyo Dola ya TZ iwe ni muungano wa nchi mbili zilizo huru za Tanganyika na Zanzibar. Hata nchi nyingine yoyote itakapo kujiunga na TZ ruhsa; endapo tu itakubaliana na matakwa ya watu wa TZ, huenda hilo likawa ndio chimbuko la Muungano wa Nchi za Afrika (United States of Africa). Mtindo huu wa DOLA utasaidia kuzihamasisha nchi nyingine za jirani Barani Afrika kutamani kujiunga katika Federation yetu; endapo tu tutaendesha mambo yetu kwa kufuata HAKI na UTAWALA WA SHERIA. Kwa wakati huu niandikapo maoni haya (20/8/2012), nchini Tanzania hakuna haki tangu tupate UHURU tarehe 9/12/2012. Hii ni kwa sababu sehemu moja ya jamii ya Watanzania imejilimbikizia haki ya kuamua nchi iendeshwe vipi na hivyo kuwafanya watu wa sehemu ya pili kuwa kama raia wa Daraja la Pili ndani ya nchi yao. Mifano ya kuthibitisha jambo hili ni mingi mno na kwa uchache niliyowahi kuithibitisha binafsi (kwa kunitokea mimi mwenyewe au kwa kuisoma katika maandiko ya kitaaluma) ni kama ifuatayo: 1. Hulka ya wafuatao imani ya Kikristo ya kufundishana chuki dhidi ya watu wenye imani za dini nyingine; hasa Waislam. Hili linathibitishwa na mifano kadhaa ifuatayo. 2. Tabia ya ukiristo kujikita katika mamlaka za utumishi wa umma na kulazimisha nembo zao kutumika maofisini na hivyo kuwafanya watu wa dini nyingine kujisikia kubaguliwa kwa makusudi; jambo linalopingana kabisa na Ibara ya 13 (1) ya Katiba ya 1977. Mfano dhahiri wa jambo hili ni kupamba Maofisi ya Umma wakati wa sikukuu kwa alama za Krismasi [Miti mikubwa Sebule za Ofisi na kuipamba kwa “Chrismas Carols” na kutoa zawadi za pombe kwa maofisa mbalimbali maofisini]; kuweka “Compact Disks” [CD] za miziki ya dini ya Kikristo wakati wote maofisini na kuiliza kana kwamba wawekaji miziki hiyo wako Kanisani au wako majumbani kwao badala ya Ofisi za Serikali ISIYOKUWA NA DINI. 3. Nyimbo hizi na alama nyingine kuwekwa wazi maofisini kunakiuka kwa uwazi Ibara ya 3(1) inayotamka kwamba Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi isiyokuwa na Dini. 4. Ndani ya Katiba Mpya, mambo haya yaandikwe na yapigwe marufuku kwa sababu yanawabagua Watanzania kutokana na imani zao. 5. Mwezi Mei, 2012 usahihishaji wa mitihani ya Wanfunzi wa Kiislam ulichakachuliwa na wanafunzi hawa wote wakaonekana wamefeli somo la “Islamic Knowledge” ili wasipate sifa za kuweza kuomba kuendelea na masomo ya juu zaidi. Jambo hili lilipogunduliwa ETI likarekebishwa na srikali. Tangu UHURU 9/12/2012 mchezo huu umeendelea kuchezwa na Wakristo dhidi ya Waislam kwa sababu huko nyuma Mwalimu Lila alithibitisha hili. Yeye akiwa kama mmoja wa wasahihishaji wa mitihani ya wanafunzi wa sekondari, aligundua watahiniwa wa Kiislam wanakatwa maksi zao na kufelishwa kwa makusudi mazima na alipouliza wenziwe katika jopo la Wasahihishaji alijibiwa kuwa “hivyo ndivyo tunavyofanya katika kipindi cha misimu yote ya kusahihisha mitihani, kwani wewe hujui?”. Alipolalamika hakuna kilichofanyika. 