Saturday, March 13, 2010

WONDER TWINS HEAD FOR HIGH SCHOOL AT AGE NINE

Wonder Twins Head For High School Aged Nine

Monday, March 1 09:37 am
SkyNews © Sky News 2010

Wonder Twins Head For High School Aged Nine
From SKYNEWS, 1 March, 2010.

WHAT IS EVEN MORE AMAZING, THESE CHILDREN ARE OF AFRICAN DESCENT AND ARE LIVING IN A CHALLENGING AND DIFFICULT ENVIRONMENT.


Paula and Peter Imafidon, from Waltham Forest, London, amazed parents and teachers when they passed an A-level maths exam at the age of seven.

The twins have been waiting to find out which secondary school they will attend, along with thousands of other youngsters - who are two years older - across the country.

Peter and Paula, who attend a state primary in London, were helped by their three older brothers and sisters, all of whom were also child prodigies.

Their father Chris said he was thrilled by his childen's achievements at school.

He denied any particular genius in the family, crediting their success to the Excellence in Education programme for inner city children from disadvantaged backgrounds.

"Every child is a genius," he said. "Once you identify the talent of a child and put them in the environment that will nurture that talent then the sky is the limit.

"Look at Tiger Woods, or the Williams sisters - they were nurtured.

"You can never rule anything out with them, the competition between the two of them makes them excel in anything they do.

"They are forever competing and fighting, even if it's just for the remote control or the computer."

Paula hopes to become a maths teacher, while Peter hopes to become Prime Minister one day.

Thursday, March 11, 2010

HABARI YA MAENDELEO YANGU KATIKA MASOMO YA UZAMIVU

Kwa kweli kila jambo hupangwa na Mungu.

1. Mimi nilijizatiti kutoa Andiko langu la kitaaluma la ["STARTING A LEGAL AID CLINIC AT MZUMBE UNIVERSIT (MULAC)]tarehe 9 Machi, 2010 kama nilivyotarajia mapema katika mkutano uliofanyika siku hiyo. Hata hivyo wajumbe wa Mkutano wa Faculty of Law Internal Examiners Board walikataa, kutokana na sababu kwamba Andiko hilo halijatolewa na kujadiliwa katika Idara ya Sheria za Utawala (Administrative Law Department) . Hivyo ikaamuliwa kwamba Andiko hilo likatolewe kwanza katika Mkutano wa Idara ya Sheria za Utawala (Department of Administrative Law).

2. Nilipomuona Mkuu wangu wa Idara Bw. Ignas Sethi Punge, na kumfahamisha jambo hilo mahsusi (alichelewa kufika kikaoni)akasema, itabidi jambo hili lipangiwe siku yoyote baada ya mkutano wa Bodi ya Kitivo cha Sheria tarehe 12/3/2010. Hivyo nimebaki nikisubiri kikao hicho kifanyike ili nikakumbushie tena Idarani kwangu kujua kama kikao cha kujadili Dondoo ya Andiko langu kitafanyika lini.

3. Tatizo ni kuwa pamebakia muda wa siku 10 tu kutoka siku ya Mkutano huo na kufunguliwa Chuo tarehe 22/3/2010. Kwa uzoefu tulionao, Chuo kikifunguliwa, inakuwa vigumu sana kuwapata walimu wa Idara wa kuhudhuria katika mikutano kwa kuwa idadi yao kubwa wanakuwa katika ratiba za kufundisha, hivyo kupanga mkutano wakati huo Kiidara inakuwa ni Mtihani mkubwa. Ndio maana naomba Mungu iwezekane mkutano huo ufanyike ndani ya siku hizo kumi(10) zitakazobaki baada ya Mkutano wa Bodi ya Kitivo cha Sheria.

4. Umuhimu wa Andiko hilo kupita na kufikia katika ngazi ya Bodi ya Kitivo cha Sheria, ngazi ya Seneti na ngazi ya Kanseli ya Chuo ni aina mbili:

(a) Kwanza hatima ya jambo zima hili itajulikana endapo Chuo kitakuwa tayari kuanzisha kituo kama hiki cha Kutoa Msaada wa Sheria kwa Wananchi kwa kutumia wanafunzi wake katika kufanya kazi mbalimbali za kisheria Ki tuoni hapo; jambo ambalo litakuwa ni faida kubwa sana kwa chuo, kwa wanafunzi wetu, kwa majirani na taifa kwa jumla. Pia kitapandisha sana hadhi ya chuo chetu kwamba ndio cha kwanza nchini kufanikiwa kuanzisha kituo kama hiki.

