Thursday, July 29, 2010

SABABU MIA MOJA ZA KUMREJESHA KAGAME MADARAKANI

KAGAME AFAGILIWA NA WANYARWANDA

"100 Reasons to Re-elect Paul Kagame"

1. Education



1. Ensuring 9-Year Basic Education for all Rwandan children that will tremendously improve literacy levels in the country
2. A promise to have Universal Secondary Education by 2017
3. Making education accessible by all with no segregations, particularly promoting Girls' and Special Needs' education
4. Encouraging parents and communities' involvement in education
5. Introducing English as medium of instruction in schools to make Rwanda more competitive on the global stage
6. Creating 14 new Higher Learning Institutions, almost tripling Higher Education enrolment in 7 year years
7. Providing scholarships to the best and brightest Rwandan students to pursue their studies in the best universities of Europe and North America;
8. Promising to achieve 100% literacy by 2017 through effective adult education;
9. Introducing technology in schools starting with primary schools under the 'One Laptop Per Child' program
10. Increasing the number of qualified teachers at all levels of education through effective distance learning and in-service training and remunerating them adequately.

2. Health


1. Raising the life expectancy in Rwanda from 43 to 53 years;
2. Introducing 6 types of health insurance including the famous "Mutuelle de Santé" resulting in a health insurance coverage of 94% of the population;
3. Introducing universal immunisation programmes;
4. Introducing health awareness programs;
5. Reducing deaths from malaria by 75%;
6. Reducing infant mortality by 70%;
7. Reducing HIV infections from 9 percent to 2%;
8. Building a clinic in every sector;
9. Reducing water-borne diseases by 60%;
10. Ensuring that more doctors and nurses are trained and deployed evenly across the country


3. Justice


1. Trying over 1,100,000 cases in the Gacaca court system;
2. Undertaking a complete restructuring of the justice sector;
3. Introducing many laws for different sectors that brings orderliness in State functioning;
4. Releasing over 80,000 genocide convicts safely into the community while ensuring law and order in the society;
5. Making convicted prisoners give back to society through work schemes;
6. Building over 100 new courts of law;
7. Training over 300 new judges;
8. Creating an independent judicially and an independent Judge selection process;
9. Promoting local mediation services to reduce backlog of court cases;
10. Introducing the commercial courts and streamlining the justice system by merging the administration process;


4. Agriculture




1. Introducing crop intensification programme and boosting agricultural production by 10 percent annually;
2. Introducing the cooperative system to buy produce from farmers;
3. Diversifying the crops cultivated through sensitisation;
4. Significantly reducing poverty and mal-nutrition through the one cow per family: "the Girinka" programme;
5. Introducing a phone text service that can inform farmers of the latest crop prices
6. Making subsidized seeds and fertilizers available on credit;
7. Promoting mechanised agriculture through a scheme of 1 tractor per village
8. Making veterinarians more widely spread across the country
9. Introducing irrigation farming
10. Making 'hunger' a history in our country

5. Economy

1. Increasing average earnings of Rwandans from $220 to $560 in 7 years!
2. Strengthening the private sector and streamlining doing business in Rwanda;
3. Increasing the tax base and total revenue collected domestically ;
4. Promoting credit to small to medium sized enterprises;
5. Increasing domestic funding of government to development projects in national budget from 10% to 50%;
6. Promoting transparency by fighting corruption;
7. Diversifying the economy by promoting new sectors like mining and tourism;
8. Promoting foreign direct investment to nearly $1 billion annually;
9. Making poverty-reduction the hallmark of economic development;
10. Cutting down on government expenditure through initiatives like reducing on the number of government vehicles;

6. Security


1. Making Rwanda one of the safest places in the world
2. Devolving security responsibility down to the local level
3. Reducing crime through local initiatives
4. Professionalising the Army and integrating former hostile elements
5. Fighting impunity and corruption in the army and hence cementing discipline
6. Sending Rwandan soldiers and Police officers to keep peace in war ravaged places like Darfur, Haiti, Liberia, etc.
7. Introducing electronic ID cards to all adults
8. Instituting a police force that is disciplined and highly professional
9. Establishing a credit scheme for the Army and Police
10. Making peace with neighbours like Democratic Republic of Congo


7. Foreign policy


1. Making Rwanda a respected partner in regional and international affairs
2. Improving Rwanda's relations with former hostile nations like France and DRC
3. Making Rwanda one of the biggest contributors of peace-keepers in the UN
4. Working tirelessly to track and prosecute Genocide suspects
5. Joining the East African Community and the Commonwealth
6. Being one of the foremost advocates of fully integrated EAC
7. Relentlessly promoting Rwanda abroad and expanding her relations to countries such as Australia, Singapore, South Korea, etc.
8. Chairing powerful global initiatives like the UN MDGs and the ITU Broadband Commission and serving on the Advisory board of the World Bank.
9. Creating special friends for Rwanda that have always defended our cause.
10. Refusing to be bullied by the west and always insisting on an equal voice for Africa on the global scene.