6. Waislam walipolalamikia hili, Rais aliyepita Benjamin William Mkapa (1995 -2005) aliwahi kusema kwamba zipo sababu za kihistoria kwamba wasomi wengi zaidi nchini Tanzania ni Wakristo kuliko Waislam na kwamba anataka apelekewa ushahidi (empirical evidence) kama kweli Waislam wanafanyiwa madhila haya makusudi ili wafeli. Je, ni ushahidi gani zaidi alioutaka Mkapa zaidi ya ule wa Mwalimu Lila? Serikali haikufanya lolote baada ya kugunduliwa hili. Imelipalilia na kulikubali liendelee. 7. Jambo la kuwa Watanzania tunapendana binafsi; Watanzania tuna umoja wa kwenye damu kwa kuoleana kokote nchini Tanzania; Watanzania tunaoana japo kuwa tuko katika dini tofauti; yote ni kiini macho cha kupendezesha baraza; mapenzi haya hayako moyoni mwa Watanzania. Watanzania hatupendani kama makundi tofauti ya imani tofauti. Ukweli huu wa kubaguliwa kinaga ubaga (kwa kufelisha Waislam) kunawafanya Waislamu wajisikie ni raia wa Daraja la 10 na wala sio la Pili nchini mwao. 8. Kusutwa kwa nafsi ya Rais Benjamin William Mkapa na kuruhusu kutolewa majengo ya Umma ya Chuo cha Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) mjini Morogoro, mwaka 2004 kuwa Chuo Kikuu cha Waislam, hakusaidii kufuta makovu ya madonda ya madhara na madhila yanayowapata Waislam ndani ya nchi yao. 9. Kitendo cha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kushindwa kuwa na asasi zake yenyewe za kuhudumia Umma wa Watanzania wote na badala yake kutoa RUZUKU (zitokanazo na kodi za Watanzania wote) maradufu kwa Wakristo kujijengea huduma hizo na kuwa ni mrija wa utajirisho wao; kwa kuwa huduma hizi ni za kibiashara; ni ubaguzi mwingine unaohisiwa kwa uchungu sana na Waislam. 10. Katika Baraza la Maulid la mwaka 2012, kauli ya Rais wa sasa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais Jakaya Mrisho Kikwete mjini Dodoma kwamba ETI Waislam hawajaomba RUZUKU hizo ni tusi kubwa kwa sababu ushahidi upo dhahiri wa maandishi wa Waislam kuomba Ruzuku hizo mwaka 1961. Jambo hili alilofanya Rais Kikwete kwa Waislam linafanana na kauli ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Andrew Chenge alipotamka mwaka 2010 kwamba shilingi zaidi ya bilioni mbili ni vijisenti tu. Tofauti ni kwamba Kikwete katukana Asasi nzima ya Uislam (kama mfumo wa maisha); wakati Chenge alitukana Watanzania kwa ujumla wao; masikini na matajiri pia. 11. Katiba mpya iweke ibara zitakazotoa usawa katika kutoa ruzuku au ifute ruzuku zote husika. Isiegemee upande mmoja. 12. Habari zote chanya za Waislam kufumbiwa macho na vyombo vyote vya habari nchini – Viwe vya umma au vya binafsi. Kinachotangazwa kuhusu Waislam ni upotoshaji wa habari zao, sana sana kwamba Waislam ni waanzilishi wa vurugu na kwamba hawataki maendeleo. 13. Habari zote chanya za Wakristo kupambwa kwa vichwa vya habari vilivyokoloea (screaming headlines) na kuzificha zile zilizo hasi kwa wasomaji ili ionekane kwamba Wakristo ndio wapenda maendeleo na hawana matatizo wala migogoro baina yao katika Dhehebu mojamoja au kati ya madhehebu tofauti. 