(b) Jambo la pili ambalo ni la kibinafsi zaidi ni kwamba Andiko hilo likishapita kote linakotakiwa kupita kiutaratibu, nimedhamiria kulichapisha Andiko hilo ili linisaidie katika kupandisha Chati yangu ya Kitaaluma Chuoni Mzumbe. Kama mfahamuvyo, katika Vyuo Vikuu vya Taaluma duniani kote kuna ile sera isemayo "EITHER YOU PUBLISH OR YOU PERISH" (Chapisha au Potea). Kwa kuwa sina nia ya kupotea, ni heri nichapishe, inshaallah.

Friday, March 5, 2010

MANUFAA YA MANDONDO (VYAKULA AINA YA MAHARAGE)

Daily Tip for insight into some of Dr. Weil's favorite foods, courtesy of Dr. Weil on Healthy Aging!


They often get a bad rap for causing indigestion and flatulence, but the health benefits of beans (and other legumes, such as lentils and chickpeas) make them a stellar choice in a healthful diet. Beans are:

1. An excellent source of vegetarian protein, providing six to seven grams per ½ cup serving.
2. High in folic acid, which may help to protect against cancers of the lung, colon, and cervix, and prevent birth defects.
3. A great source of fiber, dishing up 25-30% of the Daily Value of dietary fiber, 75% of which is insoluble - the type that reduces the risk of colon cancer.
4. A low-glycemic-index food, making them a good option for diabetics.

In addition, most varieties are inexpensive and versatile. I recommend 1-2 servings of beans and legumes per day - easy to do if you swap out meat for beans in salads and sandwiches, and make hummus or bean dip part of an afternoon snack. And if stomach upset is a concern, you can improve the quality and digestibility of beans by consuming them with grains such as brown rice, which provide a complimentary protein profile. Discarding the soaking and cooking water when using dry beans may also help reduce flatulence.

Thursday, March 4, 2010

HABARI ZA MAENDELEO YANGU KATIKA MASOMO YA UZAMIVU

Imehifadhiwa leo hii tarehe 5 Machi, 2010, nami Zainab M. Mwatawala.

1. Natanguliza Kumshukuru Mungu. Leo nina dhamira ya kuhitimisha taarifa ya malipo ya "Situational Analysis", niliyoyaomba tarehe 17/9/2009 kwa ajili ya kazi niliyoifanya kati ya tarehe 27/9/2009 na tarehe 10/10/2009 (yaani mwaka jana).

2. Hatimaye leo, baada ya "quarter" tatu za kutolewa mafungu ya fedha kupita, yaani ile ya Julai-Septemba, Oktoba-Disemba, na Januari-Machi. Leo ndio nimepokea fedha taslim kwa njia ya Hundi ya CRDB Bank (Mzumbe Branch) Na. 044685 ya tarehe 4 Machi, 2010, iliyolipwa kupitia Vocha Na. 103/3 ya tarehe 3/3/2010, ya Shilingi (Tshs.) 992,500/= (yaani kwa maneno ni: shilingi mia tisa tisini na mbili elfu, mia tano tu) kwa ajili ya kazi hiyo niliyoifanya kwa kutumia raslimali fedha binafsi wakati huo.

3. Pia habari nzuri nyingine ni kuwa HATIMAYE, Andiko langu la kitaaluma juu ya "Starting a Legal Aid Clinic at Mzumbe University", (Uanzishwaji wa Kituo cha Kutoa Msaada wa Sheria Chuo Kikuu Mzumbe - MULAC) ambalo nilisema hapo nyuma kuwa nililihadhirisha kwa hadhira ya Kitaaluma Chuo Kikuu Mzumbe tarehe 1/9/2009, nitalihadhirisha tena rasmi katika ngazi inayofuata ya Mkutano wa "Faculty of Law (FOL) Internal Examiners Board" utakaofanyika siku ya Jumanne, tarehe 9/3/2010 Chuo Kikuu Mzumbe.

4. Baada ya hatua hiyo muhimu katika ngazi ya mambo ya Kitaaluma Chuo Kikuu Mzumbe, Andiko hilo nitalihadhirisha katika Mkutano wa Bodi ya Kitivo cha Sheria (FOL Faculty Board utakaofanyika tarehe 11/3/2010, kabla ya bodi hiyo kuridhia ili lifikishwe katika kikao cha Seneti (senate) utakaofanyika tarehe 19/3/2010, Chuo Kikuu Mzumbe.

