Thursday, February 25, 2010

MGOMBEA BINAFSI CHAGUZINI TANZANIA

25/2/2010

MAZOWEYA YA MHIMILI WA UTAWALA TANZANIA KUKEJELI, KUDHARAU, KUBEZA NA KUDHIHAKI MHIMILI WA UTOAJI HAKI (MAHAKAMA)

1. Katika Kitabu kiitwacho LAW AND JUSTICE IN TANZANIA: QUARTER OF A CENTURY OF THE COURT OF APPEAL, kilichohaririwa na Peter, C.M. na Kijo-Bisimba, H. (2007), aliyekuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa [CAT] na ambaye sasa ndiye Jaji Mkuu wa Tanzania, Mheshimiwa Augustino Ramadhani aliandika makala iitwayo “Twenty Five Years of the Court of Appeal of Tanzania and the Establishment of the East African Court of Justice” [Miaka 25 ya Mahakama ya Rufaa Tanzania na Uanzishwaji wa Mahakama ya Afrika Mashariki] ianziayo ukurasa 223 wa kitabu hicho.

Katika Ukurasa wa 227 ametoa maeneo matatu ya Maagizo ambayo Mhimili wa Utawala (The Executive) nchini Tanzania umeshindwa kutekeleza kutokana na tabia yake ya kudharau, kubeza, na kudhihaki Mhimili wa Utoaji haki kama ifuatavyo:

1. Malipo ya Mafao kwa Majaji Waondolewao Madarakani

Katika hili Mahakama ya Rufaa ilishauri kuwepo na Orodha ya Makosa yanayomnyima Mafao Jaji atiwaye hatiani au Chombo kinachotoa hukumu hiyo (tribunal) kitamke endapo Jaji Mkosaji anastahili au hastahili malipo ya mafao (terminal benefits) katika kesi ya MOSES J. MWAKIBETE V THE PRINCIPAL SECRETARY (Estab.) AND THE ATTORNEY GENERAL, Court of Appeal of Tanzania at Arusha, Civil Appeal No. 27 ya 1992 (haikuripotiwa).

Hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa na Serikali hadi wakati wa kuchapishwa kitabu hicho mwaka 2007 toka mwaka 1992.

2. Malipo ya Mawakili wa Kujitegemea Wateteapo Wahalifu Kwa Mujibu wa Sheria

Mahakama ya Rufaa ilipendekeza mwaka 1991 kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali [AG] (Andrew Change – Bwana Vijisenti) kupitia upya malipo haya yaliyolipwa kati ya Tshs.120/= na Tshs.500/=; wakati huo ikilinganishwa na kiasi cha chini ya nusu dola ya Kimarekani ($).

AG hakuwahi kutekeleza agizo hili hadi miaka mitano (5) baadaye wakati CAT ilipoamua yenyewe kuongeza kiasi hicho hadi kufikia Tshs.100,000/= kwa kutumia fursa iliyojitokeza katika kesi ya THE ATTORNEY GENERAL V N.I.N. MUNUO NG’UNI [1998] TLR 464.

3. Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984

CAT ilipendekeza masuala ya kutafsiri Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 na masuala mengine nyeti ya Kikatiba yasiyofikishwa CAT kwa uamuzi yatazamwe na yafikiriwe kubadilishwa katika kesi ya SEIF SHARIFF HAMAD V SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR (SMZ) [1998] TLR 48.

Jambo hili halikufanyiwa kazi na miaka mitano (5) baadaye CAT ikalikumbusha pendekezo lake kwamba Mamlaka zinazohusika pande mbili za Muungano zichukue hatua za makusudi kuoanisha vipengele viletavyo migongano ndani ya Katiba zote mbili; ile ya Zanzibar ya mwaka 1984 na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977. HAYA HAYAJATEKELEZWA.
[mwisho wa sehemu iliyoandikwa na Jaji Mkuu)



4. MTAFARUKU ULIOPO SASA WA MGOMBEA BINAFSI
Ijumaa, Februari 12, 2010, Bw. Philip Marmo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, alisema kuwa katika uchaguzi mkuu ujao suala la kuwepo Mgombea binafsi kama ilivyoamuliwa na Mahakama Kuu tarehe 5 Mei, 2006 na kufafanuliwa na CAT tarehe 20 Februari, 2010, haliwezi kupata nafasi kwa kuwa muda wa maandalizi hautoshi.

