Friday, April 10, 2009

NYERERE LIBERATION WEEK IN DAR ES SALAAM

THE FIRST JULIUS NYERERE INTELLECTUAL FESTIVAL WEEK COMMEMORATED BY THE MWALIMU CHAIR

Nyerere, liberation and unity
Message from Issa G. Shivji, Mwalimu Nyerere Professor of Pan-African StudiesIssa G. Shivji (2009-04-09)
http://www.pambazuka.org/en/category/features/55472
cc WikimediaWith Dar es Salaam on the verge of hosting the Julius Nyerere Intellectual Festival Week from Monday 13 April, Issa G. Shivji, Mwalimu Nyerere Professor of Pan-African Studies at the city's university, offers his reflections on the pan-African struggle. Though Africa has undoubtedly suffered from the neoliberal onslaught of the past two decades, Pan-Africanism as a progressive ideology is now firmly back on the historical agenda, Shivji states, uniting in the process the continent's dual quest for unity and liberation.
Speaking at the 40th anniversary of Ghana’s independence, Mwalimu Nyerere said that his generation of African nationalists had set themselves two tasks: liberation and unity. In the first task, that of liberation, they had succeeded, but in the second they had failed. It was now the duty of the post- independence generation to bring about African unity.By liberation Mwalimu meant formal independence from colonialism. In our youthful days we greatly underestimated the importance of formal independence. Yet it was an earthshaking event for a people who had been oppressed and humiliated for four centuries of slavery and a century of colonialism. As C.L.R. James said of Ghana’s independence in 1957, it had 'raised the status of Africa and Africans to a pitch higher than it had ever reached before'.The neoliberal onslaught of the last two or so decades has dramatically brought home to us the significance of Uhuru. But it has also made us wonder, Where is Uhuru? Liberation without unity is incomplete; some would say, not possible. And they would have ample evidence from the neoliberal episode which has proved to be an unabashed attack on African sovereignty, both of the state and the people.Pan-Africanism, African unity, is back on the historical agenda. I would say so is liberation. The new generation of African nationalists can only be pan-Africanists and in pan-Africanism we have the ideology and vision of African (not Tanzanian, or Burkinabe or Algerian) liberation. The twin tasks of liberation and unity are now combined.With the wisdom of hindsight and the experience of half a century of African independence, we should critically reflect on what Nyerere said 50 years ago: ‘African nationalism is meaningless, is anachronistic, and is dangerous, if it is not at the same time Pan-Africanism.' The territorial nationalism of African states, what Nyerere derogatively used to call in Kiswahili 'vinchi' (statelets), is ‘the equivalent of tribalism within the context of our separate national states’. Has he been proved right?The Julius Nyerere Intellectual Festival Week will hopefully provide us with a forum to begin to reflect critically on the pan-Africanist message of the first generation of African nationalists and the experience of independence from the standpoint of the African working people.* Where is Uhuru? by Issa G. Shivji is now available from Fahamu Books.

* Issa G. Shivji is the Mwalimu Nyerere Professor of Pan-African Studies at the University of Dar es Salaam.* Please send comments to editor@pambazuka.org or comment online at http://www.pambazuka.org/.

MTIKISIKO WA UCHUMI WA DUNIA

Imechanginwa na kaka Dan Nkurlu wa Dallas, Texas.