14. Tabia ya Asasi nyingi za Umma kupanga mikutano yao muhimu sana ya maamuzi (Kama ya Bodi, ya Mabaraza ya wafanyazi, ya Wadhamini, n.k.) siku za Ijumaa ili AIDHA Waislam wasiihudhurie; au muda wa saa moja watakapokuwa na udhuru wa kwenda kusali, ndio maamuzi yatayowaathiri vibaya; au maamuzi mazito yawahusuyo yachukuliwe. Huu ni ubaguzi mbaya wa kumuengua mjumbe Mkutanoni kwa sababu ya imani yake. Yaani Muislam achague abaki mkutanoni ili atetee masilahi yake ya kidunia au akaabudu Mola wake na aachane na mambo yamhusuyo yeye na jamii yake duniani. Huu ni ubaguzi USIOONEKANA. Lugha waitumiayo wajumbe wa imani nyingine katika mikutano kama hii ni kwamba “Sacrifice Ijumaa hii tu” maana yake “fuata njia na utamaduni wangu na achana na huo wa kwako”. Mikutano hii muhimu isipangwe siku za kuabudia dini yoyote katika sala za pamoja (congregational prayers). Huu ni ubaguzi wa kimya kimya dhini ya Ibara ya 13 ya Katiba ya 1977 kwa ujumla wake. 15. Walimu wa Kikristo toka Chekechea, Msingi, Sekondari hadi Vyuo Vikuu kuwa na tabia ya kuwanyanyasa, kuwabagua, kuwatweza, kuwadharau, kuwapuuza, n.k. wanafunzi wasio wa dini yao. Siku hizi hata wanafunzi wa shule za misingi huliongelea jambo hili. Maana yake ni kuwa wanafanyiwa ubaguzi huo kwa dhahiri na sio kisiri tena. Watoto wanajengewa chuki baina yao yaani wa dini moja na wa dini nyingine, dhidi ya Ibara ya 13 ya Katiba ya 1977. 16. Shule za Kikristo zinakaribisha maombi toka kwa wanafunzi wa dini zote kwa kigezo cha kuziendesha kibiashara bila ubaguzi wowote. Kivitendo; shule hizi; kama ilivyokuwa shule za Mkoloni na za Makanisa toka kabla ya Uhuru; zinalazimisha Waislam kula nguruwe na kutowahudumia wakati wa hitajio maalum la mwezi wa Mfungo wa Ramadhani, na kuwapiga mafuruku kushiriki katika ibada ya pamoja ya Ijumaa. St. Scholarstica (iliyopo Moshi) ni mfano mzuri sana wa hili kwa sababu jirani yangu aitwaye Abdulrazak Luwinzo watoto wake wawili wanasoma huko na wamemsimulia hili lililowakuta mwezi wa Ramadhani ulioishia tarehe 20/8/2012 (kwa kuwa watoto wamerudi wamekondeana kwa likizo ya Sensa ya 2012), na yeye amenisimulia mimi jana tarehe 19/8/2012. 17. Tabia ya Ukristo kung’ang’ania kuwa siku ya mapumziko ni Jumapili tu wakati watu wa dini nyingine wana siku zao za mapumziko ambazo hazitambuliwi kama siku za mapumziko kama Ijumaa kwa Waislam. Na wala haitoshi kutoa muda wa kwenda kuabudu/sala kwa pamoja kwani hiyo hailingani na kutoa mapumziko kwa siku nzima. Wakristo na wapumzike Jumapili na Waislam wapumzike Ijumaa. 