Kauli hiyo ililenga kukejeli, kupinga, kudharau, kuasi na kubeza tamko la Mahakama ya Rufaa la Feruari 10, 2010 lililobariki amri iliyotolewa na Mahakama Kuu tarehe 5 Mei, 2006.

Maelezo kama hayo pia yameshatolewa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dk. Werema, na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (National Electoral Commission [NEC]).

Saturday, February 20, 2010

MTOTO ALELEWA NA NYANI TANZANIA !!!

Date: Thursday, 20 November, 2008, 11:43 M MAJIRA NEWSPAPER, TANZANIA.

Mtoto Baraka Rose (11) aliyelelewa na nyani akiandika majina yake mbele ya waandishi wa habari Dar es Salaam jana. Kulia akionesha kovu la risasi mguuni alilojlipata katika harakati za kuachanishwa na nyani mlezi wake mwaka 2005. (Picha na Richard Mwaikenda)

Na Gladness Mboma

WATANZANIA wameombwa kujitokeza kumsaidia kielimu mtoto Bahati Baraka Rose (11) ambaye anadaiwa kulelewa na nyani baada ya kutupwa porini akiwa mchanga wilayani Bukombe, Shinyanga.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kimanga, Tabata, Bw. Pastory Kyombya, alisema mtoto huyo kwa sasa analelewa na Bibi Rose Mbwambo wa Kimanga.

Alisema Bibi Mbwambo alikabidhiwa mtoto huyo na Serikali wilayani Bukombe baada ya kufuata taratibu zote za kiserikali.

Alisema Katibu Tawala wa Wilaya ya Bukombe, Bw. Richard Nhende, ndiye aliyemkabidhi Bibi Mbwambo mtoto huyo ili amlee baada ya kumwomba.

Bw. Kyombya alisema mtoto huyo anaomba kupelekwa shule kama anavyoshuhudia wenzake wakienda shule na kuwaomba wasamaria wema wajitokeze kumsaidia ili aanze shule mwakani.

Naye Bibi Mbwambo alisema alimchukua mtoto huyo Agosti mwaka huu akiwa kwenye biashara zake Bukombe.

"Nilikuwa nimepanga kwenye nyumba ya kulala wageni ya Neema, nikiwa na wenzangu, mama mmoja (hakumtaja jina) ambaye alikuwa akitupikia chakula alitujia na kutueleza matatizo aliyonayo mtoto Baraka.

"Nilimwonea huruma sana Baraka, baada ya mama huyo kutuelezea historia yake nzima na kwamba hana ndugu na maisha yake ni ya kutangatanga na kututaka tumsaidie," alisema.

Alisema yeye binafsi aliingiwa na huruma ndipo alipofuata taratibu zote za kumchukua mtoto huyo na kuja naye Dar es Salaam kumlea.

Bibi Mbwambo alisema atamtunza mtoto huyo kama anavyotunza watoto wake ila aliomba wasamaria wema kujitokeza kumsaidia ili aanze masomo mwakani ikiwezekana shule ya bweni.

Alisema mtoto huyo alilelewa na nyani miaka kadhaa porini kabla ya kuchukuliwa tena na binadamu baada ya nyani huyo mlezi kuuawa kwa risasi.

Bibi Mbwambo alisema inadaiwa mtoto huyo aliokotwa na nyani akiwa kwenye mfuko wa 'rambo' akiwa mchanga na kumlea kwa miaka mitano.

"Askari wa wanyamapori wa Ushirombo, Bukombe, ndio waliofanikisha kupatikana kwa mtoto huyo baada ya siku moja kumwona nyani akimnyonyesha.

"Hata hivyo, inadaiwa askari hao walipata shida kumchukua mtoto huyo baada ya nyani mlezi kukimbia naye mara zote kila alipokuwa akiwaona, hivyo kuchukua muda mrefu kumpata," alisema.

Alisema mtoto huyo aliendelea kulelewa na nyani huyo hadi alipofikisha umri wa miaka mitano na baadaye askari hao kumvamia tena ili kumnyang'anya mtoto huyo na kusababisha vurugu kubwa kati yao na nyani mlezi.

Bibi Mbwambo alisema katika vurugu hizo, askari walimfyatulia risasi nyani huyo na kumuua huku risasi moja ikimpata mtoto huyo kwenye kidole cha mguu wa kushoto.

Alisema askari hao walimchukua mtoto huyo na kumpeleka katika hospitali ya Bukombe ambako aliendelea kulelewa hospitalini hapo.