8. Technology


1. Making ICT the main focus of our long-term development
2. Making technology integral to government service provision
3. Supporting the one laptop per child policy
4. Laying thousands of kilometres of fibre-optic cables
5. Connecting all government centers to the internet
6. Abolishing import duties on ICT equipment
7. Building one of the best telephone network systems in the region
8. Strongly advocating for undersea cable to land on EA coastline and now eventually in Rwanda
9. Turning Rwanda into an influential country on ICT global issues
10. Emphasising on ICTs in our education programs and setting up institutions to oversee this program

9. Infrastructure


1. Constructing good roads across the country
2. Building communication towers to help link outlying areas
3. Setting up building regulations to improve basic infrastructure
4. Reducing tax on building materials to encourage growth of the industry
5. Bringing electricity to all major areas, with plans to expand it to every village
6. Coming up with a master plan and securing funding for a new international airport
7. Advocating for Isaka railway line which will reduce transport costs
8. Ensuring that Kigali master plan is implemented
9. Building district and sector headquarters nationwide
10. Investing heavily in ICT infrastructure


10. Kagame, the man


1. He is a man of principle and values
2. He is pragmatic and ready to make tough choices in the interest of his country
3. He promises and delivers
4. He is patriotic and wants the best for Rwandans
5. He is a visionary and inspirational leader
6. He is intelligent, skilful and innovative
7. He is a humble man who does not value personal gains
8. He is not a man to bully and he is never shaken by circumstances
9. He has a humble background that shapes his character as a down-to-earth leader
10. He is a family man and cherishes family values


"You Do Not Change a Winning Team"

MTU MWEUSI WA KWANZA KUCHAGULIWA URUSI

POSTED HERE ON 29/7/2010.

SOURCE: http://news. yahoo.com/ s/ap/20100725/ ap_on_re_ eu/eu_russia_ black_politician

By KRISTINA NARIZHNAYA, Associated Press Writer Kristina Narizhnaya, Associated Press Writer 2 hrs 22 mins ago -
NOVOZAVIDOVO, Russia – People in this Russian town used to stare at Jean Gregoire Sagbo because they had never seen a black man. Now they say they see in him something equally rare — an honest politician.
Sagbo last month became the first black to be elected to office in Russia.
In a country where racism is entrenched and often violent, Sagbo's election as one of Novozavidovo' s 10 municipal councilors is a milestone. But among the town's 10,000 people, the 48-year-old from the West African country of Benin is viewed simply a Russian who cares about his hometown.
He promises to revive the impoverished, garbage-strewn town where he has lived for 21 years and raised a family. His plans include reducing rampant drug addiction, cleaning up a polluted lake and delivering heating to homes.
"Novozavidovo is dying," Sagbo said in an interview in the ramshackle municipal building. "This is my home, my town. We can't live like this."
"His skin is black but he is Russian inside," said Vyacheslav Arakelov, the mayor. "The way he cares about this place, only a Russian can care."
Sagbo isn't the first black in Russian politics. Another West African, Joaquin Crima of Guinea-Bissau, ran for head of a southern Russian district a year ago but was heavily defeated.
Crima was dubbed by the media "Russia's Obama." Now they've shifted the title to Sagbo, much to his annoyance.
Click image to see more photos of Jean Gregoire Sagbo


AP


"My name is not Obama. It's sensationalism, " he said. "He is black and I am black, but it's a totally different situation."
Inspired by communist ideology, Sagbo came to Soviet Russia in 1982 to study economics in Moscow. There he met his wife, a Novozavidovo native. He moved to the town about 100 kilometers (65 miles) north of Moscow in 1989 to be close to his in-laws.
Today he is a father of two, and negotiates real estate sales for a Moscow conglomerate. His council job is unpaid.
Sagbo says neither he nor his wife wanted him to get into politics, viewing it as a dirty, dangerous business, but the town council and residents persuaded him to run for office.
They already knew him as a man of strong civic impulse. He had cleaned the entrance to his apartment building, planted flowers and spent his own money on street improvements. Ten years ago he organized volunteers and started what became an annual day of collecting garbage.
He said he feels no racism in the town. "I am one of them. I am home here," Sagbo said.
He felt that during his first year in the town, when his 4-year-old son Maxim came home in tears, saying a teenage boy spat at him. Sagbo ran outside in a rage, demanding that the spitter explain himself. Women sitting nearby also berated the teenager. Then the whole street joined in.
Russia's black population hasn't been officially counted but some studies estimate about 40,000 "Afro-Russians. " Many are attracted by universities that are less costly than in the West. Scores of them suffer racially motivated attacks every year — 49 in Moscow alone in 2009, according to the Moscow Protestant Chaplaincy Task Force on Racial Violence and Harassment, an advocacy group.
After the Soviet Union collapsed, Novozavidovo' s industries were rapidly privatized, leaving it in financial ruin.
High unemployment, corruption, alcoholism and pollution blight what was once an idyllic town, just a short distance from the Zavidovo National Park, where Prime Minister Vladimir Putin and President Dmitry Medvedev take nature retreats.
Denis Voronin, a 33-year-old engineer in Novozavidovo, said Sagbo was the town's first politician to get elected fairly, without resorting to buying votes
"Previous politicians were all criminals," he said.
A former administration head — the equivalent of mayor in rural Russia — was shot to death by unknown assailants two years ago.
The post is now held by Arakelov, a veteran of the Soviet war in Afghanistan who says he also wants to clean up corruption. He says money used to constantly disappear from the town budget and is being investigated by tax police.
Residents say they pay providers for heat and hot water, but because of ineffective monitoring by the municipality they don't get much of either. The toilet in the municipal building is a room with a hole in the floor.
As a councilor, Sagbo has already scored some successes. He mobilized residents to collect money and turn dilapidated lots between buildings into colorful playgrounds with new swings and painted fences.
As he strolled around his neighborhood everyone greeted him and he responded in his fluent, French-African- accented Russian. Boys waved to Sagbo, who had promised them a soccer field.
Sitting in the newly painted playground with her son, Irina Danilenko said it was the only improvement she has seen in the five years she has lived here.
"We don't care about his race," said Danilenko, 31. "We consider him one of us."