18. Katiba mpya iseme wazi uhuru wa kuchagua siku ya mapumziko kwa imani zote. 19. Tabia ya Wakristo kukataa katakata uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi nchini Tanzania kwa mujibu wa imani ya Dini ya Kiislam. Wakati nchi ya Tanzania imerithi mfumo wa sheria za Kikoloni za Dola la Uingereza ambalo sheria zake zimetokana na chimbuko la Kanisa (Ecclesiastical courts) na ndizo zitumikazo kwa watu wote; lakini Dola kwa shinikizo la Wakristo, linapuuzia dai la Waislam la kuwa na Mahakama yake ya Kadhi iliyokuwepo huko nyuma (kabla ya kuvunjwa miaka ya sitini – 1960s) na ikigharimiwa na Dola. Usawa wa kuhudumia watu wake unapotea wakati sheria za Tanzania zimerithi mfumo wa sheria za Kanisa na Waislam wanakataliwa Dola yao isigharimie Mahakama yao kana kwamba hawachangii kodi zao. 20. Katiba mpya iandike kuruhusu kuwepo kwa Mahakama ya Kadhi itakayogharimiwa na Dola kama ilivyokuwa huko nyuma na mambo yalikwenda vizuri kwa imani zote. 21. Tabia ya Wakristo wengi kukasirikia Vazi la Stara la Kiislam kana kwamba wameligharimia wao linawakera sana Waislam. Wengine wanafikia hata kuwaita Waislam hao (pamoja na mimi) na “kuwanasihi” waache au wabadilishe vazi hilo ili wavae kama wanavyovaa wao. Kwa Waislam vazi hilo ni sehemu ya Ibada. Wasijisikie vibaya watu wa dini nyingine kutimiza amri za Mola wao ili mradi hawavunji sheria hizo za Dola za urithi wa Kikanisa. 22. Kuruhusu MAPAMBIO [nyimbo za kidini ya kikristo] hata katika shughuli/tafrija za umma zilizoandaliwa na serikali ambako haitakikani kuwa hivyo kwa sababu serikali haina dini. Badala yake pasiwepo hata nyimbo kama hizo zinazoingiza hisia ya kubaguliwa kwa watu wa imani nyingine. 23. Katiba mpya iseme kwamba jambo hili ni marufuku. 24. Pendekezo la kuingiza katika Katiba Mpya jingine ni kuwa midhali Tanzania kwa mahesabu ya sense ya sasa ya “kusadikika” ni kuwa tuko wananchi wa imani kuu mbili wenye asilimia sawa (asilimia 32 kwa 32), basi Katiba Mpya iseme kwamba katika kila Nyanja ya Utumishi wa Umma pawepo na uwakilishi wa 50-50 ili kuondoa hizi hisia za kubaguliwa, kubaguana, chuki za dhahiri na za siri dhidi ya Waislam wa Tanzania. 25. Mambo yote haya yana haki zote za kuwekwa wazi na kuzungumzwa na kujadiliwa kinaga ubaga, bila ya kuficha kitu ili kila mtu ayafahamu na ajue kisa na sababu ya watu wa imani moja katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wanadai haki zao kila uchao; haki ambazo hazitimizwi na serikali yao. 26. Historia inatufahamisha fika kwamba hakuna haki inayopatikana hivi hivi tu bila ya kudaiwa. Na hivyo mimi ni Muislam wa Tanzania na ndio natumia haki hii ya: KUTOA MAONI JUU YA KATIBA MPYA KUTOA DUKUDUKU NA MADAI YA HAKI ZANGU ZA MUDA MREFU ZISIZOTEKELEZWA na serikali.; kwa kudai haki zangu katika njia hii. This is a priceless opportunity for Tanzanian Muslims to ventilate their grievances in full to the Constitutional Review Commission for consideration and implementation (hopefully at last).


MAONI YA KATIBA   NA.  MOJA – 20/8/2012
Ibara Na. 1 ya Katiba ya 1977:
Napendekeza Tanzania iwe nchi ya mfumo wa “Federation” rasmi ili kuondoa kero na manunng’uniko yote ya pande zote mbili za Muungano.  Kwamba nchi ya  Tanganyika ipatikane kama ilivyokuwa zamani kabla ya tarehe 26/4/1964,  na iwe nchi kamili.  Zanzibar tayari ipo na iendelee kuwa nchi kamili. 