Bibi Mbwambo alisema watu mbalimbali walikuwa wakimchukua mtoto huyo na kumlea na walioshindwa walikuwa wakimrudisha hospitalini hapo, lakini msamaria mwema alimchukua, lakini mtoto huyo alimtoroka na kuingia mitaani na kuishi maisha ya shida.

Alisema Baraka alikwishazoea kuishi maisha ya porini, akiparamia miti na kusababisha wasamaria wema waliokuwa wakimlea kulazimika kumfunga minyororo ili asitoroke.

Wednesday, January 20, 2010

HABARI ZA MAENDELEO YANGU KATIKA MASOMO YA UZAMIVU

1. Nilipoomba kwenda kusoma kwa kutumia Udhamini wa Serikali ya nchi ya Marekeni (USA) chini ya Ufadhili wa Mfuko wa Hubert Horatio Humphrey (HHH Fellowship) mwaka 2007, nilielezea nia yangu ya kwenda kusomea masomo yatakayonielekeza katika kuja kuanzisha Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wananchi (MZUMBE UNIVERSITY LEGAL AID CLINIC - MULAC)kwetu Chuo Kikuu, Mzumbe, Tanzania.

2. Nilibahatika kupata fursa ya kwenda kusoma nchini USA katika Chuo cha American University, Washington College of Law (WCL); kilichopo mjini Washington, DC; ambao ni mji mkuu wa Serikali ya nchi hiyo.

3. Niliondoka na kwenda USA kufanya masomo hayo kuanzia Agosti 2, 2008 hadi Juni 12, 2009. Wakati nipo masomoni, nilitayarisha Andiko lililoeleza namna ya kuanzisha Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wananchi (Starting a Legal Aid Clinic at Mzumbe University, Tanzania).

4. Niliporejea Juni 13, 2009 na kuripoti ofisini wiki iliyofuata, nilimuona Mkuu wangu wa Kitivo, Bw. Eleuter Gabriel Mushi na kumfahamisha juu ya masomo yangu yaliyonichukua miezi kumi huko USA. Yeye alinielekeza kwamba jambo hilo kiutaratibu huanzia katika Idara yangu husika (Idara ya Sheria za Kimataifa - Dept. of International Law). Baada ya kulishughulikia katika Idara kwa kuitisha mkutano wa Wanataaaluma na kuelezea juu ya Andiko langu na kujadiliwa (Paper Presentation), nipokee maoni na mapendekezo ya wasomi ili niyaingize katika Andiko hilo kwa nia ya kuliboresha.

5. Nilipofikisha Andiko langu kwa Mkuu wangu wa Idara; wakati huo Profesa Padma Sabaya, akaahidi kulishughulikia jambo hilo. Nilipolifuatilia baada ya wiki moja, nikaarifiwa na Katibu Muhtasi kwamba huyu Profesa kaenda India kwao kwa likizo ya mwezi mmoja. Nikauliza aliyemuachia ofisi. Nikaambiwa kuwa hakumuachia ofisi mtu yeyote na hivyo Andiko langu analo yeye na hajalifanyia kazi.

6. Kwa bahati wakati huo huo, ikatoka orodha mpya ya Walimu wa Kitivo cha Sheria na Idara zao zilizopangwa upya. Nikajikuta nimepangwa katika Idara ya Sheria za Madai na Jinai (Civil and Criminal Law Dept.) nami sikuwa na neno juu ya hilo. Mkuu wa Idara hii ni Bw. Ignas Punge. Hivyo nikachukua hatua ya kumuona mkuu wangu huyo mpya na kumweleza juu ya azma yangu ya kutoa Andiko kwa Wanataaluma wa Mzumbe kwa Kujadiliwa kwa ujumla. Yeye aliliafiki moja kwa moja na kuniagiza nimfikishie andiko hilo mapema iwezekanavyo.

7. Tarehe 15/10/2009 nilifikisha andiko hilo kwa Mkuu wangu wa Idara Bw. Ignas Pungem kupitia kwa Katibu Muhtasi wa Kitivo cha Sheria. Hii ilikuwa tayari mwezi mmoja umepita tangu nifikishe andiko langu kwa Mkuu wa Idara wa Kwanza Profesa Padma Sabaya. Safari hii kwa bahati mbaya Andiko langu halikumfikia Mkuu wa Idara yangu kama nilivyotaraji.