Kibwagizo Kipya...Mtikisiko na kuanguka kwa uchumi wa Dunia

Wimbo wetu ulio bora, ule ule wenye viitikio vingi visivyoleta maana wala mwelekeo umepata kibwagizo kipya “mtikisiko wa Uchumi wa Dunia na kuanguka kwa uchumi wa nchi Tajiri’! Naam, wanasiasa na watendaji wa Tanzania wamepata kibwagizo kipya kuwaimbisha Watanzania wimbo wa uvumilivu wa umasikini wao kwa kudai kuwa hali yetu inaendelea kuwa ngumu kutokana na kutikisika kwa uchumi wa dunia na kuanguka kwa mfumo wa fedha na mabenki katika nchi tajiri.Hebu tafakari, tangu tulipopata Uhuru wetu, tumekuwa tukipata kibwagizo kipya kila siku kuhalalishiwa umasikini na uduni wetu kila siku kutoka kwa watu tuliowapa dhamana ya kutuongoza.Tulianza na ukabaila, tukaja na ukoloni, tukaupandisha madaraja kadhaa, kama vile ukoloni mamboleo, ubwanyenye, ubepari, ikaja hekaya ya uchanga wetu, ukosefu wa wataalamu wa kutosha, ikaja unyonyaji tulioufuta kwa kutumia Azimio la Arusha, kukawa na maasi ya jeshi, uasi wa kina Kambona, kifo cha Karume, vijiji vya ujamaa, maduka ya ushirika, bei za mafuta 1974, ukame, vita vya Kagera, Makaburu, Walowezi, Manyang’au wa Kenya na kuanguka kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ulanguzi, uhujumu uchumi, uhaini, mpasuko wa chama, ruksa, kutokwajibika, Benki ya Dunia, Vyama vingi, uwekezaji, kodi, mikataba ya madini, utalii, umeme wa shida, bei za mafuta, ufisadi, VAT, mvua, ukame, ubinafsishaji na sasa tunalaumu kuanguka kwa uchumi wa dunia!Hivi, katika sababu zote hizi, ni lini tuliweza kuamka, kujipangusa vumbi na kuanza kupiga hatua kwa kujifunza kujikinga na dhoruba kwa yaliyotukumba na kujijenga kwa uimara na kinga kama ule wimbo maarufu wa mipira ya kiume wa “Salama, chaguo la Kisasa, Salama kinga njema”? Ni lini tulijipima nguvu zetu kwa dhati na kutumia bidii zetu zote, zikiandamana na maarifa na ufanisi na fikra bora kujiimarisha kutoka umasikini na unyonge?Yaani ina maana katika miaka karibu 50 tangu tujitawale, bado hatujaweza kuvumbua njia bora ya kujiimarisha kiuchumi bila kulaumu wengine kwa udhaifu na umasikini wetu?Majuzi, mamlaka ya ukusanyaji kodi na mapato ya Taifa maarufu kama TRA, imetamka kuwa ilitarajia kukusanya mapato ya Takriban Shilingi Trilioni 2.62 katika kipindi cha miezi 6 iliyopita, lakini imeweza kukusanya Shilingi Trilioni 2.45 na kupungukiwa mapato ya Shilingi Bilioni 200.00. TRA imesema kuwa kupungukiwa kwao kukusanya mapato haya, kumetokana na mtikisiko na kuanguka kwa Uchumi wa Dunia! Nimepiga mahesabu ya haraka haraka na kubaini kuwa TRA wamekusanya takriban asilimia 94 (94%) ya makisio au makadirio ya mahesabu yao, nikajiuliza, je kupungukiwa kwa asilimia 6 (6%) ni kweli kumetokana na kusuasua kwa uchumi wa dunia? na jee mtikisiko huu utatuumiza kiasi gani kwa kupungukiwa asilimia 6 ya mapato mpaka tuanze kusema hatuna pesa za kununulia madawa?Nikakumbuka Serikali ilisitisha kununua magari mapya, na hili limeokoa fedha nyingi tuu, hivyo basi pengo la 6% litajiziba! Zaidi, ni kuwa Mwezi Januari ya mwaka huu 2009, mapato yaliyokusanywa na TRA yalikuwa ni asilimia 23 (23%) zaidi ya mapato yaliyokusanywa mwezi januari ya mwaka 2008! Sasa kama uchumi wa dunia ambao tunajua ulianza kuyumba mwezi wa Septemba 2008, ulikuwa ni mbaya iweje mapato ya mwezi Januari 2009 yawe makubwa marudufu kuliko mapato ya Januari 2008?Je Serikali yetu imewahi hata mara moja kubana na kupunguza matumizi yake ambayo mara nyingi si kwa manufaa ya Taifa? Ikiwa ripoti za Utoh, mdhibiti mkuu wa mahesabu wa Serikali zinaonyesha matumizi mabaya na kukosekana kwa uhakiki na uadilifu katika kuthibitisha matumizi au kuweka kumbukumbu za matumizi kwa mujibu wa kanuni za mahesabu na kihasibu, ni vipi leo tulaumu kuyumba kwa uchumi wa Dunia kama mapato yetu yamepungua lakini hatjali jinsi tunavyoyatumia kwa kuwa tumejijengea umaarufu wa kufuja, tunakodai "Pondamali, kufa kwaja"?Nikakumbuka kauli za Rais Kikwete mwaka huu 2009, katika kipindi cha miezi miwili iliyopita ambapo aliashiria kuwa kushindwa kwa Tanzania kujinasua kiuchumi, kunatokana na hali mbaya ya uchumi duniani. Kwanza alitangaza kuomba stimuli kutoka kwa nchi tajiri, akisema ni lazima na sisi tupewe mgawo wa fedha kusisimua na kufufua uchumi wetu, baadaye akalaumu bei ya mafuta kuwa ghali sana na hivyo kutuangamiza kiuchumi.Bei ya mafuta Duniani, imeshuka tangu Julai 31 2008 ambapo pipa moja lilikuwa likiuzwa kwa Dola za Kimarekani 145, mpaka bei ya leo hii April 6 2009 ambapo pipa ni Dola za Kimarekani 52, hii ikiwa ni punguzo la asilimia 65 (65%) katika kipindi cha miezi 10! Sasa najiuliza, kama kwa