Wednesday, November 18, 2009

KIINI CHA KUANZISHWA KWA UMOJA WA VIJANA WA TANU TANGANYIKA!

Nilitaka nikumegee kipande cha kitabu cha SIMBA WA VITA KATIKA HISTORIA YA TANZANIA - RASHIDI MFAUME KAWAWA kilichotungwa na John M J Magotti. Kuna sehemu mwandishi anatueleza undani wa TYL.

Lo and behold, Banisraeli nikawakuta tena lakini kwa nini tuandikie mate? (page 43):

Kuanzishwa kwa Umoja wa Vijana wa TANU



Muasisi wa Umoja wa Vijana wa TANU alikuwa ni Kawawa. Mwaka 1958, Kawawa pamoja na Mwalimu Nyerere walihudhuria sherehe za Ghana kutimiza mwaka mmoja wa Uhuru (1958). Katika kuhudhuria sherehe hiyo wote wawili walipata fursa ya kukutana na Bi. Golda Meir ambaye wakati huo alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel . Bi. Golda Meir aliwaeleza jinsi Israel ilivyokuwa ikiwaandaa vijana wake. Utaratibu wa Israel wa kuwaandaa vijana ulimvutia sana Mwalimu Nyerere na Kawawa. Waliporejea nyumbani, Mwalimu alimpa jukumu Kawawa la kuwaandaa vijana kama vile Isrel ilivyokuwa ikiwaandaa vijana wake.



Kawawa alianzisha rasmi Umoja wa Vijana wa TANU mwaka 1958. Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Umoja Vijana ulimchagua Kawawa kuwa Mwenyekiti wao wa kwanza. Kabla ya kuanzisha Umoja wa Vijana wa TANU, Vijana walikuwa wamejiunga katika vikundi mbali mbali, kama vile, Watoto wa TANU, Bantu Group na Vijana wa TANU na "Station Group" ya Tanga ambacho baadaye kilibadili jina na kuwa TANU Volunteer Corps. Baada ya kuundwa kwa Umoja wa Vijana wa TANU, vikundi vyote hivi vikatoweka kwa maana kwamba nafasi ya vikundi hivyo ilichukuliwa sasa na Umoja wa Vijana wa TANU.



Hawa Vijana wa TANU ndiyo walikuwa wa kwanza kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ilipoanzisliwa mwaka 1964. Tanzania iliendelea kujifunza kwa Waisrael masuala yahusuyo vijana JKT ilipoanzishwa baadhi ya vijana wa Umoja wa Vijana wa TANU walipelekwa mafunzoni Israel kwa lengo kwamba ya kuhitimu mafunzo yao ndiyo wangekuwa wakufunzi katika Jeshi In Taifa na hivyo ndivyo ilivyokuwa

Monday, November 2, 2009

HAYA NDIO MATOKEO YA KUTOTUMIA WENYEJI WAZALENDO KATIKA KAZI NYETI KAMA HII TANZANIA

IMETOKA BBC 30 OKTOBA, 2009.

Charging elephant kills BBC guide
Map of Tanzania
Mr Turner was an ex-army officer who had worked with the BBC before

A man who worked as an expedition guide for a BBC children's programme has died after being charged by an elephant in Tanzania, it has been revealed.

Anton Turner, a 38-year-old Briton, was assisting with the filming of an episode of the CBBC series Serious Explorers, a spokeswoman said.

The show was tracing the footsteps of explorer David Livingstone in Africa.

"We understand at this stage that he was charged by an elephant and was mortally injured," she added.

A doctor who was travelling with the expedition treated Mr Turner at the scene, but it was understood he died shortly after the incident, the spokeswoman said.

"Three children were with the filming party at the time of the accident and are all safe. Their safety remains a priority, and all the children have been airlifted from the area.

She added: "We would like to extend our deepest sympathy to Anton's family and friends. Anton was an extremely experienced expedition safari and wildlife ranger and former Army officer who had worked with the BBC in the past.

"As is usual with a serious accident an immediate and thorough BBC investigation into the circumstances of this incident has already begun."

A Foreign Office spokeswoman said: "We can confirm the death of a British national in Tanzania on Friday.

"Next of kin are aware, and we are providing consular assistance."

Sunday, November 1, 2009

UCHAGUZI TANZANIA UNAVYOJENGEWA MAZINGIRA YA KUFINYANGA DEMOKRASIA TANZANIA

Na Abdallah Bawazir

1st November 2009

http://www.ippmedia.com/images/frontend/headline_bullet.jpg Yahusu Mabalozi wanaoingilia mambo ya nchi

http://www.ippmedia.com/media/picture/large/Memb.jpg

Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.

