Wednesday, April 24, 2013

MAREHEMU PROFESA MICHAEL WAMBALI [UDSM] AAGWA !

Imetundikwa hapa tarehe 24/4/2013

KWA  HERI  MWALIMU WETU  PROFESA  MICHAEL  WAMBALI

WAZIRI MKUU Mizengo Pinda ameongoza mamia ya waombolezaji kuuaga mwili wa aliyekuwa Mhadhiri wa Shule Kuu ya Sheria ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, na wakili maarufu Profesa Michael Wambali ambaye alifariki dunia Aprili 4, 2013 katika hospitali ya Taifa Muhimbili kutokana na majeraha aliyoyapata kwenye ajali ya gari.


Shughuli ya kuuaga rasmi mwili wa marehemu Profesa Wambali ilifanyika leo asubuhi (Jumatatu, Aprili 8, 2013) kwenye ukumbi wa Nkrumah, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kabla ya kupelekwa kanisani kwa misa maalum.
Akizungumza na waombolezaji hao kabla ya kutoa heshima za mwisho, Waziri Mkuu alisema mchango wa Prefesa Wambali kwenye fani ya sheria ni mkubwa mno na hauelezeki. “Kama walimu wenzake wangeamua kuhesabu idadi ya wanafunzi ambao Profesa Wambali aliwafundisha, ni dhahiri kuwa idadi yao ingekuwa kubwa kuliko tunavyoweza kufikiria,” alisema.
“Juzi tu tarehe 29 Machi, ametimiza miaka 59 ya kuzaliwa na siku sita baadaye akaaga dunia, lakini katika kipindi cha miaka yake 59 ni miaka 32 ambayo aliitumia hapa chuoni. Hapa tulipo wapo Majaji, Mawakili wa Serikali na wa kujitegemea, mahakimu na wengine wako mikoani wameshindwa kufika hapa leo… lakini wote hawa wamefundishwa na Prof. Wambali katika kipindi cha miaka 32 aliyokaa hapa chuoni,” alisema.
Alisema fani ya sheria imepoteza kiongozi makini na mfano wa kuigwa. “Tumepoteza kiongozi mzuri na makini siyo kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam peke yake bali ni kwa Tanzania yote,” aliongeza.

Aliwasihi wanafamilia waikubali hali ya kuondokewa na mpendwa wao, wajipe matumaini kwamba mwenzao ametangulia na akawataka waendelee kumuombea kwa Mungu ili ampokee huko mbinguni.

Kwa wanafunzi wa wafanyakazi wa Shule Kuu ya Sheria, Waziri Mkuu alikuwa na haya ya kusema: “Ingawa Profesa Wambali ameondoka, ninaamini bado ataendelea kuwa nasi kwani ametuachia kazi zake nyingi za kimaandishi ambazo zitatumiwa na wengine katika siku zijazo. Tukienzi hilo, tutakuwa tunaendeleza yale aliyokuwa akiyasimamia.”

Naye Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Dk. Asha-Rose Migiro ambaye aliwahi kufanya kazi na Profesa Wambali miaka ya 80, wakati akitoa nasaha zake alisema alifanya naye kazi ofisi moja na waliwahi kufundisha masomo ya aina moja.



Dk. Migiro alisema kila aliyewahi kuwa mwanafunzi wa Prof. Wambali hawezi kuacha kumkumbuka. “Hatuwezi kumrudisha kwa sasa ila kila aliyewahi kuwa mwanafunzi wa Profesa Wambali atamkumbuka daima. Mike ameondoka lakini atabakia mioyoni mwetu. Kila tutakapoona familia yake ama kuona kuona kazi zake za taaluma, tutaendelea kuonana naye,” alisema.



Waziri Mkuu amewasili mjini Dodoma mchana huu kuhudhuria mkutano wa 11 wa Bunge unaotarajiwa kuanza kesho (Jumanne, Aprili 9, 2013).     Mimi alinifundisha somo la "EVIDENCE"  pale  Mlimani  mwaka  1996/97 (mwenye blogu)

Thursday, April 18, 2013

ON MARGARET THATCHER'S [FORMER UK CONSERVATIVE PARTY PRIME MINISTER] PASSING

On Margaret Thatcher’s Passing


by John Andrews / April 10th, 2013

I’m just a tiny, tiny bit sad today.

So, Thatcher’s dead. I live in the town where she was born and raised. There are inevitably some who are in deep mourning today, and a few little bunches of flowers have appeared outside the corner shop that was her first family home. On the other hand, there’s also quite a bit of celebrating, and I was speaking to a woman today who said she just hopes that Cameron and Osborne and all the rest of them do the decent thing and jump onto her funeral pyre. Given the fact that her home town, once well-known for its heavy industry, is now largely silent because of Thatcher’s policies, you can see her point.

For myself, I must confess that a very tiny part of me is sad. Whilst she still breathed there was a miniscule theoretical possibility that she could be held to account for the vast crimes against humanity, in general, and the British people, in particular, that were committed by her government. I’m truly sad that even that miniscule theoretical possibility has been permanently snuffed out.

Three years into her reign a poll published in the Times revealed that she was the most unpopular British prime minister in history. And then things got worse.