__._,_.___

Monday, July 26, 2010

Na Muhingo Rweyemamu, RAI - 26/7/2010

KWA vyovyote itakavyokuwa, Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu utatawaliwa na vijana, Rai inaweza kuthibitisha.

Tofauti na miaka ya nyuma ambayo siasa za uchaguzi ziliongozwa na kutawaliwa na wazee huku vijana wakiwa wasaidizi wa ushindi wa wazee hao, mambo yanaonekana kubadilika sana katika uchaguzi wa mwaka huu na vijana wanaonekana kujizatiti na mbinu mpya kuliko watu wa makamo.

Gia aliyoingia nayo Januari Makamba, ya kutembelea Jimbo zima la Bumbuli na kufanya kile wataalam wanaita ‘participatory research’ huku akibuka na kitabu kinachoeleza hali halisi ya wakazi wa Jimbo hilo, ni moja ya mambo yaliyowashitua siyo wagombeaji wenzake tu, bali pia hata vijana waliomo bungeni.

Wakielezea hali hiyo, Ismael Jussa, Mbunge wa kuteuliwa pamoja na Zitto Kabwe, walisema jambo alilolifanya Makamba, limewapa changamoto kama vijana ili waweze kufanya mambo makubwa zaidi ya hayo siku z ijazo.

Takwimu za idadi ya watu, zinatuonyesha kwamba Tanzania ni taifa changa. Kwa maana kwamba ina idadi kubwa ya watoto na vijana kuliko watu wazima. Kwa mujibu wa Shirika la Ujasusi la Marekani, CIA, wastani wa umri wa Watanzania ni miaka 18.7 Hii maana yake ni kwamba ukichukua umri wa wazee , ukajumlisha na umri wa watoto , kisha ukagawa mara mbili, umri wa wastani ni miaka 18

Katika Tanzania watoto wenye umri wa chini ya miaka kumi na tano ni milioni 17 wakiwamo wavulana 8,853,529 na wasichana 8,805,810. Wastani wao ni asilimia 43.


Watu wenye umri kati ya miaka 15-64 ni milioni 22 wakiwamo wanaume 10,956,133 na wanawake 11,255,868 na wastani wao ni asilimia 54 ya Watanzania wote wakati wenye umri juu ya miaka 65 wanafanya asilimia 2.9 ya Watanzania kuwa au kama watu milioni moja na nusu.

Hata hivyo, ukichukua watu wenye umri tangu miaka 0 hadi miaka 29 wanatengeneza asilimia 70 ya Watanzania ambao wengi wao ndiyo kundi kubwa la wapiga kura na hasa wanaopiga kura kwa mara ya kwanza ambao wanaingia katika uchaguzi na vionjo vyao, maono yao na matamanio yao.

Idadi kubwa ya vijana wapiga kura wamo katika Shule za Sekondari za kidato cha tano na sita (1.5) na kutoka Vyuo Vikuu wamo 82,428 ambao wanatarajiwa kuleta hamasa kubwa katika kampeni hizi.

Kihistoria, vijana wamekuwa nguzo muhimu katika ukombozi wa nchi yetu kupitia TANU, na pia katika kuhakikisha ushindi wa chama hicho na Chama Cha Mapinduzi ambacho ndiyo mrithi wa TANU.

Kwa bahati mbaya, katika miongo ya karibuni, vijana wengi wamekuwa daraja la wazee katika kufikia uongozi. Umoja wa Vijana wa CCM umekuwa ukitumika kuhamasisha watu kupiga kura, kujibu mashambulizi na kwa ujumla kutia hamasa chaguzi za chama.

Miaka ya karibuni, chama hicho kikongwe kilianzisha kikundi cha ‘Tanzania One Theatre Group’ ambacho kwa kiasi kikubwa, kimefanikiwa kuwakusanya Watanzania katika sehemu za kampeni na hivyo kusikiliza hotuba.