8. Mkuu wangu huyo wa Idara akishirikiana na Wakuu wa Idara wenzake Bw. Benjamin Jonas na Bw. Cosmas Julius walifanya bidii kubwa kuona kwamba Andiko langu linajadiliwa na Wanataaluma ipasavyo tarehe 1/9/2009; na kuniongoza jinsi ya kufanya matayarisho muhimu ya maandalizi ili jambo hilo lifanyike ipasavyo. Mojawapo ya mambo hayo ilikuwa kumtafuta Mjadili Mkuu (Main Discussant), kuandaa ratiba na kutoa matangazo chuoni juu ya tukio hilo; mambo ambayo niliyafanya kwa ufanisi mkubwa chini ya uongozi na maelekezo yao.

9. Nililazimika kuanza mara moja kazi ya kuingiza mapendekezo na maoni ya wachokozi (critics) walioshiriki katika Mjadala wa tarehe 1/9/2009. Pamoja na kwamba sikuweza kupata fedha mara moja za kufanyia kazi hiyo. Baadhi ya mapendekezo yaliyotolewa na wachokozi hao ni kuwa ni muhimu kwa mimi kushirikisha vyombo na asasi na wadau mbalimbali wa kisheria juu ya jambo hili; na pia kufanya utafiti mdogo (situational analysis) kujionea na kujihakikisha katika Mahakama za ngazi ya chini kabisa nchini zinaamua kesi za aina ipi, ili nasi hatimaye tutakapokuja kuanza Kituo Chetu cha Msaada wa Sheria kwa Wananchi, tujue tutaanzia na kesi za aina ipi.

10. Nilianza na kuwaona wadau mmoja mmoja na kufika katika mahakama za Mwanzo za karibu na Chuoni kwetu. Pia nilijitahidi kuwahoji binafsi Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu Raymond Mwaikasu (tarehe 19/9/2009) wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCO) na Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu James Mwalusanya aliyeko Dodoma.

11. Nilitembelea pia Mahakama za Wilaya ya Morogoro Vijijini (Tawa Mkuyuni,Mikese, Ngerengere, Manispaa ya Morogoro (Nunge, Chamwino, Kingolwira), Mvomero (Mgeta, Mkongeni(Vikenge) na Dodoma Manispaa(Makole). Wakati wote nitembembelea Mahakama hizi mbalimbali, nilishaomba Masurufu kazi yaliyofikia Tshs.992,200.500/= ili kuifanya kazi hiyo kikamilifu. Hadi leo hii niandikavyo Ufupisho huu, tarehe 20/1/2010, Fomu hiyo ya Masurufu iliyosainiwa na Mkuu wangu wa Idara Bw. Ignas Punge toka tarehe 18/9/2009, iko mezani kwa Mkuu wangu wa Kurugenzi cha Mafunzo Endelevu (Institute of Continuing Education - ICE); ambaye ndio mwenye mafungu husika ya kufanyia utafiti wangu; na hivyo ndio muidhinishaji wa mwisho wa kutolewa masurufu hayo chini ya Kurugenzi yake. Yaani miezi minne (4) baadaye, bila kufahamu ni lini fomu hiyo itaridhiwa na kuelekezwa ikaandikiwe malipo hayo.



12. Kwa uzoefu wa kujua tatizo nililolielezea hapo juu, hata hivyo; tulishirikiana vizuri sana na viongozi hao waliotajwa na kufanikwa kumpata Mjadili Mkuu (Discussant) wa Andiko langu kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Mhadhiri Msaidizi, Bi Asina Omari; na kazi hiyo ya kitaaluma ya kutoa Andiko hilo kwa Wanataaluma wa Mzumbe ilifanyika vizuri tarehe 1/9/2009 katika Darasa la LT.3 Chuoni Mzumbe kuanzia saa 4.00 asubuhi. Walioshiriki katika kufanikisha siku hiyo ni pamoja na Bw. Thobias Mnyasenga wa Kitivo Cha Sheria na Bw. Evans Kautipe na Bw. Barnabas Chomboko; wote wa Idara ya Huduma za Kiufundi ya Maktaba Kuu ya Chuo Kikuu Mzumbe.

13. Mara baada ya zoezi hili; ili jambo hili lifikie linakotakiwa; nililazimika mara moja kuanza kuingiza maoni na mapendekezo mbalimbali kutoka katika Wachokozi walioshiriki (critics) katika Andiko langu. Pia niliingiza yale niliyoyashuhudia katika Mahakama za Mwanzo mbalimbali nilikotembelea na maoni na mapendekezo ya wadau nilioweza kuwahoji. Wakati huo huo sijakata tamaa kwamba nitaendelea kuwahoji wadau wengine zaidi na kutembelea Mahakama na Ofisi nyingine zaidi katika kufanikisha zoezi hili.