miezi 10 bei ilishuka mpaka ikafika dola 33 Disemba 30 2008, iweje tuendelee kulaumu bei za mafuta kuwa ghali? Je kama bei ya mguu wa ng’ombe imeshuka, kiasi kuweza kununua miguu mitatu badala ya mmoja kwa gharama hiyo hiyo, hivi tutaendelea kulia kuwa hatuna uwezo wa kujipatia Protini za kutosha?Kila kiongozi na mtendaji wa Tanzania anakimbilia kuimba kibwagizo kipya, “uchumi wa dunia”, najiuliza ni lini tutajiangalia ndani na kubaini kuwa hatujaathirika sana na tunaweza kupona? Nitaelewa kuwa tunaumia kama mfumo wetu huu mpya wa uchumi wa soko huria na uwekezaji ungekuwa umeshafikia hatua kuwa wawekezaji wote wameulaza na kutuachia majengo na mashimo matupo huku wao wakiwa wamekimbia na hela. Lakini hilo si kweli kwa kuwa tumeambiwa majuzi kuwa yale makampuni ya uchimbaji dhahabu, yalijikusanyia mapato ya Dola Bilioni 3 na Seikali yetu ikaambulia mapato ya Dola milioni 1 ikiwa ni asilimia 3 (3%) tuu! Baya zaidi kwa hawa waimbishaji wa kibwagizo kipya wanaendela kutafuta mbinu za kuwapa wawekezaji ahueni na kutupunguzia mapato. Ole Naiko katangaza wiki mbili zilizopita kuwa TRA na TIC wanaunda kamati ya kuwapa Wawekezaji mfumo bora na wa unafuu wa kodi! Astaghafulahi, leo tunalia tuna mapato duni, bado tunafikiria kupunguza mapato kwa kutoa misamaha ya kodi?Ni lini tutajifunza kutokana na makosa tuliyoyafanya hapo kale? Ni lini Watanzania na hasa Viongozi wetu na Watendaji watabadilisha mitazamo yao na ufikiri wao na kuanza kukubali kuwa jawabu pekee la Tanzania kuendelea si visingizio bali ni kuongeza uzalishaji mali wa ndani ambao utatokana na jasho letu na juhudi zetu na si kutegemea misaada au kulalama kuwa kuungua kwa mwingine, kumeangamiza nyanya zetu zilizo kilometa 100 mbali na kwetu na tunachokiona ni moshi angani?Sina maana ya kukataa kuwa Uchumi haujayumba Duniani, lakini si kweli kuwa Tanzania inashindwa kupiga hatua mbele kwa kuwa Mabenki ya Marekani yanafilisika. Serikali yetu badala ya kuweka kipaumbele kujenga mfumo mzuri na bora wa uzalishaji mali , kama vile Rwanda walivyoamka, imeendelea kupitisha bakuli kuombaomba kila kona. Mizengo Pinda akiwa Ireland akitembelea wafugaji na wakulima, aliomba misaada na kukaribisha wawekezaji. Je ni lini ametoa ruzuku ya maana kwa yule mkulima kule Simanjiro ili ajinunulie pembejeo au alipwe bei bora ya mazao yake? Viongozi wetu wamebakia kuwa mapambo, watalii na omba omba, kutwa kucha kupiga domo bila kufanya kazi wala kutoka jasho kuona kuwa kuna ulazima wa kubadilika vitendo na tabia kama tunataka Taifa letu lipate maendeleo ya kweli.Benki Kuu majuzi imetoa takwimu kuwa kilimo kinaingizia Taifa letu asilimia 26 (26%) ya mapato yake kutokana na mauzo ya mazao yetu. Asilimia 80 (80%) ya Watanzania wanaishi vijijini, wakijilimia kijima na zile zama za kale za mawe! Kwa nini basi kama Watanzania Milioni 30 wanaishi vijijini na takriban nusu yao wana uwezo wa kuzalisha mali, kwa nini tunaendelea kuagiza vyakula kutoka nje ya nchi na si kuzalisha kwa ziada na kuuza nje ya nchi ili tusikumbwe na mtikisiko wa Dunia?Marekani, Uingereza, Uchina, Ujapan na nchi zote tajiri, bado zinahitaji chakula, migahawa yao bado inauza Kahawa na Chai, inahitaji maharage, nyanya, bamia, vitunguu, viwanda vyao vya nguo vinahitaji pamba, nyumba na maofisi na watu wao wanapenda maua na matunda. Hata Kenya , Congo na Zambia , wanahitaji Chakula! Oman wanakodisha ardhi Kenya walime chakula, sasa iweje tusema hatuwezi kujikwamua kiuchumi kisa Mabenki ya Marekani yamefilisika kutokana na uzembe na ukosefu wa maadili, gonjwa ambalo ni kubwa nchini mwetu?Nilichojifunza kutokana na kuanguka kwa Uchumi wa Dunia safari hii, ni kuwa kama nchi yangu ni mzalishaji imara na fanisi, haiwezi kutikiswa kutokana na njaa ya jirani! Nimejifunza kuwa Watendaji wengi wetu, ama ni Wasomi Wajinga au ni Mapunguani fuata Upepo wasio na uwezo wa kukaa chini na kufikiria kwa kina njia rahisi na madhubuti za kuongeza uzalishaji huku ukipunguza matumizi yasiyo na maana!Leo hii Singapore , Spain na Ireland ambazo zilijenga uchumi wao kutokana na uwekezaji wa Soko huria, wamekuwa ni wa kwanza kupiga yowe la kichaga lile la “yewomi, yeleuwi”, uchumi wao ukiteketea kutokana na wawekezaji kukimbia na kwenda kwenye soko la bei nafuu kuzalisha!Sisi tumeambiwa,tujifunge mkanda, tujikaze kiume, tuvumilie, tuhimili makali ya umasikini yanayoongezeka kutokana na kuyumba, kutikisika na kuanguka kwa uchumi wa dunia!Uuwi, Yewomi, yeleuwi, wimbo ni ule ule, tumepata Kibwagizo kipya, tuvumilie machungu na tunogewe na umasikini wetu kwa kuwa Uchumi wa Dunia Umeyumba na Kutikisika!