Nchi hizi mbili zipige kura ya Maoni [Referendum] ili watu wake waseme endapo wanataka waendelee kuwa katika Muungano au waachane na mfumo huo.  Ili endapo zitakubaliana kuwa na Muungano, nchi hizi zikutane katika Federation ya Tanzania [TZ] (au jina lolote litakaloamuliwa na wananchi). Binafsi napendekeza jina hilo hilo libaki lakini tukiwa katika Federation. 
Kwa hiyo  Dola ya TZ iwe ni muungano wa nchi mbili zilizo huru za Tanganyika na Zanzibar.  Hata nchi nyingine yoyote itakapo kujiunga na  TZ ruhsa; endapo tu itakubaliana na matakwa ya watu wa TZ, huenda hilo likawa ndio chimbuko la Muungano wa Nchi za Afrika (United States of Africa).    
Mtindo huu wa DOLA utasaidia kuzihamasisha nchi nyingine za jirani Barani Afrika kutamani kujiunga katika Federation yetu; endapo tu tutaendesha mambo yetu kwa kufuata HAKI na UTAWALA WA SHERIA.
Kwa wakati huu niandikapo maoni haya (20/8/2012), nchini Tanzania hakuna haki tangu tupate UHURU tarehe 9/12/2012.  Hii ni kwa sababu sehemu moja ya jamii ya Watanzania imejilimbikizia haki ya kuamua nchi iendeshwe vipi na hivyo kuwafanya watu wa sehemu ya pili kuwa kama raia wa Daraja la Pili ndani ya nchi yao. 
Mifano ya kuthibitisha jambo hili ni mingi mno na kwa uchache niliyowahi kuithibitisha binafsi (kwa kunitokea mimi mwenyewe au kwa kuisoma katika maandiko ya kitaaluma) ni kama ifuatayo:
1.    Hulka ya wafuatao imani ya Kikristo ya kufundishana chuki dhidi ya watu wenye imani za dini nyingine; hasa Waislam.  Hili linathibitishwa na mifano kadhaa ifuatayo.
2.   Tabia ya ukiristo kujikita katika mamlaka za utumishi wa umma na kulazimisha nembo zao kutumika maofisini na hivyo kuwafanya watu wa dini nyingine kujisikia kubaguliwa kwa makusudi; jambo linalopingana  kabisa na Ibara ya 13 (1) ya Katiba ya 1977.   Mfano dhahiri wa jambo hili ni kupamba Maofisi ya Umma wakati wa sikukuu kwa alama za Krismasi [Miti mikubwa Sebule za Ofisi na kuipamba kwa “Chrismas Carols” na kutoa zawadi za pombe kwa maofisa mbalimbali maofisini]; kuweka “Compact Disks” [CD] za miziki ya dini ya Kikristo wakati wote maofisini na kuiliza kana kwamba wawekaji miziki hiyo wako Kanisani au wako majumbani kwao badala ya Ofisi za Serikali ISIYOKUWA NA DINI.  
3.   Nyimbo hizi na alama nyingine kuwekwa wazi maofisini kunakiuka kwa uwazi Ibara ya 3(1) inayotamka kwamba Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania ni nchi isiyokuwa na Dini.  
4.   Ndani ya Katiba Mpya, mambo haya yaandikwe na yapigwe marufuku kwa sababu yanawabagua Watanzania kutokana na imani zao.
5.   Mwezi Mei, 2012 usahihishaji wa mitihani ya Wanfunzi wa Kiislam ulichakachuliwa na wanafunzi hawa wote wakaonekana wamefeli somo la “Islamic Knowledge” ili wasipate sifa za kuweza kuomba kuendelea na masomo ya juu zaidi.  Jambo hili lilipogunduliwa  ETI likarekebishwa na srikali.  Tangu UHURU 9/12/2012 mchezo huu umeendelea kuchezwa na Wakristo dhidi ya Waislam kwa sababu huko nyuma Mwalimu Lila alithibitisha hili.  Yeye akiwa kama mmoja wa wasahihishaji wa mitihani ya wanafunzi wa sekondari, aligundua watahiniwa wa Kiislam wanakatwa maksi zao na kufelishwa kwa makusudi mazima na alipouliza wenziwe katika jopo la Wasahihishaji alijibiwa kuwa “hivyo ndivyo tunavyofanya katika kipindi cha misimu yote ya kusahihisha mitihani, kwani wewe hujui?”.  Alipolalamika hakuna kilichofanyika.
