Saturday, June 19, 2010

MAJIBU YA KUKATISHATAMAA BINAFSI NA KITAASISI

KUJENGA NCHI NI KAZI, NA NI KAZI KUBWA SANA.

Hatimaye baada ya kuelezea ugumu wa mimi kufanya mambo mawili kwa pamoja yafuatayo; ambayo yote yalihitaji muda na kujitolea kwangu kwa bidii yangu yote, yaani:

1. Kuandaa Mabadiliko ya Andiko (Proposal improvement) la kuanzia Kituo cha Kutoa Msaada wa Sheria Chuo Kikuu Mzumbe

2. Kukazania kusoma sana kutayarisha andiko la kwanza kwa masomo ya Digrii ya Uzamivu (PhD Proposal rectification and modification).

Niliandika barua kwa Mkuu wangu kuomba kwamba Jambo la kwanza likabidhiwe kwa mtu (watu wengine) kwa sababu nimetingwa sana na jukumu la pili ambalo tayari nilikuwa nimechelewa (time-barred).

Mkuu wangu wa Kazi akanifahamisha tarehe 14/6/2010 kwamba kwa kuwa hakushirikishwa katika jambo hilo tangu mwanzo, yeye hawezi kufanya lolote. (Wakati nalifanya jambo hili, yeye alikuwa masomoni, na pia kila barua niliyoandika juu ya suala hili niliinakilisha ofisini kwakwa kwa taarifa). Hii maana yake ni kwamba dhamira yangu ya kukienzi chuo changu kwa kufungua kituo kama hicho imekufa kifo cha MENDE.

Hivi sasa nahaha sana kuhangaikia shule yangu ambayo nikifanikiwa nayo, inshaallah, sijakata tamaa, nitaendelea na jambo hilo Na. 1 hapo juu hata kama italazimika kufanya hivyo nje ya Taasisi yangu niliyodhamiria kuwa kianzishwe hapo. Mungu anajua yote, amin.

3 comments:

  1. This comment has been removed by a blog administrator.

    ReplyDelete
  2. This comment has been removed by a blog administrator.

    ReplyDelete
  3. This comment has been removed by a blog administrator.

    ReplyDelete