Thank you and have a wonderful day.Dan A. NkurluOperations Manager, Dallas Cash VaultWells Fargo Bank-CSSO1201 Main Street , Mac T5323-011Dallas , TX 75202Office: 214-761-0333Fax: 214-761-0326Cell: 612-708-1529Dan.Nkurlu@Wellsfargo.Com

JAJI WA MAHAKAMA YA RUFAA HAONI TABU KUJIFULIA NGUO

Leo nina habari za Jaji Mweusi Pekee katika Mahakama ya Rufaa ya Shirikisho nchini Marekani (United States Supreme Court) Mheshimiwa Jaji Clarence Thomas ambaye gazeti la "The Examiner" la Washington DC, la tarehe 2 Aprili, 2009 lilimnukuu juu ya mambo mengi tu kama ifuatavyo; kama alivyonukuliwa katika Hafla ya Jioni (gala) ya Asasi ya Haki za Binadamu (Bill of Rights Institute): Kwa bati alilopiga kichwani (mvi), naweza kuthubutu kusema kuwa ana umri wa miongo kama 6 hivi au keshaimaliza (60s).

"This is a rare sighting for me to be out during the week, especially a sitting week," akiwa na maana kwamba ni nadra sana yeye kukubali mialiko kama hii wakati Mahakama ikiwa kazini. Yaani anakuwa bize sana na kazi za kusoma kesi, kusikiliza kesi na kuandaa hukumu za kesi wakati huo.

"I would like to thank my bride for being here. We have been a team for a while and enjoy each other a lot, ... I tend to be morose; she tends to be energetic." Hapa ana maana kwamba anamshukuru sana mkewe aliyenaye na ambaye wamekuwa kama timu, wakati yeye akiwa anatafakari mambo ya kisheria, mkewe anakuwa mchangamfu kwa maana ya kwamba hawi kikwazo katika utendaji wake wa kazi za kila siku na wala halalamiki kwa hilo.

Anasema anapojisikia kulemewa na majukumu yake, "when he feels down" huwa anamgeukia mkewe "what I tell my wife is the 'Inter-Net', and I look up great speeches, like General Douglas MacArthur's speech at West Point." Hapa huenda akawa ana maana kwamba mkewe humsaidia katika kuzisikiliza au kupekuwa kwenye tovuti, Hotuba za waliomtangulia kama ya Kamanda huyu maarufu wa majeshi aliyemtaja.