14. Tarehe 28/10/2009 kulikuwa na Mkutano wa Kitivo cha Sheria (Internal Examiners Board of the Faculty of Law). Nilitaraji kwa nia njema kabisa kwamba Andiko langu lingekuwa moja ya Ajenda ya Mkutano huu kwa kuwa hakukuwa na fursa ya mkutano mwingine Kitivoni kujadili jambo hili. Kwa bahati mbaya, Andiko langu halikuwahi kumfikia Mkuu wangu wa Idara Bw. Ignas Punge; badala yake Katibu Muhtasi Grace Nyamhagata, alifikisha lile Andiko langu kwa mwalimu mwingine kwa makosa (Prof. Khan). Baada ya kugundua kosa hili siku hiyo ya mkutano, nikahakikisha safari hii nimefikisha Andiko langu kwa Mkuu wangu kwa mikono yangu miwili. Mkuu wangu wa Idara amenifahamisha kwamba Andiko hilo litajadiliwa katika kikao kijacho cha Kitivo kabla ya kwenda kwenye vikao vya juu zaidi.

15. Hivyo, leo niandikavyo Ufupisho huu wa jambo hili; tarehe 20/1/2010; haijatokea fursa nyingine ya kufanyika Mkutano katika Kitivo cha Sheria, Chuo Kikuu Mzumbe. Na hiyo ndio fursa inayosubiriwa ili Andiko langu lijadiliwe kabla ya kufikishwa na Kitivo katika Mkutano wa Kitivo (Faculty of Law Board), ili hatimaye likikishwe katika Kamati ya Seneti (senate). Fursa inayoonekana kujitokeza hivi karibuni ni Mkutano wa Kitivo Ujao utakaojadili Matokeo ya Mitihani ya Kitivo cha Sheria unaotarajiwa kufanyika baada ya kusasahihishwa Mitihani ya Semesta ya Kwanza ya Chuo kwa mwaka 2009/2010, kunako mwishoni mwa mwezi Februari au mwanzoni mwa Machi, 2010. Nami naisubiri fursa hiyo kwa hamu sana, ili hatimaye jambo hili liweze kupiga hatua inayofuata.

16. Hadi hapa, nilidhamiria kuelezea mtulinga nipitiao katika kufanikisha jambo hili ambalo si tu kuwa ni kwa manufaa ya Chuo Kikuu Mzumbe, bali ni kwa manufaa yangu kitaaluma kwa sababu hatimaye nataraji kulichapisha Andiko hilo litakapopitishwa na Seneti, ili iwe sehemu ya kufikiriwa kwangu kupandishwa cheo; pamoja na Maandiko mengine. Kigezo kimojawapo cha kupandishwa cheo katika ngazi za kitaaluma katika vyuo vya kitaaluma ni kutoa machapisho ya kitaaluma.

Zainab Mwatawala, Chuo Kikuu Mzumbe, 21/1/2010.

Tuesday, January 19, 2010

MIAKA 42 YA MAADHIMISHO YA KUUWAWA KWA DR. MARTIN LUTHER KING WA USA

Imechangiwa na Kaleema Hasan Sumarey wa Detroit, USA.
Monday, January 18, 2010
Dr. Martin Luther King, Jr, 42 Years Later.
I was sixteen years old the day Dr. King was murdered, sixteen years old. I was deeply involved in the radical black student movement and thus considered Dr. King's message of non-violence as wrong headed and too deeply embedded in religious rhetoric. I respected Dr. King very much, just did not at the time agree with his tactics. This was a condition of my political education, to love him, but not “follow him.” To defend him and join him, but not “follow him.” We live and learn.

You have to remember it was the sixties, I was sixteen and the urgency for black liberation was hot in my heart and blood. I wanted to be a free woman in all ways and did not want to feel like I was begging some benevolent white person for my freedom and the freedom of my people. It appeared to me that Dr. King’s message carried that signification.

On that April 1968 day I fully understood the signification of his message. I had been ill and stayed home from school and "organizing the student masses." When the report came on my little clock-radio, that Dr. King was dead, I cried for a long time. I had no inner power to stop my tears; it was if my own brother or father had been killed. I spoke these words aloud to myself, "if they will kill Dr. King, they will kill anybody." This was the one thought I had about his murder. I was sixteen and understood that “freedom wasn’t free.” And that if I was serious, I had to be willing if called upon, to give what all our great freedom fighters had given, their lives, personal safety, freedom and aspirations for fame, fortune and recognition.