She began by causing the deaths of a thousand people over a clump of wind-blown rocks 8,000 miles away from Britain, supposedly to defend the right of 2,000 people to call themselves British. It would have been cheaper for this supposed champion of democracy and devotee of Chicago-school economics to pay for those people to move lock, stock and barrel to the UK, accommodate them and give them all Income Support for the rest of their lives, than to wage a war and support a military garrison on the Malvinas to the end of time. But that little fact is always conveniently overlooked.

Thatcher’s foreign policies had one striking feature in common: her government’s support of murderous dictatorships was total; and the line-up of tyrants who enjoyed the backing of her government is quite impressive. There was Pol Pot, for example, and the unspeakable Suharto in Indonesia. Everyone knows about the blood-soaked Pinochet whose evasion from justice was actively assisted by Thatcher’s government. Less well known about are the assortment of Middle-Eastern despots her government aided; but the daddy of them all, the most ruthless oppressor on the face of the Earth, the US government, was always Thatcher’s favourite; and she made significant contributions to its goal of world domination. It’s impossible to know how many tens, if not hundreds of thousands of unnecessary deaths were aided and abetted by Thatcher’s government.

Impressive though her foreign policies obviously were, they pale to insignificance compared with the treacherous actions of her government against the British people. Her mission from the outset was to kill-off the trade union movement which, for all its imperfections, was the only real champion the ordinary Briton had. Once that was done it was game over, lambs fattened and ready for slaughter. She proceeded to kill-off the main source of Britain’s wealth, our manufacturing base; and then rapidly sold off every bit of family silver she could get her hands on. In quick succession Britain’s essential publicly owned utilities were flogged at fire-sale prices: transport, water, electricity, communications, gas… all went under the hammer. Millions of jobs were trashed or scrapped altogether, and then she turned her attention to the last remaining protection the British people had: public services. Why did she do all this? Just so a tiny, tiny handful of obscenely wealthy people could become even more obscenely wealthy.

What a great legacy. You can see why people want to put up statues to her.

The economic wasteland that Britain is today is not all Thatcher’s fault: others followed her who could have put things right, but didn’t. Nevertheless, it was Thatcher who started the ball rolling.

There was never any real chance that Thatcher would have to account for her crimes, but I am truly sad that the miniscule theoretical possibility that she could have been brought to justice is now gone forever.

Tuesday, April 16, 2013

HAKIELIMU's (NGO) VIEWS ON THE 2013/2014 TANZANIAN BUDGET !!!


Imetundikwa hapa leo hii tarehe  16/4/2013.

TAMKO LA HAKIELIMU KUHUSU

BAJETI YA SEKTA YA ELIMU MWAKA WA FEDHA 2013/2014

 
UTANGULIZI

Yanayotokea sasa katika sekta ya elimu yanaleta aibu kusimulia na yanaumiza kutafakari. Uwezo duni wa vijana wanaohitimu shule za msingi na sekondari, wanafunzi kufaulu bila kujua kusoma na kuandika, kuporomoka kwa ufaulu na kuongezeka kwa kiwango cha kutojua kusoma na kuandika ; haya ni baadhi tu ya mambo ambayo yanapaswa sasa kutufumbua macho na kutufanya tutambue ukweli kuwa tunapoteza mwelekeo na kama hatua za makusudi za kunusuru elimu zisipochukuliwa, basi tujue tunajenga taifa la watanzania wasio na ujuzi na maarifa ya kutatua changamoto za kiuchumi, kisiasa na kijamii zinazoendelea kutukabili.

Hali hii imeshaanza kuathiri upatikanaji wa maendeleo ya mtu binafsi, familia na hata taifa kwa ujumla. Tumepuuza kwa muda mrefu hali ya kushuka kwa ubora wa elimu, leo hii tunashuhudia matunda yake na kama tutaendelea “kufunika kombe mwanaharamu apite” tutajifariji na uwepo wa wanafunzi shuleni lakini wasio jifunza kikamilifu wala kuelimika ipasavyo, hatimaye kuwa na taifa mbumbumbu ambalo litashindwa kujiongoza.

Matokeo ya mtihani wa kitaifa wa kidato cha nne mwaka 2012 yanaakisi kiwango cha juu cha kudorora kwa elimu nchini na matokeo ya kuipuuza elimu. Tumeshuhudia watahiniwa 240,903 sawa na asilimia 60.6 wakipata daraja SIFURI katika matokeo hayo; 103,327 sawa na asilimia 26.02 wakipata daraja la nne huku wanafunzi 23,520 tu, ambao ni sawa na asilimia 5.16 (waliopata kati ya daraja la kwanza, la pili na la tatu) ndiyo wakihesabiwa kufaulu vizuri.

Matokeo ya mtihani wa kitaifa wa darasa la saba mwaka 2012 hali kadhalika, sehemu kubwa ya waliochaguliwa (zaidi ya wanafunzi 294,833) wamepata ufaulu wa daraja “D”. Aidha, zaidi ya watahiniwa 139,923 sawa na asilimia 35.45 ya waliofanya mtihani wa kitaifa wa kidato cha pili 2012, hawakufaulu. Kiwango cha kutojua kusoma na kuandika kinazidi kuongezeka na sasa kimefikia asilimia 30 tofauti na ilivyokuwa miaka ya 1980 ambapo ilikuwa asilimia 9 tu. Wanafunzi wengi wanamaliza darasa la saba hawajui kusoma na kuandika.