5. Mkutano wa Seneti ndio ngazi ya mwisho itakayopendekeza endapo Andiko hilo lipite au la; yaani kikao hicho kina mamlaka ya kulipeleka pendekezo la kuanzisha rasmi Kituo cha Kutoa Msaada wa Sheria Chuo Kikuu Mzumbe (MULAC) kwa Baraza la Chuo (Mzumbe University Council), litakalokutana tarehe 26/3/2010 Chuo Kikuu Mzumbe. Hii ni kwa mujibu wa Kalenda ya Kitaaluma (ALMANAC) Chuo Kikuu Mzumbe ya mwaka 2009/2010.

6. Namuomba Mungu anisaidie ili kusiwe na vipingamizi, vigingi, wala vikwazo vitakavyokwamisha kazi hii kusonga mbele kadri ya ratiba hiyo niliyoielezea.

Wednesday, March 3, 2010

WATANZANIA JINSI TUNAVYOANGAMIZA TAIFA KWA KUTUMIA KUKU

Imechangiwa na Patricia Chenga kupitia email {bwanawangu@yahoo.com}


Kwa mujibu wa matokeo ya uchunguzi wa kitabibu, baadhi ya kuku wa kufugwa wanaoingia sokoni wamekuzwa kwa kutumia ‘utundu’ wenye hatari wa baadhi ya wafugaji wasio waaminifu kwa kulisha mifugo hiyo dawa za ARV ambazo huwafanya kuku hao kuonekana wakubwa na wanene kwa muda mfupi.

Uchunguzi huo unakwenda mbele zaidi na kubainisha kwamba, tabia za dawa hizo ambazo ni kujenga mwili na kuimarisha kinga ya magonjwa kwa mwathirika wa Virusi vya Ukimwi, ndiyo inayompata mlaji wa kuku hao.

Inadaiwa kuwa, kuku hao wanapokula chakula kilichochanganywa na dawa hizo, huweza kutumia siku kumi na mbili hadi kumi na nne kutoka kuwa vifaranga hadi utayari wa kuingizwa kwenye soko la walaji.

Ili kukamilisha uchunguzi huo, Amani lilituma machero wake maeneo ya Kibamba, nje kidogo ya Jiji la Dar ambapo ndipo kwenye viwanda vya kuzalisha kuku wa ‘sampuli’ hiyo.

Kwa mujibu wa kijana mmoja ‘profesheno’ wa kutunza kuku katika moja ya nyumba maarufu kwa uzalishaji maeneo hayo, ambaye hakutaka jina lake lichorwe kwenye ‘pepa’ hii, alikiri kuwepo kwa ishu hiyo, lakini alibainisha kuwa hajui bosi wake anapochukulia vidonge hivyo vya ARV’S.

MADHARA:
Kwa mujibu wa Daktari mmoja wa Hospitali ya Taifa Muhimbi ambaye aliomba hifadhi ya jina lake, mtu anayependa kula kuku waliokuzwa kwa kutumia ARV na yeye huanza kunenepa kupita kawaida, lakini uzito unaweza kuwa tofauti na unene ‘boya’.

Mtabibu huyo aliongeza kuwa, watoto wengi wanaozaliwa siku hizo ambao wazazi wao wamekuwa watumiaji wazuri wa kuku, hukua haraka kiasi kwamba, mtoto wa miaka 18 huonekana kama ana miaka 27.

Aidha, alidai kuwa, wengi ambao kuku hao wamekuwa chakula chao kikuu, hufika mahali wanakuwa ‘legelege’ katika utendaji wa kazi wa kila siku tofauti na zamani huku sehemu kubwa ya chakula hicho ikiangamiza ‘pati’ ya subira na uvumilivu na mlaji kuwa na hasira.

Dalili nyingine ni mtu kuhisi muda wake wa kuchoka unakuwa mfupi akilinganisha na zamani na wakati mwingine hali ya kuhisi kusinzia humtawala hata kama anafanya kazi.

Sunday, February 28, 2010

K U Z E E K A

KUZEEKA - imechangiwa na dr. Wilbert Bunini Manyilizu wa Chuo Kikuu, Mzumbe, Tanzania.

* Kila mmoja anazeeka/ataazeeka

* Kuna tabia za kimwili na kiakili zinazoambatana na mchakato huu usioepukika wa kuzeeka

* Kasi ya kuzeeka hutofautiana kutoka mtu hadi mtu kutokana na sababu mbalimbali za kimaisha, mazingira, tabia, vyakula na kadhalika.


