Friday, May 15, 2009

WANYAMAPORI WA AFRIKA HAWANA MIPAKA

Jamani, WANYAMAPORI wetu wa Afrika tangu lini wamewekewa mipaka? Tuliowekewa mipaka ni sisi wanadamu tu. Hawa hawana hatia. Kama wanafanya uharibifu, ni dalili ya wazi kwamba wenzetu jirani wameshaharibu mazingira yao kiasi kwamba sasa hawana jinsi ya kujipatia chakula; na ndio sababu ya kuvamia mashamba upande wapili ! Tusiwalaumu wanyama, tujilaumu sisi wanadamu hatuko makini na maliasili zetu.


Date: Thursday, May 14, 2009, 3:44 PM

TEMBO, NYUMBU WA KENYA WAHARIBU MAZAO KILIMANJARO



Written by Rehema Matowo
elephants.jpg
MKUU wa Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro, Anarose Nyamubi ameiomba serikali kuchukua hatua za haraka kuwaondoa wanyama wakali kutoka nchini Kenya waliovamia makazi ya watu katika Wilaya hiyo na kusababisha wakazi wa maeneo hayo, kuogopa kutoka nje kwa kuhofia kujeruhiwa na tembo na nyumbu.


Nyamubi aliyasema hayo, katika kikao cha 18 cha ushauri cha Mkoa kilichofanyika juzi na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali na kufafanua kuwa kundi la Nyumbu, tembo na swala kutoka katika msitu wa hifadhi wa Amboseli nchini Kenya wamevamia katika Wilaya hiyo na kuharibu mazao ya chakula.


UNAONA BASI, HATA WANYAMA WA KENYA WANATAKA KUHAMIA TANZANIA!
Jitukali.

No comments:

Post a Comment