Vyama vingine vinejitahidi kuanzisha vikundi ingawa hakuna chama chenye kundi lenye nguvu kama TOT. Hata ndani ya CCM, vikundi vingi vya vijana vimejaribu mara kadhaa kuibuka lakini havikufika mbali.

Safari hii, mambo yamebadilika kabisa, badala ya vijana kuwa wasindikizaji wa wazee, sasa vijana wameamua wenyewe kushika bendera ya chama hicho. Katika sehemu kadha wa kadha, mwitikio wa vijana umewakosesha raha wazee hata kabla ya kipindi cha kampeni kuanza.

Idadi ya vijana waliochukua fomu kugombea Ubunge na Udiwani kwa tiketi ya CCM ni kubwa mno na kutakuwa na shughuli pevu wakati wa uteuzi.

Sambamba na hilo, ujio wa waziwazi wa wanafunzi wa Vyuo Vikuu katika harakati za uchaguzi mkuu wa mwaka huu, unaonyesha mabadiliko makubwa yatakayotokea wakati wa kampeni.

Katika mkutano mkuu wa CCM, vijana waliwafunika wazee kwa kila hali. Ukumbi ulikuwa ni wa shamrashamra zilizoongozwa na vijana.

Nyimbo pamoja na hotuba za vijana zilikuwa za mikiki mikiki. Wakati fulani ilionekana kwamba vijana wanataka kuimaliza enzi ya kikundi cha TOT ingawa waswahili walisema uzee ni dawa.

Pale vijana kwa mfano wa Vyuo Vikuu waliposimama kuimba wimbo wao, ukumbi mzima ulilipuka kwa shangwe na kujumuika katika kucheza wimbo huo unaokwenda kwa jina la NI KIKWETE.

Vijana kama Bushoke, Marlow, Flora Mbasha na Doki waliwafanya wajumbe wa mkutano mkuu kushindwa kuketi kwenye viti vyao. Katika kipindi cha burudani hizo, muda pekee wajumbe walipopata nafasi ya kupumzika, ni pale nyimbo za TOT zilipokuwa zikipigwa.

Ujio wa vijana katika kampeni hizi, unatufundisha jambo moja kwamba hali ya sasa ya siasa, ni sawa na jini aliyefunguliwa kwenye chupa. Uwezekano wa kumrudisha ni mgumu na kwa msingi huo, ni lazima tujifunze namna ya kuishi naye.

Mazingira ya zamani ya siasa za nchi zetu, yalikuwa yanatoa nafasi pana kwa viongozi waliomo madarakani kuwa walezi wa vijana wanaochipukia katika uongozi. Kwa sasa, hali hiyo haipo sana. Hivi karibuni, Chama Cha Mapinduzi kilikuwa na semina kule Iringa ambayo ilikuwa ikiwaandaa vijana wake. Hata hivyo, hayo siyo maandalizi ya kisiasa, yalikuwa maandalizi kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka huu.

Vyama vya upinzani navyo vinao vijana machachari waliokuwamo bungeni na wale waliomaliza shule. Kwa bahati mbaya, habari zao hazisikiki sana kama zinavyosikika zile za CCM na labda sababu kubwa ni ukosefu wa chombo cha kitaifa cha kuwaunganisha na kuwapatia mafunzo vijana. Baada ya siasa kupigwa marufuku katika shule na katika vyuo, vijana wanasiasa wanaokotwa barabarani au wale ambao waliasi amri ya kuzuia siasa katika taasisi za elimu. Kinachoshangaza ni kwamba hata wale vijana wanaochukua kozi za Political Science, hawana muda rasmi ulioruhusiwa kisheria na kitaratibu wa kufanya mazoezi kwa yale wanaotarajia kufanyia kazi.

Kwa nini vijana wanahitaji kuandaliwa? Kwanza kilichojitokeza kule Dodoma ni sababu tosha ya kuwafikirisha wazee na kuwaandaa vijana ili watambue nini cha kuongea, wakiongee lini na wapi.

Kwa mfano katika mkutano huo wa Dodoma, vijana wa Vyuo Vikuu walikaribishwa kusoma risala yao ambayo baadaye tulikuja kupata taarifa kwamba haikuwa imesomwa na yeyote. Yaani ilikuwa risala ya mashtukizi.

CCM ilikuwa imewaalika viongozi wa vyama vya upinzani. Walikuwapo Mwenyekiti Mrema, Mwenyekiti Lipumba na Mwenyekiti Dovutwa pamoja na wengine. Vijana katika hotuba yao, waliwageukia wageni hao ambao kimsingi walikuwa ni wageni wa mwenyekiti wa chama chao, wakasema: “Hawa Mavuvuzela, hawatuwezi”.

Kwa ujumla, maneno hayo yaliwaudhi viongozi wengi wa vyama hivyo. Mmojawao, Profesa Ibrahim Lipumba aliamua kuondoka kabla ya muda wake. Ilipofika muda wa Mwenyekiti kuongea, tofauti kati ya watu waliopata malezi ya kisiasa na wale ambao hawajapata malezi ya kisiasa ilijionyesha. Kikwete aliwakaribisha wageni wake, kuwasifia, kuwapa nafasi ya kuongea na kuwaomba uchaguzi wa mwaka huu uwe wa kistaarabu kwa sababu “tunajenga nyumba moja, hatuna sababu ya kugombania fito”. Hayo ni maneno yaliyosemwa na mtu aliyewakaribisha wageni nyumbani mwake. Mwenyeji, hatarajii watoto wake ‘wawachape fimbo’ wageni wake.