Na itokeapo kwamba mambo yanakuwa kama kawaida, huwa anakwenda "pangoni" (basement) kuangalia mchezo wa kuigiza wa Televisheni wa "Saving Private Ryan".

Kwa sisi Waafrika hatuna mfano wa hili pango ninalozungumzia hapa. Huku Marekani, nyumba nyingi huanzia ghorofa moja au zaidi chini ya ardhi. Zinazoitwa Basement. Kama kwa mfano sehemu niliyopanga mimi. Naishi chini ya nyumba na hii ni studio basement kwa sababu inajitegemea (haichangii mlango wala maliwato. Ndio kwa DC nalipia $1,200 kwa mwezi. Kwa fedha zetu kwa wastani tu ni sawa na Tshs.1,200,000/=) za Tanzania. Pango la nyumba katika jiji hili kuu la Serikali hii ni kiboko.

Mheshimiwa huyu anaendelea kusema "I have to admit that I am one of those people that thinks the dishwasher is a miracle, I like to load it." Yaani, anakiri kwamba yeye ni kati ya watu wanaofikiri kwamba mashine ya kuoshea vyombo ni muujiza, hivyo anapenda sana kupangilia vyombo humo ili vioshwe na mashine hiyo.

"I still take out the trash, and me and my wife go to football games. We go motor-homing."
Mheshimiwa anasema hadi leo hii bado anakusanya na kutupa taka za nyumbani mwake, na pia huenda kuangalia michezo na mkewe. Pia wanapenda kuishi katika gari.


Kuishi katika gari huku Marekani ni sehemu ya utamaduni wao. Yaani mtu anakodi au ananunua gari/nyumba, gari hizi ni kama nyumba kwa sababu zina kila aina ya huduma ya nyumba ndani yake. Kwa hiyo ukiwa na gari kama hii, unaweza kuamua kwenda utakako, bila ya kuwa na gharama ya malipo ya malazi wala kula hoteli. Wapo watu nchini Marekani wanaoishi maisha yao yote katika nyumba zitembeazo kama hizi. Na wengine nyumba hizi huzipigia kambi ( kambi zinalipiwa) kwa maana ya kwamba mtu anaweza akapiga kambi katika nyumba hiyo bila ya kulazimika kutembea nayo. Na hizi kambi zipo katika miji maalum na sehemu maalum zilizotengwa kwa ajili ya gari za aina hii kupiga kambi. Kwa watembeao kama Mheshimiwa huyu, anapofika katika kambi hizi, inabidi alipie kwa siku, au wiki, au mwezi, n.k.

Alipoulizwa maoni yake juu ya Mahakama Kuu kabisa ya Marekani na jinsi ilivyombadilisha akajibu "not a whole lot. It's changed my hair. It's given me some girth." Anajibu kwamba Mahakama imemzeesha kwa kumuongezea bati alilo nalo kichwani (mvi) na kwamba imemuongezea uzito (kwamba sasa amenenepa). Mheshimiwa huyu hapa ana maana ya kwamba uzito wa kazi za Mahakama hii haumpi nafasi ya kutosha ya kufanya mazoezi, na kwamba kule kufikiri sana masuala mazito ya kesi wanazoshughulikia ndio zimemuongezea mbuliza (mvi)

Juu ya kazi yake ya Ujaji anasema "This job - it's easy for people who have never done it. What I've found is they know more about it than I do. Espeically if they have the title of law professor." Anasema kazi yaonekana rahisi kwa watu wasioifanya. Nimegundua kwamba walimu wa sheria wanaifahamu zaidi kazi hii kuliko mimi. (hapa bila shaka alikuwa anatania kwa sababu mjuaji wa kazi yoyote ni mtendaji kazi ile, sio mjua nadharia yake).

Mahakama ya Juu kabisa ya Rufani nchini Marekani ina majaji tisa tu. Katika Chumba cha Mahakama Majaji hawa hukaa kwa uzoefu wao (seniority). Jaji Mkuu anakaa kiti cha katikati. Anayemfuata anakaa kulia kwake, na kushoto kwake atakaa anayemfuata huyu. Na kulia kwake ni hivyo hadi wote waketi. Mheshimiwa jaji Clarence Thomas hukaa upande wa kulia (kwa Jaji Mkuu) wa meza ya majaji kabla ya Jaji wa mwisho kulia kwake.

Mheshimiwa Jaji huyu katika Kesi za Mahakama hii huwa ni Msikilizaji tu. Huwa haulizi maswali japo hii ni fursa kwa Majaji kuuliza swali lolote kwa mtoa hoja awe mtetezi au mshitaki.