MABADILIKO YA KIMWILI WAKATI WA MKCHAKTO WA KUZEEKA

Tabia za kuzeeka Mwili huonekana mapema zaidi kuliko zile za kisaikolojia.
Uzee huanza lini?
Unapozaliwa tu unaanza kuzeeka. Japo kuzeeka halisi ni pale kukua kunapokoma.
Mchakato wa kuzeeka haraka au taratibu hutegemea mtu binafsi.
Uzee huja kwa kasi tofauti kati ya mtu na mtu na kwa viwango tofauti kati ya kiungo na kiungo katika mtu huyo huyo.
Kwa nini mtu anazeeka?
Nadharia za sayansi za mchakato wa kuzeeka zinaeleza kuwa:

1. Kadiri siku zinavyopita kuna upotevu wa chembe chembe zinazotengeneza mwili hasa mtu anapokuwa ametoka kwenye utoto au ujana na anaposimama kukua. Hii ni hali ya kurithi ambayo kila mtu ameumbwa nayo.

2. Baadhi ya chembe chembe kama vile zile za damu za ngozi, ubongo nakadhalika hazigawanyiki tena ili kuongezeka (yaani hakuna kukua tena).Kukua maana yake ni kuongezeka wingi wa chembe chembe za mwili na ubongo kunakotokana na kugawinyika kwake.

3. Chembe chembe kama za neva za fahamu, misuli nakadhalika zinapopotea kwa kuzeeka na kufa kunakotokana na kushindwa kugawanyika, hupotea milele.

4. Viunganishi ( ni kama jointi za matofali ya nyumba= matofali ni chembe chembe) vya chembe chembe za mwili katika viungo vyote kama vile kwenye ngozi, misuli, ubongo nakadhalika. Tishu hizi ambazo ni viunganishi vya chembe chembe hukakamaa na kupoteza uwezo wake wa asili na kukatika kwa kukomaa, hivyo kubakia jointi dhaifu kwa kuunganisha chEmbe chembe. Hii huonekana wazi sana kwenye ngozi inapozeeka na kubakia tepetepe.

Pia tukumbuke kuwa takataka au makapi yanayotokana na michakato mbalimbali ndani ya mwili huharakisha kuzeeka kwa chembe chembe kwa kuwa na sumu na kemikali ambazo hazikutolewa kwa wakati na hivyo huchangia kuzeesha na kuchosha chembe chembe na kuzifanya zife kwa kukosa huduma bora zikilinganishwa na zile chembe chembe zisizozeeka.

MABADILIKO YA KAWAIDA YA MCHAKATO WA KUZEEKA

MACHO

1. Macho huanza kuonesha dalili za kushindwa kuona vizuri kati ya umri wa miaka 30 mwishoni na 40 mwanzoni. Macho huendelea kupungua nguvu zaidi na zaidi kadiri mtu anavyoendelea kuzeeka. Mtu hulazimika kukunja uso au kuweka ukurasa wa maandishi mbali akijitahidi kuona vizuri.

2. Kadiri mtu anavyozeeka lensi ya jicho hupoteza uwezo wake wa kulengesha mwanga unaotoka nje ya jicho kwenda kwenye retina ambako ndiko kuliko mlango unaoenda kwenye ubongo kunakotoa tafsiri ya kitu kilichopo mbele ya macho kama ni mtu, gari, mti na kadhalika.

3. Ukubwa wa tundu dogo linaloonekana jeusi kwenye jicho (pupil) hupungua kwa kukakamaa sababu hupoteza mnyambuliko (flexibility) kadiri mtu anavyozeeka hivyo kuruhusu mwanga kidogo sana kupitia lensi kwenda kwenye retina. Hivyo mtu hujaribu kukodoa macho na kukunja uso ili kuruhusu mwanga mwingi bila mafanikio kwani uzee ndio ulioleta matatizo hayo. Tatizo hili mtu huliona zaidi anapokuwa akiangalia kwenye mazingira ya mwanga mdogo sana kama vile anapoendesha gari usiku. Macho huchoka sana na uso huanza kuzoea kukaa katika mkazo huo na hatimae huanza kubadilika uso na kuwa na makunyanzi tofauti na wakati wa ujana wakati hapakuwa na ulazimishaji wa kuona.