It was at that moment I appreciated the importance of critical thinking or Malcolm’s revolution of the mind. This lesson, I might add, had also been drilled into me by my two Mississippi parents. "Always think for yourself." "Don't be an educated or any other type of fool." "Do what's right." "Watch the crowd you follow, same as you watch the ones you think you are better than."


It was at Dr. King’s death, that moment in 1968 that I knew I had nothing to lose and everything to gain by continuing to be as revolutionary as I could be. Given what I have learned over the years about my own personal shortcomings, failures and periods of deep sleep and disenchantment I continue to experience the realization that this ain't a friendly place, but that, that ain't not the point.

To struggle is the point. While there has been much demonizing of the sixties, for me, it was the best time to be a black teen-age girl/woman. It was the best time because everything and everyone was subject to examination, unlike today, where most things are to be accepted on face value or simply dismissed based on some infactual (I know its not a word) mind twisting wordology designed to invoid meaning through obtained through close inspection of concepts, ideological origins, purpose and usage, ownership, reality construction, meaning manufacturing, disinformation construction, knowledge for whom and what purpose. . .

The sixties and being sixteen taught me the value of struggle. I learn everyday the value of living for more than your own ambitions and ideas. Dr. King’s death on my generations watch, taught me the honor of taking the bullet (death, poverty, any number of assassin's tactics) that can cause a silent resurrection of people of good will all over the world to make sacrifices in order to make the world better, more equitable, more just, more compassionate, more safe, and more peaceful for the people now suffering from the greed, inhumanity and opportunism of the few. That bullet Dr. King took (and Malcolm and so many others) woke me up. And each time I doze off to sleep, I think of, dream of, and dream about Dr. King. And each time I wake from my sleeping I am refreshed, I am sixteen again, only these times, I pray 42years wiser.
Posted by kaleema hasan at 2:26 PM 1 comments
Labels: Remembering Dr. King and April 4 1968

SOCIAL SECURITY REGULARITY AUTHORITY IN TANZANIA

Mohamed el Munir Safieldin Has sent in the following Contribution::

Social welfare and protection system should be multi-dimensional targeting various vulnerabilities and not one group such as the aging people.



I thank Mr. Festo E. Maro for his contribution and the questions he posed with regard to the management of the to-be-established Social Security Regularity Authority. With no intention to undermine the main question posed in this contribution, I would like to propose widening the scope of social welfare to make it a net work of well coordinated schemes that, when taken together, they address all vulnerable segments of the society whether or not they contribute (or contributed at a previous stage) to a social welfare fund. The reason I am making this proposal is that a number of studies in Africa and Latin America have shown that an increasing number of aging people is using their welfare benefits to support their grand children (many of them orphaned by HIV/AIDS) or their daughters who have become single-mothers. This sharing of benefits by the recipients within an extended family network benefits some unintended members but decreases the material benefits of the intended members. The ultimate result of such situations is that the beneficiary and the individuals he/she feels obliged to support will all survive at levels below descent human living standard. The overall objective of achieving social welfare for the society will be attained only when we have a social protection system that cares for all vulnerable groups such as single mothers; widows; people with disabilities; aging people; and vulnerable children.



It is also important to note that the number of people who contribute/contributed to pension funds and other contributory social welfare systems in developing countries are limited compared to other vulnerable groups in these societies. This is attributable to reasons that have to deal with types of employment and the relatively recent history of welfare programs in these countries.



Who should manage such schemes or system? Certainly the state has a prime responsibility here. However, for the purpose of accountability and transparency, senior technical positions should be offered on competitive grounds to those who have the required technical competencies, commitment, vision and zeal. Beneficiaries and civil society organizations should be represented (as appropriate) at the central and sub-national levels of the management structure.



How should such management systems work? The decentralization of the management structure of social protection is important. The identification of beneficiaries and the assessment of benefits/impact on them must be entrusted to accountable management structures at district levels.