Mwanzo wa ngoma ni lele. Tunatarajia kuyaona mengi wakati wa uchaguzi.

MAOFISA WA TAKUKURU WANUSURIKA KIPIGO

Imeandkwa na Martha Mtangoo, Dodoma; Tarehe: 25th July 2010 Habari Leo



MAOFISA watatu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), mkoani hapa juzi walinusurika kupigwa na wananchi katika Kata ya Makulu,Kijiji cha Njedengwa baada ya kudhaniwa ni wezi.

Mkuu wa Takukuru mkoani hapa, Eunice Mmari aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa tukio hilo lilitokea juzi saa mbili usiku baada ya kupatiwa taarifa na raia mwema kuwa kuna baadhi ya viongozi wa eneo hilo wapatao 30 wamekusanyika nyumbani kwa Mwenyekiti wa Tawi la CCM Njedengwa kwa ajili ya kupewa pesa ili wamchague diwani.

Mmari alisema mara baada ya kupatiwa taarifa hiyo wakiwa njiani kuelekea eneo la tukio, waliona mtu akiwa katika pikipiki akiwa mbele ya gari lao waliamua kumpita na baada ya kumpita mtu huyo alipiga kelele za kuwataarifu Takukuru waliokuwa wanaelekea eneo hilo.

Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Takukuru wananchi hao waliokuwa wamekusanyika katika nyumba hiyo walipiga filimbi na kuwataarifu wanakijiji wenzao kuwa wameingiliwa na majambazi hali ambayo iliwafanya wanakijiji hao kuwazingira maofisa wa Takukuru na kutaka kuwapiga wakidai kuwa ni wezi.

Akielezea zaidi juu ya tukio hilo, alisema kuwa zaidi ya wanakijiji 200 waliwazingira na kutaka kuwapiga ambapo wengine waliwamwagia pombe na kudai kuwa ni wezi huku wengine wakisema kuwa kama wamekuja kwa ajili ya kumharibia diwani wao hawamuwezi ni bora wakamuacha.

Alisema kuwa waliwekwa chini ya ulinzi huku wakiwa wamezungukwa na wananchi kwa zaidi ya saa mbili.

Alifafanua kuwa sakata hilo liliisha saa nne na nusu usiku baada ya Mwenyekiti wa kitongoji hicho kuwasihi na kuwaachia huru wananchi hao ambao walitaka pia kuvunja vioo vya gari ya maofisa hao.

Aidha alisema kuwa, mbali na tuhuma hiyo pia Diwani huyo wa Kata ya Makulu, Ali Biringi anachunguzwa na Takukuru baada ya kukutwa na kadi 98 zisizo halali za CCM.

Alisema kuwa awali Takukuru ilipata taarifa juu ya diwani huyo kuwa na kadi hizo ambapo alikutwa na jumla ya kadi 177 za CCM ambapo baada ya kukaguliwa alikutwa na jumla ya kadi 98 zisizo halali na kuwa uchunguzi bado unaendelea

M A Z I N G A O M B W E YA C C M TANZANIA

http://newhabari.co.tz

*Yajipanga kusimamia njia kuu za uchumi
*Yasisitiza elimu ya kujitegemea kwanza


*Yasema bila sayansi Taifa halifiki popte
*Yaagiza Serikali kufumua mitaala ya elimu
*Yakiri wingi wa wasomi umeanza kuwa tatizo

CHAMA cha Mapinduzi (CCM), kimeufanyia mapinduzi makubwa Mwelekeo wake wa sasa kwa kuamua uwalenge zaidi wananchi wa kipato cha chini ili waweze kushiriki katika mfumo halisi wa uchumi wa dunia ya sayansi na teknolojia.

Sambamba na hayo, Chama hicho kimeangalia kwa kina mwenendo wa uchumi wa dunia, na siasa za hapa nchini na kubaini kwamba kuna kila sababu ya kupunguza pengo kati ya walio nacho na wasio nacho.

Na ili kufanikisha mambo hayo, CCM imeamua kwamba kuanzia sasa itarejesha mfumo wa Upangaji wa Mipango na Usimamizi wa Uchumi ili kuipa dola nafasi ya kuwa mhimili wa uchumi katika mazingira ya ujenzi wa msingi wa uchumi wa kisasa wa Ujamaa na Kujitegemea katika mazingira ya uchumi wa soko na utandawazi.

Maamuzi hayo yamo katika madokezo yake kadhaa, ambayo yalipitishwa na Halmashauri Kuu ya CCM kabla ya kuwasilishwa katika Mkutano Mkuu wa chama hicho uliomalizika mwishoni mwa wiki mjini Dodoma.