Takwimu za elimu hadi mwaka 2012 zinaonesha hali ya mazingira ya kujifunzia katika shule zetu kuanzia elimu ya awali mpaka sekondari kutokuwa ya kuvutia. Uwiano wa mwalimu mwenye sifa kwa mwanafunzi kwa elimu ya awali umebaki kuwa 1:124 badala ya 1:25; uwiano wa matundu ya vyoo kwa wanafunzi msingi unakadiriwa kuwa 1:56 badala ya 1:25 kwa wavulana na 1:55 badala ya 1:20 kwa wasichana. Mrundikano wa wanafunzi darasani ni mkubwa mno, wastani kwa nchi nzima ni 1:70 badala ya 1:40, uhaba wa madawati unafikia asilimia 49.1 kwa sasa ikiwa ni upungufu wa takribani madawati 1,879,806 kati ya 3,893,338 yanayohitajika.
Shule za sekondari pia zinaathiriwa na changamoto za namna hii ikiwa ni pamoja na tatizo la uhaba wa mabweni, maabara, vitabu na walimu wa masomo ya sayansi. Pia hamasa ya mioyo ya walimu kujitolea na kuridhika na ualimu iko chini sana(HakE, 2011). Changamoto hizi zinatupa ishara kuwa shule zetu za umma (msingi na sekondari) si shule ambazo zina viwango vya kuridhisha na hata kumsaidia mwanafunzi afundishwe na ajifunze ipasavyo.

Siyo siri kuwa changamoto hizi zina uhusiano wa moja kwa moja na upangaji wa vipaumbele vyetu na maamuzi ya matumizi ya rasilimali za taifa. Ikiwa tunataka kutoka hapa tulipo kwenda mahali bora zaidi ni lazima upangaji wa bajeti katika sekta ya elimu uangaliwe kwa makini sana kwa kuwashirikisha wadau wote wa sekta ya elimu ili kutatua changamoto za sekta ya elimu. HakiElimu inaishauri serikali sasa kuacha visingizio vya uhaba wa bajeti na wahisani kukwamisha utekelezaji wa mipango ya kuikwamua elimu. Kwa kutambua mchango wa ushiriki wa wadau na HakiElimu tukiwa wadau tunaosononeshwa na hali mbaya ya elimu inayoendela kwa sasa, yafuatayo ni maoni au mapendekezo ya HakiElimu katika upangaji wa bajeti ijayo ya sekta ya elimu 2013/2014. Na haya tungependa yatiliwe mkazo sana;-
TATIZO LA WANAFUNZI KUTOJUA KUSOMA NA KUANDIKA

Hili bado ni tatizo kubwa na hadi sasa serikali haijawa na mkakati maalumu wa kuondoa tatizo hili. Shule za msingi kwa madarasa yote bado zina wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika. Hali hii imejitokeza pia katika baadhi ya shule za sekondari licha ya serikali kudai itawabaini na kuwaondoa. Tatizo hili lazima lianze kufanyiwa kazi kwa kuwa na mpango maalumu wa kutathmini idadi kamili ya wanafunzi hao na kupanga mkakati wa makusudi wa kutokomeza tatizo la kuwa na wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika sekondari. Mpango huu lazima uwashirikishe wadau wote wa sekta ya elimu hasa wazazi na kamati za shule ili watambue majukumu yao katika kuondoa tatizo hili.

Kwa kuwa elimu ya awali ni msingi wa mwanafunzi katika kujifunza kusoma na kuandika, tunataka kuona bajeti hii inatia mkazo katika uwekezaji katika elimu ya awali hasa kuwa na walimu bora na vifaa vya kujifunzia na kufundishia. Uwekezaji katika elimu ya awali utachangia sana kupunguza tatizo sugu la kuwa na wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika katika shule za msingi. Tunatambua kuwa katika Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM III), Serikali imeazimia kuanzisha fungu maalumu katika bajeti ya elimu (separate budget line) kwa ajili ya elimu ya awali na kutenga asilimia 20 ya matumizi yake ya kawaida kwa ajili ya sekta ya elimu huku asilimia 60 ya fedha zitakazotengwa kwa ajili ya sekta kuelekezwa katika elimu ya awali na msingi. HakiElimu ingependa kuona mpango huu ukianza kutekelezwa kikamilifu katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha 2013/14.

UHABA WA FEDHA NA WATAALAMU IDARA YA UKAGUZI WA SHULE

Ripoti ya tathmini ya Mpango wa pili wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM II) inaonesha kutofikiwa kwa malengo ya ukaguzi wa shule hivyo kuziacha shule nyingi bila kukaguliwa. Sababu kubwa ya kutofikiwa kwa malengo ya ukaguzi ni uhaba wa fedha unaosababisha uhaba wa vitendea kazi na wataalamu wa ukaguzi. Mwaka 2011/12 shule za msingi zilizokaguliwa ni 3,061 tu kati ya 7,200 zilizopangwa kukaguliwa (sawa na asilimia 42.5). Aidha, sekondari 935 (43.3%) zilikaguliwa kati ya 2,100 zilizopangwa kukaguliwa. Hii ni kusema ni asilimia 19.1 pekee kati ya shule za msingi nchini hukaguliwa na asilimia 21.4 tu ya sekondari hukaguliwa kwa mwaka. Tafsiri hapa ni kuwa uwezo wa fungu la ukaguzi katika bajeti ni kukagua asilimia 20 tu ya shule zake zote, asilimia 80 ya shule hazipati fursa ya kukaguliwa kutokana na uhaba wa bajeti.