6.   Waislam walipolalamikia hili, Rais aliyepita Benjamin William Mkapa (1995 -2005) aliwahi kusema kwamba zipo sababu za kihistoria kwamba wasomi wengi zaidi nchini Tanzania ni Wakristo kuliko Waislam na kwamba anataka apelekewa ushahidi (empirical evidence) kama kweli Waislam wanafanyiwa madhila haya makusudi ili wafeli. Je, ni ushahidi gani zaidi alioutaka Mkapa zaidi ya ule wa Mwalimu Lila? Serikali haikufanya lolote baada ya kugunduliwa hili.  Imelipalilia na kulikubali liendelee.
7.   Jambo la kuwa Watanzania tunapendana binafsi; Watanzania tuna umoja wa kwenye damu kwa kuoleana kokote nchini Tanzania; Watanzania tunaoana japo kuwa tuko katika dini tofauti; yote ni kiini macho cha kupendezesha baraza; mapenzi haya hayako moyoni mwa Watanzania.  Watanzania hatupendani kama makundi tofauti ya imani tofauti.   Ukweli huu wa kubaguliwa kinaga ubaga (kwa kufelisha Waislam) kunawafanya Waislamu wajisikie ni raia wa Daraja la 10 na wala sio la Pili nchini mwao. 
8.   Kusutwa kwa nafsi ya Rais Benjamin William Mkapa na kuruhusu kutolewa majengo  ya Umma ya Chuo cha Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO)  mjini Morogoro, mwaka 2004 kuwa  Chuo Kikuu cha Waislam, hakusaidii kufuta makovu ya madonda ya madhara na madhila yanayowapata Waislam ndani ya nchi yao. 
9.   Kitendo cha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kushindwa kuwa na asasi zake yenyewe  za kuhudumia Umma wa Watanzania wote na badala yake  kutoa RUZUKU (zitokanazo na kodi za Watanzania wote) maradufu kwa Wakristo kujijengea huduma hizo na kuwa ni mrija wa utajirisho wao; kwa kuwa huduma hizi ni za kibiashara;  ni ubaguzi mwingine unaohisiwa kwa uchungu sana na Waislam.
10.                Katika Baraza la Maulid la mwaka 2012, kauli ya Rais wa sasa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais Jakaya Mrisho Kikwete mjini Dodoma kwamba ETI Waislam hawajaomba RUZUKU hizo ni tusi kubwa kwa sababu ushahidi upo dhahiri wa maandishi wa Waislam kuomba Ruzuku hizo mwaka 1961.   Jambo hili alilofanya Rais Kikwete kwa Waislam linafanana na kauli ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Andrew Chenge alipotamka mwaka 2010 kwamba shilingi zaidi ya bilioni mbili ni vijisenti tu.  Tofauti ni kwamba Kikwete katukana Asasi nzima ya Uislam (kama mfumo wa maisha); wakati Chenge alitukana Watanzania kwa ujumla wao; masikini na matajiri pia. 
11.                Katiba mpya iweke ibara zitakazotoa usawa katika kutoa ruzuku au ifute ruzuku zote husika. Isiegemee upande mmoja. 

12.                Habari zote chanya za Waislam kufumbiwa macho na vyombo vyote vya habari nchini – Viwe vya umma au vya binafsi.  Kinachotangazwa kuhusu Waislam ni upotoshaji wa habari zao, sana sana  kwamba Waislam ni waanzilishi wa vurugu na kwamba hawataki maendeleo. 