Maamuzi hayo, yanaonekana kwamba Tanzania imeamua kufuata mfumo wa uchumi wa China; nchi ambayo Ujamaa pamoja na Ubepari vinafanya kazi sambamba, huku nguvu ya kiuchumi ya mabepari ikisaidia kupambana na umaskini wa walio wengi.

Tangu mageuzi hayo ya kukumbatia mifumo miwili ndani ya nchi moja yaasisiwe mwaka 1978, China imepiga hatua kubwa katika maendeleo ya uchumi. Mwaka jana, pato la nchi hiyo lilikuwa Yuan trilioni 30.07 ambazo ni sawa na dola za Marekani trilioni 4.287, ikiwa na ongezeko la uchumi la asilimia 9.3.

Mageuzi hayo, yaliletwa na Den Xiao Ping, ambaye alibadilisha mfumo wa Kikomunisti uliokuwa umeitenga China ya Mao Tse Dong na ulimwengu wa nje.

Baada ya mabadiliko hayo, uchumi wa China umekuwa ukikua kwa kasi ya ajabu, kiasi cha kuwa tishio kwa mataifa makubwa kiuchumi kama vile Marekani na Japan.

Katika kijitabu cha CCM cha Mwelekeo wa Sera za CCM katika Miaka ya 2010 hadi 2020, CCM inataja malengo makuu ya mwelekeo huo ambayo yana mambo kama sita hivi.

Baadhi ya mambo hayo ni pamoja na kupambana kikamilifu na suala la uchumi duni na tegemezi, kwa kujenga msingi wa uchumi wa kisasa wa Taifa linalojitegemea, na unaozingatia matumizi ya kiwango cha juu cha maarifa yatokanayo na sayansi na teknolojia.

Ili kuweza kufanikisha jambo hilo, chama kinaziagiza Serikali zake kujipanga kuwawezesha wananchi kiuchumi, kwa kuwapa elimu ya kisasa itakayowawezesha kufanikisha Mapinduzi katika Kilimo na Ujasiriamali.

Chama hicho kinasema ili mkakati wa kujenga msingi wa uchumi wa kisasa wa Taifa linalojitegema, ni lazima itolewe elimu ya kisasa. Na kwa msingi huo, Chama kinaziagiza Serikali zake mbili; Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, kuchungulia upya katika mitaala yake na kuifumua ili kuweza kukumbatia sayansi na teknolojia tangu ngazi ya awali ya mfumo wa elimu.

“Kwa vile uchumi wa kisasa unahitaji watenda kazi wenye ujuzi na maarifa ya sayansi na teknolojia, ni lazima (watenda kazi hao) waandaliwe kwa kupewa elimu bora na ya kisasa,” inasema sehemu ya kijitabu hicho cha Mwelekeo wa CCM.

Aidha, chama hicho kinasema bila matumizi ya elimu ya sayansi na teknolojia, nchi haiwezi kuondokana na uchumi ulio nyuma na tegemezi.

“Kwa hiyo, lazima yafanyike marekebisho katika mitaala ili mafunzo yanayotolewa yapate mwelekeo wa sayansi na teknolojia. Serikali itatilia mkazo uwekezaji wa raslimali katika utafiti na kuufanya utafiti kuwa agenda ya kitaifa kwa kutenga asilimia moja (1%) ya pato ghafi la Taifa, kwa ajili ya utafiti na maendeleo,” inasema sehemu ya kijitabu hicho na kuongeza kuwa lazima Serikali isimamie taratibu za uhawilishaji wa teknolojia na utoaji hakimiliki kwa watafiti na wagunduzi.”

Kwa ujumla, mwelekeo huu unaonyesha dhamira ya CCM katika uwezeshaji wa wananchi mmoja mmoja na katika vikundi.

CCM inasema: “Mkakati mkuu wa uwezeshaji wa kiuchumi wa wananchi, ni ule unaohakikisha kwamba wananchi wenyewe wanamiliki na kuendesha uchumi wa nchi yetu ama mmoja mmoja kwa kupitia vyama vyao huru vya ushirika au kwa kupitia kampuni za wananchi ya ubia.

“Wakati huo huo, Watanzania wenye vipaji wataandaliwa katika fani za uongozi wa uchumi na kuwasaidia watu ambao wako tayari kuthubutu kuchukua hatua za kiuchumi. Kuthubutu kiuchumi, ndiyo chimbuko la msukumo katika uchumi wa kisasa.”

Moja ya mambo ambayo yamekuwa yakimhangaisha Rais Jakaya Kikwete tangu alipokuwa akinadi Ilani ya CCM ya mwaka 2005, ilikuwa ni tatizo la uwezeshaji wa watu wenye uwezo wa kuthubutu. Amerudia kusema mara kadhaa na amerudia tena kwenye mkutano mkuu uliomalizika Dodoma, kwamba benki za biashara si rafiki wa masikini.

Kwa maneno mengine, Mwelekeo huuu wa sasa wa CCM umekuja na majawabu juu ya dukuduku la muda mrefu la Rais Kikwete, la kutafuta uwezeshaji wa watu wenye nia ya kuthubutu kufanya mambo makubwa.