Athari za shule kutokaguliwa ni nyingi, kwa mfano utendaji wa walimu kutopimwa, utekelezaji wa mitaala, maendeleo ya shule na wanafunzi kutopimwa. Kama ukaguzi haufanyiki kwa nini tunashangaa wanafunzi kufeli au kumaliza elimu ya msingi na kufaulu mitihani ilihali hawajui kusoma na kuandika? HakiElimu inatoa rai katika bajeti ya 2013/14 kutoa kipaumbele katika kuimarisha ukaguzi wa shule. Serikali itenge fungu la kutosha kwa ajili ya ukaguzi, tumeona athari ya shule kutokaguliwa katika matokeo mabaya ya wahitimu wa darasa la saba, kidato cha pili na cha nne 2012 na tusingependa kuona haya yakijirudia.

SERA YA ELIMU NA MAFUNZO NA SERA YA ELIMU YA AWALI

Serikali imeendelea kupanga bajeti zake kwa kuzingatia “Sera ya Elimu na Mafunzo iliyopitwa na wakati” (ETP 1995). HakiElimu inajiuliza Mpango wa III wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM III) ambao serikali imeanza kuutekeleza umetokana na sera gani? Pia Mabadiliko ya mtaala wa elimu kutoka kuwa Mtaala unaoangalia maudhui kwenda katika Mtaala unaomjengea mwanafunzi ujuzi ulifanywa kwa kutumia sera gani? Je imetumia sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 1995 au rasimu ya sera mpya ambayo bado haijapitishwa?

Tunahoji sera gani kwa kuwa sera ya 1995 inayopigiwa kelele kutokidhi mahitaji na kupitwa na wakati haijapatiwa mbadala na ni wazi kuwa kuendelea kupanga bajeti kwa kutumia sera iliyopitwa na wakati kunaweza kusitupe matokeo mazuri yanayokusudiwa katika elimu kama ambavyo tumeshuhudia katika matokeo ya kidato cha nne 2012. Wakati umefika sasa waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi aje na majibu juu ya lini sera hii itakuwa tayari na itaanza kutumika ili kutoa dira katika mipango na utelekelezaji wake ikiwemo bajeti.

UHABA WA FEDHA ZA RUZUKU SHULENI

Ili kuinua ubora wa elimu, serikali iliazimia kutoa ruzuku kwa kila mwanafunzi kupitia MMEM na MMES Shilingi 10,000 kwa kila mwanafunzi wa shule ya msingi na 20,000 kwa mwanafunzi wa sekondari kila mwaka. Hata hivyo, takwimu za elimu 2012 zinaonesha wastani wa sh. 6,025 tu ndizo hufika shuleni badala ya 10,000/= kwa shule za msingi na wastani wa shilingi 14,178/= pekee badala ya shilingi 20,000/= zilizoahidiwa kwa kila mwanafunzi wa Sekondari.
Hali hii imekwamisha shughuli nyingi za maendeleo ya wanafunzi shuleni, vitabu havinunuliwi kwa wakati, nyenzo za kufundishia na fedha za uendeshaji wa shule hazitoshi. HakiElimu inaishauri serikali kutenga kiwango kamili cha 10,000/= na 20,000/= kama mipango inavyoonesha. Na tena ni muhimu upangaji uzingatie mfumuko wa bei ambao umekuwa ukiathiri pia uwezo wa shilingi katika kufanya manunuzi, itakumbukwa kuwa upangaji wa kiwango hiki cha ruzuku ulifanyika 2002-2006 wakati mfumuko wa bei ukiwa katika wastani wa 4.4% wakati leo wastani wa mfumuko wa bei ni asilimia 14.9% , hii ni mara tatu zaidi ya kiwango cha awali.

UPANGAJI NA USIMAMIZI WA FEDHA ZA UMMA

Serikali imekuwa ikitoa ahadi juu ya kupunguza bajeti ya matumizi ya kawaida kwa muda sasa, (Hotuba ya Waziri wa Fedha Juni 9, 2011). Hata hivyo bado Wizara ya Elimu imeendelea kutenga fedha nyingi katika matumizi ya kawaida huku eneo la “matumizi mengineyo” likiendelea kutengewa fedha nyingi zaidi. Takwimu zinaonesha bajeti ya matumizi ya kawaida ya wizara imeongezeka kutoka bilioni 523.8 mwaka 2011/12 hadi bilioni 631.9 mwaka 2012/13, sawa na ongezeko la asilimia 20; wakati fedha za matumizi mengineyo (posho, mafuta, safari, samani na ukarimu) ikiongezeka kutoka bilioni 207 mwaka 2011/12 hadi bilioni 386 mwaka 2012/13 sawa na ongezeko la asilimia 86. Hii ina maanisha bado agizo na ahadi ya kupunguza matumizi yasiyo ya lazima halizingatiwi katika bajeti zetu.