MAJUMBA YA MAKUMBUSHO WASHINGTON DC

Tarehe 9 Aprili, 2009 niliwahi kupata fursa ya kutembelea makumbusho Kadhaa hapa Washington DC, ambayo kwa bahati nzuri yote ni bure. Gharama yako ni usafiri kwenda na kurudi.

Nikaamua kutembelea makumbusho ya National Museum of African Art, yaliyopo 950 Independence Ave. SW, Washington DC. Nilipofika tu mlangoni baada ya kusachiwa, kitu cha kwanza nilichokiona kulia kwangu ukutani ni KANGA NZITO YA NIDA DSM!

Hapo nikasema ama kweli na sisi tunakumbukwa huku Marekani. Nilipouliza Mapokezi nikaambiwa kuwa kanga hiyo ilitengenezwa mahsusi kwa ajili ya Siku ya Kuapishwa kwa Rais Barack Hussein Obama, na kwamba hakuna doti za biashara dukani kwao. Na kweli ilikuwa na picha ya Obama katikati na maandishi yake yalisema hivi: 'UPENDO NA AMANI AMETUJALIA MUNGU'. Kisha katika kibao cha maelezo wakatafsiri usemi huo katika kiingereza "God has blessed us with Love and Peace". Kwa kweli nilifurahi sana kuona alama ya utamaduni wa Mtanzania katika Makumbusho haya. Kwa bahati mbaya sehemu muhimu sana ya Makumbusho haya inafanyiwa Ukarabati Mkubwa kwa sasa kiasi kwamba sikuweza kuzunguuka zaidi ili nione vilivyomo humo kwa sababu kwenye ukarabati ni sehemu iliyokatazwa kuingia.

Hata hivyo pia niliwahi kutembelea THE SMITHSONIAN CASTLE ambayo ndio makao makuu ya Makumbusho yote nchini Marekani yaitwayo "Smithsonian". Makumbusho yote yenye jina hili ni bure kwa sababu ni Urithi wa Marekeni kutoka kwa Bwana wa Kiingereza mwenye jina hili "Smithson". Bwana huyu aliishi katika karne ya 19 nchini Uingereza. Bwana huyu hajawahi kufika Marekani. Yeye alikuwa ni Muingereza. Bara la Amerika alilisikia tu kutoka kwa wenzie na habari mbalimbali vitabuni. Aliamua kurithisha mali zake zote baada ya kufa kwake kwa Wamarekani baada ya kukataliwa kuwamo katika kundi la Wateule (Royalty) wa Uingereza kwa sababu yeye alikuwa kilokote (mtoto wa nje ya ndoa). Kwa sababu hii, hakuwa na haki ya kurithi utajiri mkubwa wa baba yake. Alifanya jitihada sana katika maisha katika taaluma ya tafiti mambo mbalimbali baada ya kufanikiwa kulimbikiza mali nyingi tu.

Hivyo alipofariki 1829, Waosia wake uliposomwa juu ya kurithishwa huku, ndio sababu Bunge la Marekani likatunga sheria kufanya mali yake ni kwa ajili ya Makumbusho ya Watu Wote kwa kutotoza gharama yoyote katika Makumbusho hayo. Hadi sasa, yapo majumba ya Makumbusho 17 yaliyo chini ya Asasi hii ya Smithsonian jijini Wasington DC, USA. Sehemu kubwa ya Makumbusho haya yapo mtaa huu wa "Uhuru.", unaotazama uwanja maarufu wa kitaifa nchini Marekani "The Mall" . Hii "Mall" ni kiasi cha kilometa tatu za urefu, na upana unaofanana na upana wa Uwanja wa Mnazi Mmoja Dar es Salaam. Uwanja huu ndio ulijaa umati wa watu siku alipoapishwa Rais Barack Obama Jauari 20, 2009 na kuvunja rekodi ya kujaza uwanja (crowd-puller) kwa Marais wote walipita wa Marekani.

Makumbusho mengine yaliyojaa elimu kedekede ni yale ya National Museum of Natural History. Humu mna historia ya Sayari yetu dunia tangu viumbe hai vilipoanza hadi tulipo sisi binadamu na hadi tunavyojimaliza, pamoja na kupungua kwa nguvu ya jua na kuiacha dunia tupu miaka milioni nne na nusu ijayo. Kunaonyeshwa pia viumbe hai walivyoanzia baharini, waliopukutika/waliopotea (extinct) na waliopo sasa. Pia kuna bustani ya Darwin ya maua ya Orchids. Bustani hii ni hai na inatunzwa kila siku. Humo katika bustani kunanukia vizuri sana mauwa haya, ambayo yako katika aina mbalimbali na rangi mbalimbali.