13.                Habari zote chanya za Wakristo kupambwa kwa vichwa vya habari vilivyokoloea (screaming headlines) na kuzificha zile zilizo hasi kwa wasomaji ili ionekane kwamba Wakristo ndio wapenda maendeleo na hawana matatizo wala migogoro baina yao katika Dhehebu mojamoja au kati ya madhehebu tofauti. 
14.                Tabia ya Asasi nyingi za Umma kupanga mikutano yao muhimu sana ya maamuzi (Kama ya Bodi, ya Mabaraza ya wafanyazi, ya Wadhamini, n.k.) siku za Ijumaa ili AIDHA Waislam wasiihudhurie; au muda wa saa moja  watakapokuwa na  udhuru wa kwenda kusali, ndio maamuzi yatayowaathiri vibaya; au maamuzi mazito yawahusuyo yachukuliwe.  Huu ni ubaguzi mbaya wa kumuengua mjumbe Mkutanoni kwa sababu ya imani yake. Yaani Muislam achague abaki mkutanoni ili atetee masilahi yake ya kidunia au akaabudu Mola wake na aachane na mambo yamhusuyo yeye na jamii yake duniani.  Huu ni ubaguzi USIOONEKANA.  Lugha waitumiayo wajumbe wa imani nyingine katika mikutano kama hii ni kwamba “Sacrifice Ijumaa hii tu” maana yake “fuata njia na utamaduni wangu na achana na huo wa kwako”.  Mikutano hii muhimu isipangwe siku za kuabudia dini yoyote katika sala za pamoja (congregational prayers).   Huu ni ubaguzi wa kimya kimya dhini ya Ibara ya 13 ya Katiba ya 1977 kwa ujumla wake. 
15.                Walimu wa Kikristo toka Chekechea, Msingi, Sekondari hadi Vyuo Vikuu kuwa na tabia ya kuwanyanyasa, kuwabagua, kuwatweza, kuwadharau, kuwapuuza, n.k. wanafunzi wasio wa dini yao.  Siku hizi hata wanafunzi wa shule za misingi huliongelea jambo hili.  Maana yake ni kuwa wanafanyiwa ubaguzi huo kwa dhahiri na sio kisiri tena.  Watoto wanajengewa chuki baina yao yaani wa dini moja na wa dini nyingine, dhidi ya Ibara ya 13 ya Katiba ya 1977. 
16.                Shule za Kikristo zinakaribisha maombi toka kwa wanafunzi wa dini zote kwa kigezo cha kuziendesha kibiashara bila ubaguzi wowote.  Kivitendo; shule hizi; kama ilivyokuwa shule za Mkoloni na za Makanisa toka kabla ya Uhuru; zinalazimisha Waislam kula nguruwe na kutowahudumia wakati wa hitajio maalum la mwezi wa Mfungo wa Ramadhani, na kuwapiga mafuruku kushiriki katika ibada ya pamoja ya Ijumaa.   St. Scholarstica (iliyopo Moshi) ni mfano mzuri sana wa hili kwa sababu jirani yangu aitwaye Abdulrazak Luwinzo watoto wake wawili wanasoma huko na wamemsimulia hili lililowakuta mwezi wa Ramadhani ulioishia tarehe 20/8/2012 (kwa kuwa watoto wamerudi wamekondeana kwa likizo ya Sensa ya 2012), na yeye amenisimulia mimi jana tarehe 19/8/2012. 
17.                Tabia ya Ukristo kung’ang’ania kuwa siku ya mapumziko ni Jumapili tu wakati watu wa dini nyingine wana siku zao za mapumziko ambazo hazitambuliwi kama siku za mapumziko kama Ijumaa kwa Waislam.  Na wala haitoshi kutoa muda wa kwenda kuabudu/sala kwa pamoja kwani hiyo hailingani na kutoa mapumziko kwa siku nzima.  Wakristo na wapumzike Jumapili na Waislam wapumzike Ijumaa.