Pia utekelezaji wa bajeti ya sekta ya elimu umekuwa si mzuri. Licha ya serikali kudai haina fedha za kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya elimu, bado kumekuwa na usimamizi mbaya wa hata zile fedha kidogo zinazopangwa. Ripoti ya Mkaguzi wa Hesabu za Serikali ya mwaka 2010/2011 imebainisha fedha zilizotolewa kwa miradi ya MMEM na MMES kushindwa kutumiwa na Halmashauri katika kutekeleza miradi hiyo. Hata fedha zinazotolewa kwa ajili ya mfuko wa jimbo ambazo zingesaidia kuboresha shule zetu nazo hazitumiki.

Rai yetu ni kuwa bajeti hii ya mwaka wa fedha 2013/14 iachane na matumizi ya kawaida yasiyokuwa ya lazima, badala yake fedha hizo zitumike kutatua changamoto muhimu kama vile urekebishaji wa maslahi ya walimu kama mishahara, posho za mazingira magumu, nyumba katika maeneo yasiyokuwa na nyumba za kupanga na kuboresha mazingira yao ya kufundishia shuleni. Hatua hii itasaidia kurudisha morali wa ufundishaji na kupunguza matatizo ya ufaulu nchini. Upangaji wa fedha na matumizi yake katika elimu kamwe hauwezi kuwa na mafanikio iwapo kutaendelea kuwepo kwa kutoelewana kati ya walimu na serikali. Mwalimu ni mtekelezaji mkuu wa bajeti na mipango shuleni, hivyo hakuna budi kukawa na maelewano kati ya wadau hawa muhimu ili utekelezaji wa mipango uwe na ufanisi na uwekezaji ulete tija.

Pia, tufike mahala sasa tupange bajeti kwa kuwa na vipaumbele vichache ili tuvitekeleze. Ni dhahiri kuwa, Serikali haiwezi kutatua matatizo yote kwa wakati mmoja, hivyo lazima tujenge utamaduni wa kuwa na kipaumbele au vipaumbele vichache katika bajeti kwa kila mwaka wa fedha ili kutatua changamoto za sekta ya elimu. Bajeti hii lazima ieleze bayana mikakati ya Wizara ya kuboresha usimamizi na ufanisi wa fedha za umma hasa katika kuhakikisha fedha zinafika kwa walengwa kwa wakati, zinatumika kama zilivyopangwa na zinatumika ipasavyo kwa mantiki ya kuleta ufanisi wa fedha.

Elizabeth Missokia

Mkurugenzi Mtendaji
HakiElimu

Sunday, April 14, 2013

FAIDA ZA MTI WA MLONGE [MORINGA]

 Imedakwa toka mitandaoni, leo hii 14 Aprili, 2013.

 FAIDA  ZA  MTI  WA  MLONGE  [MORINGA]

KAMA kuna mti wenye faida nyingi za kiafya, basi Mlonge unaweza kuwa unaongoza. Kila eneo la mti huu, kuanzia majani, maua, mbegu, magamba  hadi mizizi yake ina virutubisho vya kipekee vyenye faida nyingi za kiafya kwa binadamu.

Majani ya Mlonge yanaweza kutafunwa mabichi, yaliyochemshwa kama mboga au yaliyokaushwa na kusagwa kuwa unga. Unga wake unaweza kuhifadhiwa kwa miezi kadhaa bila kupoteza ubora na faida zake za kiafya.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na shirika moja lijulikanalo kama Trees For Life, majani ya Mlonge yana Vitamin A nyingi kuliko karoti, vitamin C nyingi kuliko machungwa na madini ya Potassium nyingi kuliko ndizi mbivu, halikadhalika ubora wa protini yake ni bora kushinda maziwa na mayai.

Kutokana na kuwa na kiasi kingi cha madini ya chuma  (Iron), kasiamu (Calcium) na vitamin nyingi za aina mbalimbali, majani ya mmea huu yamekuwa yakitumika kama ‘tonic’ kwa watoto wadogo na vijana ili kuimarisha mifupa na kusafisha mfumo wa damu mwilini.

Ili kutengeneza ‘tonic’, saga majani mabichi ya Mlonge pamoja na maji, yachuje kisha changanya na maziwa halisi. Inaelezwa kuwa juisi ya aina hii ni dawa nzuri kwa waja wazito, kwani huboresha njia ya uzazi na kumuwezesha mama kuzaa bila matatizo na kuondoa matatizo baada ya kujifungua.

Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali, mti wa Mlonge unatibu karibu magonjwa 300 ya aina mbalimbali, yakiwemo yale magonjwa sugu, baadhi yake ni kama haya yafuatayo:

Mlonge unaweza kutibu Pumu, Kikohozi na Kifua Kikuu. Aidha, magonjwa mengine kama Kisukari, Shinikizo la damu (la juu na chini), magonjwa ya ngozi, magonjwa ya kwenye njia ya mkojo (UTI) kuongeza kinga ya mwili (CD4) na kuongeza nguvu za kiume.

Saturday, March 30, 2013

MAONI YA C U F KWA TUME YA KATIBA TANZANIA

IMETUNDIKWA HAPA LEO HII  30  Machi, 2013. 


 THE CIVIC UNITED FRONT
(CUF - Chama Cha Wananchi)

 MAONI YA THE CIVIC UNITED FRONT (CUF- CHAMA CHA WANANCHI) KWA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA-  07 JANUARI,  2013

 UTANGULIZI;

Kwa niaba ya The Civic United Fronf (CUF-Chama Cha wananchi), na kwa niaba
 yangu binafsi napenda kuchukua fursa hii kukushukuru wewe Mwenyekiti wa
 Tume ya Mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na
  wajumbe  wako kwa kutualika rasmi Chama Cha CUF mbele ya Tume yako kutusikiliza na
 kupata maoni ya chama chetu juu ya mchakato huu muhimu kwa mustakbali mwema
 wa Taifa letu la Tanzania pamoja na watu wake.