Jumla ya Makumbusho ya Smithsonian, kama yalivyoorodheshwa katika kitabu cha Washington DC Official Guide Winter/Spring, 2009 kinachotolewa na Washington DC Convention and Tourism Corporation ni kama ifuatavyo:

1. Anacostia Community Museum. Hii Makumbusho imo ndani ya nyumba iliyokuwa ya Mheshimiwa Frederick Douglas, Mmarekani Mweusi wa karne ya 19 aliyeukataa Udhalilishwaji wa Watu weusi nchini Marekani. Yeye alimtumia rafiki yake Mmarekani mweupe kumnunulia nyumba hii kwa kuwa wakati huo Mtu Mweusi Marekani hakuruhusiwa kununua nyumba. Rafiki yake Mweupe akamnunulia nyumba hiyo kisha kumkabidhi na hati zake.

2. Freer Gallery of Art and Arthur M. Sackler Gallery
3. Hirshhorn Museum & sculpture Garden (humu mna masanamu yakiwa kichele)
4. National Air and Space Museum
5. National Air and Space Museum Steven F. Udvar-Hazy Center
6. National Museum of African Art (humu mna Kanga ya Tanzania)
7. National Museum of American History
8. National Museum of Natural History
9. National Museum of The American Indian (mna mkataba wa Geronnimo)
10. National Portrait Gallery (humu iko picha ya Angelina Jolie)
11. National Postal Museum
12. National Zoological Park (humu mna Panda wa China)
13. Fenwick Gallery of the Smithsonian American Art Museum
14. Smithsonian American Art Museum
15. Arts & Industries Building
16. Smithsonian Associates
17. Smithsonian Institution Information Center.

KIPIMO CHA SARATANI YA MATITI (MAMMOGRAM) MAREKANI

Leo nawafahamisha kuhusu kipimo tajwa kinavyofanywa huku kulikoendelea.

Nilifika kwenye kitua cha kutolea huduma hii kiitwacho Washington Radiology Associates, P.C. kilichpo Chase Tower, 4445 Willard Avenue, suite 200, Chevy Chase, Maryland 20815. Msishangae kwamba nimesema ni Washington DC. Kwa sababu DC imepatikana kutoka jimbo la Maryland katika historia yao. Kwa hiyo pamoja na kwamba kituo hiki kiko Maryland, kiko jirani (mpakani) kabisa na jimbo hilo ndio maana nasema hivyo.

Muda wangu wa kumuona mtaalam (Radiologist) mhusika ulipofika akaniita jina. Huyu ni Dr. Lee wa Washington Radiology Associates, P.C., Chase Tower, 4445 Willard Avenue, Suite 200, Chevy Chase, Maryland 20815. Nikamfuata alikokuwa akielekea. Akanifikisha katika chumba kidogo (cubicle) na kunifahamisha niondoe nguo zote za juu ya tumbo; yaani kifua kiwe wazi. Nikafanya hivyo na kuelekezwa nijivalie joho nililolikuta katika plastiki, kwa maelezo kwamba, baada ya kulitumia, nilitie katika kikapu ndani ya chumba hicho.

Akanichukua hadi chumba cha kipimo. Katika Upimaji matiti, mashine ya mammogram imesimamishwa hivyo hata kipima chake ni kupima ukiwa umesimama. Kuna vipimo vya aina tatu. Kwanza unapimwa sehemu nzima ya mbele ya kifua ikichanganya matiti yote mawili. Kisha unapimwa titi moja moja kwa ubavuni kwake. Kwa kuwa upimaji huu unagandamiza sehemu hizi nyeti za wanawake, kuna hisia za uchungu kiasi fulani. Kwa kuwa maumivu haya huchukua muda mfupi na kwa kuwa kile ni kipimo kwa ajili ya afya zetu, hayo yote yanakuwa si kitu. Ili mradi mtu upate tiba.

Baada ya kunipima akaniarifu kuwa nitarajie majibu toka kwa dakitari wangu aliyenipima Pap Smear Dr. Andrew Engel wa Foxhall OB/GYN Associates, P.C., 4910 Massachusetts Ave. NW. , Suite 112, Washington DC 20016-4368, Washington DC, USA. Kwamba yeye akishapata majibu ya kipimo changu, atakipeleka kwa Dakitari aliyenipeleka kwake. Kipimo hiki kinagharimu $300.