Regards



Munir Safieldin
Deputy Representative
UNICEF Tanzania Office

Monday, January 18, 2010

MALUMBANO YA SIASA ZA TANZANIA NA ZANZIBAR

From: yussuf_salim@hotmail.com, January 18, 2010


Makamba sikia : Amani atimiza ahadi kwa Marehemu Baba yake

Makamba anazidi kukiaibisha chama chake kwa mara nyengine tena, kwa kutoa kauli zisio na mvungu. Katika mtindo wake wa kawaida wa kusema kwanza halafu kufikiri baadae, anarejea tena kuwafanya viongozi wengine wa nchi, kukenya –kenya huku wakigubika nyuso zao zisionekane. Kwa viongozi wengine wa CCM hali hii kwa mara nyengine tena imewafanya wajionee aibu upya. Kauli za kuvurumisha maneno ovyo, hulengea aliyekuwemo na asiyekuwemo. Mwenyewe Makamba, akijiona stadi wa kusema, hatambui kwamba hajirejeshi yeye mwenyewe tu nyuma au sio kuirejesha CCM tu nyuma , bali heshima ya Tanzania nzima inaathirika wakati kiongozi wa juu kama yeye nchini, kila kukicha, heshi kuteleza na kujiona kapwetereka kwenye matope na kuipaka nchi nzima matope.

Hivi punde shehe Makamba aliushangaza ulimwengu wa waungwana alipotoa kauli za kuwakashif Watanzania wanaoheshimiwa Ulimwengu kote. Kauli hizo zilikuwa sawa na matusi mazito kwa Watanzania wote, Waafrika na jumuia ya Kimataifa kwa jumla ambao walikuwa wakiwathamini na kuwa enzi viongozi hao wakiwemo Mwana Diplomasia mashuhuri Salim Ahmed Salim na Mheshimiwa Jaji Warioba, wote wawili wakiwahi kushika nyadhifa nzito za Uwaziri Mkuu wa Tanzania. Vipaji viwili hivi vimeshaweka rikodi sio Tanzania tu bali hata Ulimwengu mzima wa Kimataifa. Leo Katibu Mkuu wa CCM anawatukana Viongozi hao hadharani bila kuona hata haya au vibaya.

Kipi chema mtu utatarajia kitatoka katika mdomo wa Katibu Mkuu huyu, ikiwa bwana huyu wakati huo huo atajiweka mstari wa mbele kutaka kuwafyeka wale Wabunge mashujaa wa CCM waliojitolea kutetea maslahi ya Watanzania wasiojiweza na kutetea mali ya Tanzania kwa jumla, lipi jengine hatalifanya. Badala ya desturi ya Kiongozi wa juu wa chama kujivunia kuwa na Wabunge wapenda nchi na walinda mustakbal kama hawa, kinyume chake tunamuona anatumia kila mbinu, pamoja na kubadili katiba, kuhakikisha anawaangamiza Wabunge hao. Mshangao mkubwa na bumbuwazi linampiga mtu akitanabahi kwamba kuna Kiongozi kama huyu: na kujiuliza ni maslahi ya nani mtu huyu anayatetea? Ya mafisadi waliopita au ni ufisadi ujao? Na ufisadi huo una majoka gani ndani ya mapango yake? Kama itakavyokuwa, majoka hayo hayataleta maendeleo Tanzania bali yatazidi kurejesha maendeleo nyuma na kuzidisha umasiki kwa wengi na kuzidisha utajiri kwa wachache. Ama kweli, wale waliosema kwamba kuna wanajeshi fulani hutumia vichwa vyao na wengine kutumia BUNDUKI zao, hawajakosea.

Hivi punde Wazanzibari wameamua kuchoshwa na kupigana na kuchingana wenyewe kwa wenyewe na wameamua kurudi kwa Mola wao, kumuomba msamaha kwa yaliyopita na kuamua kusameheana na kuheshimiana kama ni Wazanzibari sawa bila ya kujali mirengo yao. Wazanzibari wametanabahi kwamba hakuna yoyote kati yao aliye bora ya mwenziwe mbele ya Nchi yake na mbele ya Mola wake. Wote wamezaliwa sawa na wana haki sawa katika nchi yao ya Zanzibar. Viongozi, Rais Amani na Maalim Seif, wameamua kuchukuwa dhamana zao walizopewa na wafuasi wao, nayo ni kuwaongoza wao na nchi yao ielekee kwenye Mustakbal bora wa Zanzibar na Wazanzibari wote.

Laa, kwa Makamba hayo haiwezekani, jambo jema na usalama kwake ni marufuku kwa Zanzibar. Kila watu wakitesana, kuuwana, kunajisiana, kufanya watoto wadogo mayatima na wanawake vizuka ndio akina Makamba wanavyofurahi. Wanageuka kama wale Waspeni wanaofurahishwa na mchezo wa n´gombe na kuona raha pale n´gombe anapochirizika damu na hatimae kutiwa upanga wa roho na kufyatua fyatua miguu huku wakikata roho wakizungukwa na dimbwi la damu. Hali kama hiyo huwa wanaifurahia kina Makamba wanapowaona Wazanzibari wakikata roho wakimiminika na kuogelea katika madimbwi ya damu zao wenyewe.