 Aidha, tunampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Jakaya  Mrisho Kikwete kwa kuanzisha mchakato huu wa mapitio makubwa na kukusanya
 maoni ya katiba ya nchi yetu ili ikidhi matakwa ya wakati wa sasa na
 kutupeleka mbele zaidi kwa ustawi wa Taifa letu na watu wake. Madai haya ya
 kuandaa mchakato wa kuwa na katiba mpya inayokidhi matakwa ya wakati
 tulionao ni madai ya msingi ambayo chama chetu cha CUF kimekuwa
 kikiyasisitiza tangu kurejeshwa tena kwa mfumo wa demokrasia ya vyama vingi
 vya siasa nchini mwaka 1992 na mara zote kuainisha suala hili katika
 manifesto zake za uchaguzi.

 Kutokana na muongozo wa Tume ya Mabadiliko ya katiba maoni yetu yamejikita
 katika maeneo yafuatayo:

(i)     Misingi na Maadili ya Kitaifa, Madaraka ya
(ii)    Wananchi, Muundo wa Nchi na Taifa ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
(iii)    Haki za Binadamu na Wajibu wa Wananchi,
(iv)    Ardhi, Maliasili na Mazingira
 (v)    Mihimili ya Nchi (Ardhi, Watu na Utawala),
(vi)    Mihimili ya Utawala (Serikali,
(vii)    Bunge na Mahakama),
(viii)   Muundo na Mamlaka ya Serikali za Mitaa, na
(ix)    Vyombo vya Ulinzi na Usalama.

 Kwa muhtasari maudhui haya Chama Cha Wananchi CUF kinapendekeza yafuatayo
 katika mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya Mwaka 1977;

 1. Muundo wa serikali tatu za muungano; yaani serikali ya Zanzibar, serikali
 ya Tanganyika na Serikali ya Mungano.

2. Uanzishwaji wa Tume huru za uchaguzi mapema iwezekanavyo. Kwa kuwa Tume
 ya uchaguzi inapaswa kuanza kazi zake mapema ili kufanikisha uchaguzi wa
 mwaka 2014/15, Tume haiwezi kusubiri mabadiliko ya katiba yakamilike ndio
 ianze kazi zake kwa Muundo mpya utakaopendekezwa.

3. Katiba yenye misingi ya mfumo wa uwajibikaji kwa watendaji wote wa umma
 na uainishwaji wa wazi wa Dira ya Taifa.

 4. Katiba itakayotoa haki kwa wagombea binafsi kushiriki katika uchaguzi.

5. Katiba itakayotoa uhuru wa vyama vya siasa kuungana muda wowote
 vitakapoona inafaa bila kupoteza usajili wa kawaida wa vyama hivyo.

6. Katiba itakayoweka muundo wa kuwa na Rais mtendaji "Executive President"
mwenye madaraka yanayopimika na kukubalika yasiyobana wala kuingilia au
 kuondoa uhuru wa utendaji kazi wa mihimili mingine ya dola. Rais achaguliwe
 kwa kupata asilimia 50+1 au zaidi ya kura zilizopigwa.

 7. Katiba yenye kuweka mfumo sahihi wa kulinda rasilimali za Taifa na
 kuhakikisha zinawanufaisha Watanzania wote kwa haki na usawa.

 8. Katiba itakayompa kila Mtanzania kwa nafasi yake kushiriki katika
 maendeleo ya nchi yake kwa kuwa na muundo wa serikali itakayoshirikisha
 kila   Mtanzania mwenye uzalendo wa kweli na uwezo wa kutoa mchango wake kwa ajili
 ya maendeleo na ustawi wa taifa.

 9. Katiba itakayoweka muundo wa uwakilishi wa uwiano (propotional
 representation) ili kila kura itakayopigwa kuwa na thamani tofauti na
 utaratibu wa sasa wa mshindi kuchukua vyote (winner takes all) hata kama ameshinda kwa kura moja.

 10. Katiba itakayo hakikisha uwepo wa mgawanyo wa madaraka kati ya serikali
 kuu na serikali za mitaa kwa kuondoa mfumo wa kuziburuza serikali hizo
 zilizokaribu na wananchi. Wilaya zisianzishwe kiholela. Vigezo vya
 halmashauri ya wilaya, miji, manispaa na majiji vitawekwa na sheria.
 Utawala wa mikoa uondolewe.

 11. Katiba itakayoweka msingi wa kuzuia ufisadi mkubwa wa rasilimali za
 nchi  hasa kwa njia ya uingiaji wa mikataba, Bunge likiwa ni chombo cha
 uwakilishi  wa wananchi lazima lishirikishwe.

 12. Katiba itakayoweka Muundo wa Tume huru za Taifa za uchaguzi tangu ngazi
ya uteuzi wake kuanzia ngazi ya Taifa hadi ngazi ya chini. Katiba
 itakayoto fursa matokeo ya uchaguzi kwa ngazi zote kuhojiwa mahakamani ikiwemo
  matoke ya uchaguzi wa Rais.