Huu haukuwa mwisho wa kipimo hiki. Wiki mbili baadaye nikaitwa tena kuhakikisha kipimo hicho hicho. Safari hii ya pili baada ya kupimwa, Dr. Ingrid Ott wa taasisi hii akajihakikishia zaidi kwa kuchukua maji yaliyomo ndani ya "cyst" kwa kuyafyonza na sindano. Maji hayo yalionyesha rangi ya njano kavu. Baada ya kuyachunguza akaniambia niko salama. Hata hivyo kwa watu wa umri wangu wa miaka 55 akasema inabidi niache kutumia vyakula vitokanavyo na wanyama (dairy products) kama vile maziwa, jibini, mtindi, na nyama yenyewe; vyakula ambavyo kwa asili yetu Walugulu wa Morogoro huwa ni nadra sana kuvihudhurisha katika milo ya kila siku.

Kisha nikapewa picha zote nilizopigwa siku ile (x-ray, ultra-sound) na kushauriwa kuwa niwe natembea nazo ili nikienda kwenye kipimo kama hicho mwakani, dakitari aweze kuzisoma na kuangalia kama kuna tofauti yeyote itakayojitokeza. Yaani nimrahisishie kazi endapo kutajitokeza tofauti ya hali iliyopo sasa.

TEMBO SHAMBA LA WANYAMA NCHINI POLAND

Walalamikaji katika habari hii hawakuchukua tahadhari ya kufanya utafiti kwanza kujua endapo tembo hubaleghe miaka mingapi ili atafute mwenza kwa ajili ya kuzaliana.

Polish politician fumes over "gay" elephant in zoo - Hii si kweli. Ni jitihada za Mashoga kutulazimisha tuamini kwamba wapo wanyama Shoga.

A Polish politician has criticised his local zoo for acquiring a "gay" elephant named Ninio who prefers male companions and will probably not procreate, local media reported on Friday. Skip related content

"We didn't pay 37 million zlotys (7.6 million pounds) for the largest elephant house in Europe to have a gay elephant live there," Michal Grzes, a conservative councillor in the city of Poznan in western Poland, was quoted as saying.

"We were supposed to have a herd, but as Ninio prefers male friends over females how will he produce offspring?" said Grzes, who is from the right-wing opposition Law and Justice party.

The head of the Poznan zoo said 10-year-old Ninio may be too young to decide whether he prefers males or females as elephants only reach sexual maturity at 14.

(Reporting by Chris Borowski; editing by Andrew Roche)

Thursday, April 9, 2009

JENNIFER LOPEZ WINS CYBER WAR ON COPYRIGHT

Jennifer Lopez wins cybersquatting case

American singer and actress Jennifer Lopez has won a cybersquatting case against a U.S. web operator who registered two Internet addresses that used her name for commercial profit, a U.N. agency said on Thursday.

The disputed domain names, jenniferlopez.net and jenniferlopez.org, directed users to a website that generated paid advertising revenues, according to the ruling issued by the World Intellectual Property Organisation (WIPO).

An independent arbitrator ordered the domain names transferred within 10 days to the Jennifer Lopez Foundation, which filed the complaint. The charitable foundation promotes better access to healthcare for women and children.

The Grammy-nominated singer, widely known as J.Lo, joins other celebrities in ousting cybersquatters through the dispute procedure, including Pierce Brosnan, Tom Cruise, Celine Dion, Scarlett Johansson, Nicole Kidman, Madonna and Julia Roberts.

Lopez, who is from the South Bronx, registered her name as a trademark in the United States in May 1999 and has sold more than 48 million albums worldwide, according to her complaint.

A man based in Phoenix, Arizona, named as Jeremiah Tieman, registered both domain names and asserted that he ran primarily a fan site devoted to providing news and information about the star, according to the arbitrator, Williams Towns.

Tieman "registered two domain names that are identical to the complainant's mark and has used those domain names to attract Internet users to a website from which (he) generates pay-per-click advertising," Towns said in his ruling.

The American arbitrator found that the registration had been for commercial use and was in bad faith.

Lopez, 39, and her husband, salsa singer Marc Anthony, had twins in February. It is her third marriage. The couple starred together in "El Cantante," a 2006 film about salsa legend Hector Lavoe.

(For the full WIPO arbitration report go to: http://www.wipo.int/amc/en/domains/decisions/html/2009/d2009-0057.html )

(Reporting by Stephanie Nebehay; Editing by Jonathan Lynn)