Tuesday, April 28, 2015

SHUJAA BRIGEDIA JENERALI MSTAAFU HASHIM MBITA AFARIKI DUNIA

Brigedia Jenerali Hashim Mbita atangulia mbele ya haki 

Source:  Michuzi.blogspot 

Brigedia Jenerali Mstaafu Hashim Mbita aliyekuwa Katibu Mtendaji wa Kamati ya Ukombozi ya uliokuwa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU), amefariki dunia asubuhi hii tarehe 26/4/2015  katika hospitali kuu ya Jeshi, Lugalo, jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa za kifamilia, mazishi yanatarajiwa kufanyika katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam siku ya Jumanne Aprili 28, 2015 - saa 10 Alasiri baada ya swala.

Msiba upo nyumbani kwa marehemu Chang'ombe jirani na TCC Club jijini Dar es salaam.

Mzee Mbita atakumbukwa Tanzania, bara zima la Afrika na dunia kwa jumla kama mmoja wa makamanda mahiri aliyeshiriki kikamilifu katika uondoshaji wa utawala wa ukoloni barani Afrika, hususan utawala kidhalimu wa makaburu Zimbabwe na Afrika ya Kusini na hatimaye kuachiwa huru kwa aliyekuwa Rais mzawa wa kwanza nchini Afrika Kusini, hayati Nelson Mandela.

No comments:

Post a Comment