Kwa mujibu wa CCM, kwa mtazamo mpana wa Sera ya Uwezeshaji Kiuchumi, aina ya kwanza ya uwezeshaji ni ile ya mtu mwenyewe kujiwezesha. Yaani mtu anajiwezesha pale anapotambua vipaji alivyonavyo na anaamua kujituma kwa kuvitumia vipaji hivyo.

“Kwa ujumla, elimu yetu hadi hivi sasa imeegemea kwenye kuelimisha watu ili waajiriwe au watumwe. Lazima sasa elimu tunayoitoa kwa vijana wetu ijielekeze kwenye kuandaa watu wenye kujituma. Wanaojiajiri ni watu wanaojituma.

“Kuna vijana wengi wanaomaliza masomo ya sekondari, ya vyuo na hata vyuo vikuu, lakini hawapati kuajiriwa kwa sababu uchumi haupanuki kwa haraka kiasi. Hivyo jambo jema la nchi kuwa na watu wengi, vijana wengi waliosoma vizuri, sasa limeanza kuwa tatizo kwa nchi

“Kuwa na vijana wengi waliosoma, ni nguvu kubwa kwa Taifa. Ili Taifa liweze kuitumia nguvu hiyo kwa maslahi ya vijana wenyewe na kwa maendeleo ya kiuchumi na jamii ya nchi yetu, CCM itazitaka Serikali kuibua Mpango Kabambe wa kuwawezesha kiuchumi vijana wasomi walio tayari kujituma kwa kujiajiri ili watumie nguvu na maarifa waliyonayo,” CCM inaagiza.

Je; ni mpango gani umeandaliwa kwa vijana hawa? Chama hicho kinasema kwamba Serikali italazimika kuwapa mafunzo ya ujasiriamali na yanayohusu shughuli wanazokusudia kuzifanya, lakini pia Serikali iweke utaratibu mwepesi wa kupata mikopo nafuu.

Chama hicho kinasema wale wote watakaokuwa na nia ya kushiriki katika mpango huo, washauriwe kuunda chombo chao cha kushauriana.

“Utaratibu wa aina hii, wa kuwawezesha wasomi na wataalamu kujiajiri, una manufaa mawili kwa Taifa. Kwanza, unatoa ajira ya uhakika kwa wahusika na hivyo kuipunguzia nchi tatizo la watu kukosa ajira na madhara yake, na pili; unawezesha wasomi kutoa mchango chanya katika kujenga uchumi wa kisasa na kuongeza utajiri wa nchi,” inasomeka sehemu ya kijitabu hicho.

Chini ya utaratibu wa kuwawezesha wasomi, wajasiriamali, wafanyabiashara wa kati na wa juu, CCM inaziagiza Serikali zake kuandaa mkakati wa kibenki ambao utawezesha upatikanaji wa mikopo kwa makundi yote hayo.

“Benki nyingi tulizonazo sasa kwa aina ya shughuli zao, ni benki za kibiashara zaidi kuliko zile za kuendeleza sekta za uzalishaji mali, hususan kilimo. Aidha, hutoza riba kubwa. Hivyo ni muhimu Serikali ikahakikisha kuwa kwa makusudi, vinaanzishwa vyombo vya fedha ambavyo vitasaidia kuwawezesha wananchi kwa riba nafuu kuliko ilivyo sasa, ikilenga uanzishwaji wa Benki ya Kilimo, Benki ya Kuendeleza Viwanda na Benki ya kutoa mikopo ya muda mrefu ya ujenzi wa nyumba,” inaagizwa.

WAGOMBEA MCHINGA WATUHUMIANA UCHAWI

Imeandikwa na Rashidi Mtagaruka, Lindi; Tarehe: 25th July 2010 Habari Leo



KAMPENI za kuwania uteuzi wa kugombea ubunge ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) jimbo la Mchinga lililopo Lindi Vijijini, mkoani Lindi, zimeingia sura mpya baada ya mgombea mmoja kumtuhumu mwenzake kuwa mchawi.

Tukio hili lililoshuhudiwa na mwandishi wa habari hizi, lilitokea juzi saa tatu na nusu asubuhi katika ofisi za CCM mjini hapa, lilimhusisha Mbunge anayetetea nafasi yake, Mudhihir Mudhihir ambaye alimuomba Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Muhamed Gwaja kuwaondoa watu watatu wanaofuatana na mgombea mwenzake, Saidi Mtanda.

“Mheshimiwa Mwenyekiti, sina imani na watu walio ndani ya gari ya Mtanda, kwa maana ni wachawi,” alisikika akisema Mudhihir.

Hata hivyo Mtanda ambaye katika kampeni hizo zilizoanza Julai 22 mwaka huu, katika kata za Kiwawa na Milola alikuwa akitumia gari lake binafsi, alipinga pendekezo hilo kwa madai linapingana na kanuni za uchaguzi.

