Thursday, September 13, 2012

MAAZIMIO YA KAMATI KUU YA CHADEMA TANZANIA DHIDI YA MAUWAJI YA DAUDI MWANGOSI

Imeingizwa hapa tarehe 13/9/2012.

Imesomwa na Mwenyekiti  wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa,  FREEMAN  MBOWE, Tarehe 10 Septemba, 2012. 

 1. Uwajibikaji wa kisiasa wa viongozi wa serikali na idara zake.,Waziri 
 Emmanuel Nchimbi, IGP Saidi  Mwema, Paul Chagonja, RPC Morogoro,  Kamanda wa FFU,   
 RPC IRINGA na Kamanda wa FFU wajiuzulu na/au wafukuzwe kazi.
 
 2.RPC Morogoro na Iringa, makamanda wa FFU Morogoro na Iringa,  Askari waliouwa wakamatwe mara moja na kufunguliwa mashitaka.



3.Rais aunde tume huru ya uchunguzi wa vifo tata katika matukio yA  kisiasa.

1.  ARUSHA vifo 3.
2.  IGUNGA,vifo vingi havijulikani bado,
3.  ARUMERU MASHARIKI, vifo 5,
4.   SINGIDA kifo 1,
5.  MOROGORO  kifo  1,  18 Agosti, 2012.
 IRINGA kifo cha Daudi Mwangosi, Mwandishi wa Habari wa Channel Ten, 2 Septemba, 2012. 
 CHADEMA   haitatambua wala kushirikiana na kamati batili ya NCHIMBI.

4.Msajili wa vyama vya siasa John Tendwa ni mtu hatari kwa taifa kwa kauli 
tata anazozitoa.anashirikiana na au anajipendekeza kwa CCM na Serikali 
yake.CHADEMA tangu sasa haitafanya kazi na Tendwa wala kufanya mawasiliano 
 naye ya kiofisi.Labda kama atagundua makosa yake na kuomba msamaha,
CHADEMA  itatafakari namna ya kufanya naye kazi tena.

 5.TBC TAIFA Television na Redio ni hatari kwa taifa,kwa kubobea kupotosha 
 umma juu ya matukio mengi.Hivyo CHADEMA Inatangaza mgogoro na TBC na 
inaelekeza na kuomba wanachama ,wapenzi,na wananchi wote wapendao ukweli na 
haki,kuisusia TBC

6.Jeshi la Polisi lijue kuwa Maandamano ndiyo siasa yenyewe na mikutano ya hadhara ni lazima kwa 
mawasiliano ya umma na siasa.kuzuia vitu hivyo ni 
 kunyima wananchi haki yao ya kikatiba ya uhuru wa kukusanyika na kutoa 
 maoni,pia kupata habari na taarifa

7.Operesheni MOVEMENT FOR CHANGE M4C,Inaendelea kadiri ya ratiba 
ilivyopangwa katika utaratibu uleule uliokuwepo awali.Inarejea Iringa Siku si nyingi.
Na kamati kuu Imetoa msisitizo MAALUM kwa jimbo mojawapo 
 singida,ambapo wamesema watatumia helcopita,magari,pikipiki na baiskeli na 
 miguu,na badala ya kupita vijijini kama majimbo mengine,Chadema wanasema kwa 
 sababu maalum katika jimbo hilo watapita kitongojikwa kitongoji,ili kufunza 
 adabu baadhi ya viongozi (msisitizo ni wa msoma MAAZIMIO.jimbo hili laweza 
kuwa la Mwigullu Mchemba,kadiri ya wanahabari waliokuwepo)

 8.Kutokana na mgogoro wa muda mrefu mkoani mwanza uliosababisha meye wa 
 chadema kuvuliwa umeya kinyume na utaratibu na kwa njama za CCM na 
 Serikali,na bahati mbaya sana kwa kushirikisha madiwani wa CHADEMA,KAMATI 
 KUU imewavua UANACHAMA madiwani wake wawili 1 ADAMU CHAGULANI wa kata ya 
 IGOMA na HENRY MATATA wa KITANGIRI, PIA uongozi wote wa CHADEMA mkoa wa 
 Mwanza Umevunjwa.

No comments:

Post a Comment