18.                 Katiba mpya iseme wazi uhuru wa kuchagua siku ya mapumziko kwa imani zote.
19.                Tabia ya Wakristo kukataa katakata uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi nchini Tanzania kwa mujibu wa imani ya Dini ya Kiislam.  Wakati nchi ya Tanzania imerithi mfumo wa sheria za Kikoloni za Dola la Uingereza ambalo sheria zake zimetokana na chimbuko la Kanisa (Ecclesiastical courts) na ndizo zitumikazo kwa watu wote; lakini Dola kwa shinikizo la Wakristo, linapuuzia dai la Waislam la kuwa na Mahakama yake ya Kadhi iliyokuwepo huko nyuma  (kabla ya kuvunjwa miaka ya sitini – 1960s) na ikigharimiwa  na Dola.  Usawa wa kuhudumia watu wake unapotea wakati sheria za Tanzania zimerithi mfumo wa sheria za Kanisa na Waislam wanakataliwa Dola yao isigharimie Mahakama yao kana kwamba hawachangii kodi zao. 
20.                Katiba mpya iandike kuruhusu kuwepo kwa Mahakama ya Kadhi itakayogharimiwa na Dola kama ilivyokuwa huko nyuma na mambo yalikwenda vizuri kwa imani zote. 
21.                Tabia ya Wakristo wengi kukasirikia Vazi la Stara la Kiislam kana kwamba wameligharimia wao linawakera sana Waislam.  Wengine wanafikia hata kuwaita Waislam hao (pamoja na mimi) na “kuwanasihi” waache au wabadilishe vazi hilo  ili wavae kama wanavyovaa wao.  Kwa Waislam vazi hilo ni sehemu ya Ibada.  Wasijisikie vibaya  watu wa dini nyingine kutimiza amri za Mola wao ili mradi hawavunji sheria hizo za Dola za urithi wa Kikanisa. 
22.                Kuruhusu MAPAMBIO [nyimbo za kidini ya kikristo] hata katika shughuli/tafrija za umma zilizoandaliwa na serikali ambako haitakikani kuwa hivyo kwa sababu serikali haina dini.  Badala yake pasiwepo hata nyimbo kama hizo zinazoingiza hisia ya kubaguliwa kwa watu wa imani nyingine. 
23.                Katiba mpya  iseme kwamba jambo hili ni marufuku. 
24.                Pendekezo la kuingiza katika Katiba Mpya jingine ni kuwa midhali Tanzania kwa mahesabu ya sense ya sasa ya “kusadikika” ni kuwa tuko wananchi wa imani kuu mbili wenye asilimia sawa  (asilimia 32 kwa 32), basi Katiba Mpya iseme kwamba katika kila Nyanja ya Utumishi wa Umma pawepo na uwakilishi wa 50-50 ili kuondoa  hizi hisia za kubaguliwa, kubaguana, chuki za dhahiri na za siri dhidi ya Waislam wa Tanzania. 
25.                Mambo yote haya yana haki zote za kuwekwa wazi na kuzungumzwa na kujadiliwa kinaga ubaga, bila ya kuficha kitu ili kila mtu ayafahamu na ajue kisa na sababu ya watu wa imani moja katika Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania wanadai haki zao kila uchao; haki ambazo hazitimizwi na serikali yao. 
26.                 Historia inatufahamisha fika kwamba hakuna haki inayopatikana hivi hivi tu bila ya kudaiwa.  Na hivyo mimi ni Muislam wa Tanzania na ndio  natumia haki hii ya:  KUTOA MAONI JUU YA KATIBA MPYA KUTOA DUKUDUKU NA MADAI YA HAKI ZANGU ZA MUDA MREFU ZISIZOTEKELEZWA na serikali.; kwa kudai haki zangu katika njia hii.  This is a priceless opportunity for Tanzanian Muslims to ventilate their grievances in full to the Constitutional Review Commission for consideration and implementation (hopefully at last).
























No comments:

Post a Comment