“Mwenyekiti kabla ya kukubaliana naye, kwanza atoe ushahidi wa kauli yake, maana Kanuni za uchaguzi hazijasema mahala popote kwamba mgombea haruhusiwi kuongozana na ndugu zake wakati wa kampeni,” alisema mgombea huyo ambaye ni msaidizi wa Katiku Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba. Mtanda aliongeza kuwa:

”Lakini pia kama Mudhihir mwenyewe si mchawi aliwezaje kuwabaini ndugu zangu katika msafara huo kuwa ni wachawi?”

Baada ya mabishano ya muda mrefu, Mtanda alitumia busara ya kuepusha mzozo huo ambao ulionekana kutaka kuathiri msafara wao uliokuwa ukielekea kata za Rutamba na Nangaru.

Akizungumza na gazeti hili baada ya ndugu hao watatu wa Mtanda kushushwa, Mkurugenzi wa Uchaguzi wilayani humo, Mohammed Nyama alisema haoni sababu ya kushushwa kwa watu hao. “Mudhihir hakupaswa kuwa na wasiwasi kiasi hicho, maana nchi yetu haiamini masuala ya uchawi.

Ninachoshukuru ni kuwa busara zimetumika kuepusha shari katika kampeni,” alisema. Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi anayefuatilia kampeni hizo, baadhi ya wagombea wamekuwa wakipata wakati mgumu kuwashawishi wanachama wa CCM wa jimbo la Mchinga.

Jimbo la Mchinga kwa miaka 15 sasa limekuwa chini ya Mudhihir ambao katika uchaguzi wa mwaka huu wamejitokeza wanachama wengine watano wanaoomba kuteuliwa kuiwakilisha CCM katika jimbo hilo. Mbali ya Mudhihir na Mtanda, wengine ni Mayasa Mikidadi, Khalfan Ng’uto, Said Farahani na mgombea aliyetambuliwa kwa jina moja la Mpwatile.

MGOMBEA AKUTWA NA MGUU WA MTU MAKONGOROSI, CHUNYA, TANZANIA

Mgombea akutwa na mguu wa mtu Mbeya
*Ni wa Chadema aliuficha uani, akamatwa

Na Maregesi Paul

MGOMBEA ubunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), katika Jimbo Jipya la Makongorosi lililoko Wilaya ya Chunya, Mkoa wa Mbeya, George Mtasha (50), amekamatwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya baada ya kukutwa na mguu wa mtu.

Katika tukio hilo, Mtasha ambaye pia ni mwenyekiti mstaafu wa chama hicho Mkoa wa Mbeya, amekamatwa na mwenzake aliyefahamika kwa jina la Paul Mnyambwa (43).

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Adcocate Nyombi, aliiambia MTANZANIA kwa njia ya simu jana kuwa, Mtasha na Mnyambwa walikamatwa jana saa 12.50 alfajiri baada ya polisi kupata taarifa kutoka kwa raia mwema, kwamba watu hao wanamiliki mguu wa mtu.
“Ni kweli kuna watu wawili wakazi Bwawani, Makongorosi Chunya ambao wote ni wafanyabiashara wa madini ya dhahabu, tunawashikilia hapa. Kabla ya kuwatia mbaroni, awali tulipata taarifa kutoka kwa raia wema ambao walitwambia kwamba, watu hao wanamiliki mguu wa mtu kitendo ambacho ni kinyume cha sheria.

“Tulipopata taarifa hizo, vijana wetu kutoka hapa mkoani, walikwenda huko na kufanya upekuzi katika nyumba ya Mtasha ambapo walikuta mguu wa kushoto ukiwa umefukiwa kwenye takataka ndani ya ua wa nyumba yake. Kwa hiyo, hivi tunavyozungumza watuhumiwa wote wameshafikishwa hapa mkoani, tunaendelea kuwahoji ili tujue ni kwa nini wanamiliki mguu huo na wameutoa wapi,” alisema Kamanda Nyombi.

Kwa mujibu wa Kamanda huyo wa polisi, mguu huo ni wa kushoto na ni kipande kilichoanzia gotini hadi kwenye nyayo.

Akizungumzia tukio hilo, Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Mbeya, Shambwee Shitambala, alisema kukamatwa kwa Mtasha ni pigo kwa chama hicho kwa kuwa alikuwa ameahidi kukisaidia chama wakati wa uchaguzi mkuu.

“Taarifa za kukamatwa kwa Mtasha ninazo ila inaonekana kuna mazingira ya kisiasa kwa sababu ni juzi tu amerudisha fomu za kugombea ubunge katika Jimbo la Makongorosi. Katika tukio hili nasikia mtoa taarifa alimpigia simu RPC badala ya OCD wa Chunya, kisha askari polisi wakatoka Mbeya Mjini kuja kuwakamata watuhumiwa Chunya wakati hata hapo Chunya kuna polisi,” alisema Shitambala ambaye kitaaluma ni mwanasheria.

Mtasha amekuwa Mwenyekiti wa Chadema tangu chama hicho kilipoanza kujulikana mkoani Mbeya miaka mingi iliyopita. Aliondolewa katika wadhifa huo Machi mwaka huu baada ya kushindwa katika uchaguzi uliomweka madarakani, Sambwee Shitambala.