Akina Makamba hawachoki kutumia vibaraka na vitimba kwiri vyao vinavyo vikiwemo vile vinavyo gombania tiket za Uraisi wa Zanzibar kuvusha wanajeshi na polisi kutoka Bara kwenda Zanzibar kuuwa, kunajisi n.k. na wao wakikaa juu ya majukwaa na kupiga makofi.

Viongozi wema mfano wa akina Mwanadiplomasia Salim Ahmed, Jaji Warioba, Wabunge washupavu wanaopigania walalahoi, ni viongozi wanao hatarisha maslahi ya akina Makamaba na Msekwa. Viongozi wanaowatakia mema Watanzania ni maadui kwa watu kama Makamba na Msekwa. Kina Makamba hawaoni raha kama madimbwi ya damu za Wazanzibari hayamwagiki kila kukiwa na uchaguzi. Kwa hivyo kwao Viongozi kama Rais Amani na Maalim Seif ni watu wanaowaogopa sana na sifa kwao kuwawekea kila vizingiti.

Lakini Makamba kasahau kwamba kuna jambo linaloitwa ”Ya Mbayana”, na hili lina ashirika wazi pale Makamba anapojaribu kumnukuu Mwenyekiti Mao na kusema kwamba ”ukimuona adui anakusifu ujue ana lake. ” Kauli hii ina ukweli kabisa na kumdhihirisha nani ni adui wa Wazanzibari na adui wa kutaka kumuangamiza Rais Amani, yule wa msatri wa mbele kabisa wa kutaka kuafanya hivyo ni Makamba akifuatiwa na Msekwa. Wanajaribu kumramba kisogo Rais Amani wakidhani hawaoni. Wamejionyesha kwamba ni wao ndio hasa MAADUI wenyewe, kama alivyosema Mwenyekiti Mao. Huyu wa pili, yaani Msekwa, vile vile anamuonea choyo cha kisiasa Rais Amani kwa kuwa ingawa ni Makamu Mwenyekiti kama yeye, lakini mwenziwe ni Rais wa nchi nzima, ingawa walifanya mbinu za kuinyan´ganya Zanzibar U-Makamu wake wa U-Rais.

Napenda kumkumbusha Katibu Mkuu Makamba kwamba, Mwenyekiti Mao katika mengi aliyosema, alisema vile vile kwamba, ”kuna kutofautiana kwa kimgongano na kutofautina kusiko kwa kimgongano” yaani ”antagonistic contraditions na non-antagonistic contradictons” au msemo huo haujui ? Kutokana na msemo huo ndio maana Mwenyekiti Mao na Chang Kai Chek wakaamua kuungana na kumtoa Mjapani NCHINI mwao. Sasa inaonyesha Rais Amani na Maalim Seif wamesoma somo hilo vizuri, ila Katibu Makamba bado anataka damu imwagike akidhani vitimbwa kwiri wake watamsaidia kwa njama hizo.

Somo jengine muhimu Mheshimiwa Makamba inafaa ajifunze ni kwamba Rais Amani anatekeleza lile Marehemu Baba yake alilolianza lakini kutowahi kulimaliza. Sidhani kama hili analijua ndugu Makamba, kwani ni wale tu wanaojua shina na kina cha historia ya Zanzibar ndio wanaoweza kujua undani huo. Makamba akae ajue kwamba kabla ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mzee Abeid Amani Karume na Sh. Ali Muhsin walikuwa na mazungumzo ya siri kabisa kutaka kufanya serikali ya MSETO Zanzibar. Kwa bahati hii au ile Mapinduzi yakatokea kabla mpango huo kutekelezwa na ndio maana wakati Sh. Ali Muhsin akishindikizwa kuingia katika kambi ya Rahaleo alipokamatwa baada ya Mapinduzi Mzee Karume akamwambia kwamba ”haya Mapinduzi yameharibu mpango wetu Serikali ya Kitaifa”.

Hio ni sababu moja wapo ya kumfanya Rais Amani akawa na deni la kutimiza ahadi kwa Marehemu Baba yake.

Wasalaam

Dr. Yussuf S. Salim

Copenhagen

Denmark