13. Katiba itakayopambanua mgawanyo wa madaraka na mamlaka ya mihimili yote
 mikuu katika nchi kwa maana ya Bunge, Serikali na Mahakama.

 14. Katiba itakayoeleza wazi kuhusu haki na wajibu wa dola kuhakikisha
 elimu ya watoto wetu, matumizi ya rasilimali za taifa, huduma za msingi za afya,
 ulinzi wa nchi yetu na sera za ardhi na kilimo zinasimamiwa na kutekelezwa
 kwa manufaa ya wananchi wote. Katiba ndiyo yenye nafasi ya kulinda haki hizi
za mwananchi na si huruma ya mtawala atakaye kuwepo kwa wakati huo au chama
 cha siasa. Sera za kitaifa lazima zifuate na kuheshimu haki zilizoainishwa
 ndani ya katiba.

15. Kuhakikisha kwamba wananchi wana madaraka ya kujiamulia wenyewe masuala
 ya maendeleo yao kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.;

16. Katiba yenye kulinda haki za binaadamu, na kupinga aina zote za ubadhilifu, ukandamizaji, ubaguzi wa aina yeyote iwe wa kidini, kikabila, kijinsia au kikanda.

17. Katiba yenye kuweka misingi endelevu ya kulinda amani ya nchi yetu.

 18. Masuala ya Ardhi yawe na sura kamili katika katiba mpya. Ardhi ni mali
 ya Watanzania wote. Mtanzania peke yake ndiye anayeweza kumiliki ardhi moja
 kwa moja.

 19. Katiba inayohakikisha kuwa haki za msingi za makundi maalum, wanawake,
 watoto, wazee wasiojiweza na walemavu zinalindwa kwa kuanishwa ndani ya
katiba.

Chama cha CUF kipo tayari kutoa ushirikiano unaostahiki kwa Tume katika
 kipindi chote cha mchakato huu pamoja na kushirikiana na Watanzania wote
 bila kujali itikadi za kisiasa na tofauti nyinginezo, kuhakikisha kuwa kwa
 pamoja nchi yetu inakuwa na katiba bora yenye kukidhi haja na matakwa ya
 hali ya kisiasa, kiuchumi na ustawi mwema wa jamii ya Watanzania.
 Ni matarajio ya Chama Cha Wananchi CUF kuwa maoni haya yatazingatiwa na
 kuingizwa katika rasimu ya mabadiliko ya katiba kwa mjadala na hatimaye
 kufanyiwa maamuzi yanayofaa kwa mustakbali mwema wa Taifa letu la Tanzania.

 Mungu Ibariki Tanzania na watu wake.

 HAKI SAWA KWA WOTE

 Prof Ibrahim Haruna Lipumba,
 Mwenyekiti wa CUF Taifa

 Contact;
 P.O.Box 10979
 Dar es salaam, Tanzania.
 lipumba@yahoo.com

Tuesday, March 26, 2013

SHEIKH BILAL REHANI WAIKELA ATINGA MAHAKAMANI KISUTU, DAR ES SALAAM, TANZANIA.


Imetundikwa hapa leo hii tarehe 26/3/2013.

Kutoka:  tz_muslim_community@yahoogroups.com, 25/3/2013.

Asalaam aleikum warahmatullah wa barakatuh,


Haya ndio yaliyojiri mahakama ya Kisutu pale Sheikh Bilal Rehani Waikela ambae alipanda kizimbani kutoa ushahidi wake upande wa washtakiwa.

Sheikh Waikela alikuja kutoka Tabora.

Hakika mahakama jana walisikia ambayo si wengi wamepata kuyasikia katika maisha yao yote.

Sheikh Waikela ameanza kwa kutaja umri wake wa miaka 87 na akaieleza mahakama kuwa ameanza kuutumikia Uislam mwaka 1940 akiwa katika Anjuman Muslim na ilipokuja East African Muslim Society ( EAMWS) akawa kiongozi.

Akaeleza pia yeye ni muasisi wa Mabaraza ya Misikiti Duniani makao makuu yake Makka.

Akasema yeye Tabora ni mtu wa tatu kujiunga na TANU na katika Tanganyika ni mtu wa 264.

Sheikh Waikela akaeleza kuwa yeye alikuwa bega kwa bega na Nyerere katika kuipigania uhuru wa Tanganyika na akimchukua Nyerere ndani ya gari yake Tabora na wakila chakula nyumbani kwake.

Waikela aliichekesha mahakama aliposema wakati ule alikuwa kijana ana fedha na akicheza tennis.

Akaeleza kuwa Gavana Edward Twinning aliingiza fitna nchini kuhusu Waislam kutaka kuwachonganisha na Wakristo katika suala la elimu ili avunje juhudi za TANU kudai uhuru.

Nyerere alimsihi Waikela kuwa katika hutuba zake ajitahidi sana kuliweka suala hilo vyema ili pasiingie mtafaruku na nchi ikawa kama India na Pakistani Waislam na Wahindu wakagawana nchi katika misingi ya dini.

Waikela akasema hilo walilifanyia kazi na hali ikabaki shwari hadi uhuru ukapatikana.

Matatizo yakaja baada ya uhuru kupatikana.