4. Ulengaji wa kuona na kulenga (focusing) hupungua mtu anapozeeka na usahihi wa kuona kitu kwa mipaka, rangi na sura kwa uzuri hupungua. Uwezo wa kuona vitu vya pembeni vya jicho pia hupungua na kumlazimisha mtu huyu kugeuza shingo ili kuona kitu ambacho angeona bila kugeuza shingo, hasa wakati wa giza.

5. Uwezo wa kuona rangi pia hupotea kidogo kidogo kadiri ya umri unavyosonga mbele.

MASIKIO

1. Hupoteza uwezo wa kusikia sauti kali bali nafuu huwepo kama sauti zikiwa kubwa lakini za pichi ya chini.

2. Sauti ambayo wazee husikia vizuri wakati mwingine huonekana kero kwa vijana walio na masikio yanayosikia vizuri.

3. Maneno yakichanganywa na muziki na sauti zingine kidogo husababisha tatizo la kutokuelewa ujumbe kwa kadiri mtu anavyozeeka. Huwapo nafuu ya kuelewa na kufuata maongezi kama vyombo vya sauti zingine tofauti na maongezi vitazimwa kwa ajili ya mzee. Vyombo hivyo ni kama redio, runinga, ngoma au maongezi pembeni.

4. Vitu hivi kama vitaendelea kusikika huleta ghadhabu ya haraka na tafsiri tofauti kwa mzee kama vile huonesha kumdharau, kutokumheshimu na kadhalika.

5. Matokeo yanayojitokeza kwa mzee kwa kutokuzingatia haya ni pamoja na mzee huyo kutofurahia maongezi, kuzira (Kususa), malalamiko, kujitenga na kujenga dunia ya upweke. Hamu ya chakula hupotea na afya hudhoofu zaidi. Mzee huyu huendelea kuumia ndani kwa ndani na hivyo kinga yake dhidi ya maradhi huporomoka kwa kasi kutokana na msongo wa mawazo ambayo ni matatizo ya akili. Vyote hivi huongeza kasi ya kuzeeka na hatimaye kupoteza maisha.


LADHA YA CHAKULA NA HARUFU

1. Milango ya kupokea Ladha ya chakula hudhoofika na kushindwa kupeleka taarifa za ladha ya chakula kwenye ubongo kwa kadri mtu anavyozeeka. Hii hujitokeza mtu anapofikia miaka ya hamsini, hii huendelea hivyo hadi miaka sabini ambapo wazee wengi hupoteza sehemu kubwa ya milango hii na hivyo kuwa na matatizo ya kula.

2. Tatizo kubwa la wakati wa uzee ni ulaji wa tabu ambao husababisha afya kudhoofika sana hasa wasipokuwa na wasimamizi wa utaratibu wa chakula na aina za vyakula wapendavyo wazee wenyewe.

3. Matatizo ya ulaji yanaweza kuwa makubwa sana kama kuna tatizo la upendo na huduma hafifu anazoona mzee. Wazee huzira kwa urahisi wanapoona hawathaminiwi na kujiona hawana faida na kuona heri wafe badala ya kuendelea kusumbua watu. Hulalamika, hukata tamaa na kupoteza hamu ya kula. Hali hii pia huathiri milango ya ladha ya chakula.

4. Uwezo wa (kunusa) milango ya kupokea harufu nzuri na mbaya ya chakula kudhoofika na kushindwa kugundua chakula kizuri cha kutia hamu ya chakula.

FOUR LIFESTYLE STEPS TO A HEATHY HEART

4 Lifestyle Steps to a Healthy Heart
Tip of the Day 2/28/2010 by Dr. Weil (www.drweil.com)


Maintaining the right mix of healthy lifestyle habits is the best way to achieve optimal cardiovascular function. Incorporate the following into your daily routine to help promote the health of your heart:

1. Exercise. Regular exercise helps maintain the health of blood vessels, strengthens the heart muscle itself, and can help reduce heart disease risk factors including high cholesterol, high blood pressure, insulin resistance, and stress. Aim for 30 minutes a day of moderate aerobic activity on most days of the week. For individual guidance, consult a personal trainer.
2. Lose weight. If you are overweight or obese, even modest weight loss can significantly lower cardiovascular risks.
3. Don't smoke. Smoking is the major preventable risk factor for heart disease, and has negative health consequences for your entire body, from your taste buds to your energy levels to your skin. Seek support and guidance in quitting.
4. Manage stress. Uncontrolled stress can raise blood pressure, cholesterol levels, and homocysteine levels. Practice breath work, meditation, guided imagery, visualization or another relaxation technique, and participate in regular moderate exercise (including yoga and T'ai chi), stay social, and laugh often.