Waikela akaieleza Mahakama jinsi Sheikh Hassan bin Amir alivyomtahadharisha kuhusu njama zilizokuwa zinapikwa serikali dhidi ya EAMWS na akamweleza kuwa wanafiki ndiyo wanaotumiwa.

Sheikh Waikela aliwataja Mahakamani wanafiki hao kwa majina mmoja baada ya mwingine.

Akaeleza mkutano wa EAMWS katika Ukumbi wa Aga Khan Girls mwaka 1963 alipomsomea Nyerere risala ya Waislam kuhusu fitna iliyokuwa ikienezwa nchini dhidi ya Waislam na Uislam.

(Risala hii kwa sasa ni maarufu inajulikana kama ''Moto wa Waislam Ukiwaka.'')

Anasema hotuba hii ndiyo iliyosabaisha yeye kuwekwa kizuizini mwaka uliofuatia 1964 na alipotoka jela alipewa hati ya kifungo ambayo Sheikh Waikela aliieleza Mahakama kuwa ameitundika nyumbani kwake ukutani kama pambo.

Mahakama ilifahamishwa kuwa mmoja wa washitakiwa ni binti yake aitwae Dentation Waikela ambae alizaliwa baba yake ikiwa jela.

Sheikh Waikela akaeleza jinsi Nyerere alivyowawezesha kundi la Adam Nasib kwa fedha na ushirikiano wa serikali kupita majimboni kuwashawishi Waislam kujitoa EAMWS lakini hawakufanikiwa.

Katika majimbo 20 ni majimbo 8 tu ndiyo yaliyokubali kujitoa.

Hata hivyo serikali ilikatumia nguvu na kuitisha mkutano wa wanasiasa Waislam Iringa na Bakwata ikaanzishwa na serikali ikaweka askari wenye silaha katika ofisi zote za EAMWS na kuzifunga na makufuli na minyororo.

Binafsi Sheikh Waikela akaeleza Mahakama kuwa alihongwa shs: 40, 000 na Geoffrey Sawaya aliyekuwa Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai, hongo ambayo aliikataa.

Hao waliokubali hongo ile ndiyo walioshirikiana na serikali katika kuiweka BAKWATA madarakani.

Kuhusu kiwanja cha Markaz Chang'ombe anasema kile kiwanja ni mali ya EAMWS na madhumuni yake ilikuwa ni kujenga Chuo Kikuu.

Kwa hakika alisema mengi na mwisho alimuomba hakimu awape Waislam haki yao



Tuesday, March 19, 2013

HOW GRANDCHILDREN PERCEIVE THEIR GRANDPARENTS !!!!

Posted here on 19/3/2013.

How children perceive their Grandparents……



1. She was in the bathroom, putting on her makeup, under the watchful eyes of her young granddaughter, as she’d done many times before. After she applied her lipstick and started to leave, the little one said, “But Grandma, you forgot to kiss the toilet paper good-bye!” I will probably never put lipstick on again without thinking about kissing the toilet paper good-bye….

2. My young grandson called the other day to wish me Happy Birthday. He asked me how old I was, and I told him, 80. My grandson was quiet for a moment, and then he asked, “Did you start at 1?”

3. A grandmother was telling her little granddaughter what her own childhood was like. “We used to skate outside on a pond. I had a swing made from a tire; it hung from a tree in our front yard. We rode our pony. We picked wild raspberries in the woods.”

The little girl was wide-eyed, taking this all in. At last she said, “I sure wish I’d gotten to know you sooner!”

4. When my grandson Billy and I entered our vacation cabin, we kept the lights off until we were inside to keep from attracting pesky insects. Still, a few fireflies followed us in. Noticing them before I did, Billy whispered, “It’s no use Grandpa. Now the mosquitoes are coming after us with flashlights.”

5. A second grader came home from school and said to her grandmother, “Grandma, guess what? We learned how to make babies today.” The grandmother, more than a little surprised, tried to keep her cool. “That’s interesting.” she said… “How do you make babies?”

“It’s simple,” replied the girl. “You just change ‘y’ to ‘i’ and add ‘es’.”

6. Children’s Logic: “Give me a sentence about a public servant,” said a teacher. The small boy wrote: “The fireman came down the ladder pregnant.” The teacher took the lad aside to correct him. “Don’t you know what pregnant means?” she asked.

“Sure,” said the young boy confidently. ‘It means carrying a child.”

7. A grandfather was delivering his grandchildren to their home one day when a fire truck zoomed past. Sitting in the front seat of the fire truck was a Dalmatian dog. The children started discussing the dog’s duties.

“They use him to keep crowds back,” said one child.

“No,” said another. “He’s just for good luck..”

A third child brought the argument to a close. “They use the dogs,” she said firmly, “to find the fire hydrants.”

8. A 6-year-old was asked where his grandma lived. “Oh,” he said, “she lives at the airport, and when we want her, we just go get her. Then, when we’re done having her visit, we take her back to the airport.”

9. Grandpa is the smartest man on earth! He teaches me good things, but I don’t get to see him enough to get as smart as him!

10. After putting her grandchildren to bed, a grandmother changed into old slacks and a droopy blouse, took her teeth out and proceeded to wash her hair. As she heard the children getting more and more rambunctious, her patience grew thin. Finally, she threw a towel around her head and stormed into their room, putting them back to bed with stern warnings. As she left the room, she heard the three-year-old say with a trembling voice,

“Who was THAT?”