Vyama vya upinzani vimelaani kauli iliyotolewa na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, kuwaonya mabalozi wanaowakilisha nchi zao nchini kuwa wanaweza kutimuliwa endapo wataingilia mambo ya ndani ya nchi.

Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti jana, baadhi ya viongozi wa vyama hivyo, wametahadharisha kuwa endapo onyo hilo la serikali litatekelezwa, Tanzania inaweza kuingia katika orodha ya nchi zenye mgogoro kidiplomasia na nchi fadhili na pia inaweza kuwekewa vikwazo vya kiuchumi na watakaoathirika ni wananchi wa kawaida kama vile ilivyo Zimbabwe.

Viongozi hao wa vyama vya upinzani wametoa tahadhari hiyo, ikiwa ni siku chache tu, baada ya Membe kuonya kuwa balozi yeyote anayeiwakilisha nchi yake nchini akibainika kushirikiana na vyama vya upinzani kutaka kuking'oa madarakani chama tawala atafukuzwa nchini.

Akizungumzia onyo hilo la serikali kwa mabalozi, Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia, jana alisema kuwa kauli hiyo ya Membe si ya kiungwana kwa mabalozi na inafaa kulaaniwa na wana-demokrasia wote.

Alisema kuwa mabalozi wapo nchini si tu kwa ajili ya ushirikiano wa kiserikali kati ya nchi zao na Tanzania, bali pia kuangalia masuala mbalimbali kama vile demokrasia, haki za binadamu na utawala bora, na kwamba mambo hayo yanapokiukwa wanaweza kukemea na kwamba jambo hilo si kuingilia mambo ya ndani ya nchi.

Alisema kuwa nchi wafadhili zinachangia zaidi ya asilimia 40 ya bajeti ya serikali, hivyo hawawezi kukaa kimya kuona baadhi ya mambo kama vile ukiukwaji wa demokrasia na haki za binadamu yakitokea.

"Mabalozi wanajua mipaka ya kazi zao hawaingilii mambo hivyo ni mpaka pale wanapoona kuna tatizo, nchi zao zinachangia zaidi ya asilimia 40 ya bajeti ya serikali, hivyo hawawezi kukaa kimya wanapoona kuna ukiukwaji wa demokrasia na uvunjaji wa haki za binadamu", alisema.

Mwenyekiti huyo wa NCCR-Mageuzi, alidai kuwa uzoefu umeonyesha kuwa vyama tawala barani Afrika mara nyingi ndiyo vimekuwa chanzo cha vurugu na machafuko pale vinapominya demokrsia, kukiuka haki za binadamu na kuvuruga chaguzi na kwamba vinapobanwa na wafadhili hapo ndipo vinapowaona wabaya. Aliitahadharisha serikali kutowabana mabalozi pale wanapoingilia kati mambo ambayo yanaonekana wazi kukiuka misingi ya demokrasia na haki za binadamu, kwani kwa kufanya hivyo kunaweza kuisababishia nchi matatizo makubwa kama vile kuwekewa vikwazo na watakaoathirika ni wananchi wa kawaida.

Alisema anashangaa kuona serikali ikianza kuvibana vyama vya upinzani wakati huu wa kuelekea uchaguzi mkuu mwakani, kwa kuweka masharti mbalimbali kama vile kuzuia vyama visipate ufadhili wa nje wakati wa uchaguzi. "Mambo yote haya yanafanyika kwa ajili ya uchaguzi mkuu mwakani, hili si jambo zuri" alisema.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa, alisema serikali haina mamlaka ya kuvizuia vyama vya upinzani kupata misaada kutoka nje ya nchi wala kuwazuia mabalozi kuingilia mambo yanayoweza kuivuruga nchi na kuleta machafuko.

"Kwa mujibu wa mkataba wa Vienna ambao Membe ndiyo ameutumia kuwaonya mabalozi kutoingilia mambo ya ndani ya nchi, serikali haiwezi kuwazuia mabalozi kuingilia mambo ya nchi kama kuna unyanyasaji, ukandamizaji wa demokrasia, ukiukwaji wa haki za binadamu na kuvururuga chaguzi" alisema. Kuhusu dhamira ya serikali kutaka kutunga sheria ya kuvizuia vyama vya siasa kupata misaada ya kifedha kutoka nje ya nchi wakati wa uchaguzi, Dk. Slaa, alisema kuwa sheria hiyo ina lengo la kuvikandamiza vyama vya upinzani.

"Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndiyo kinachoongoza kwa kupata misaada mingi ya kifedha wakati wa uchaguzi kutoka kwa vyama marafiki nje ya nchi na ushahidi tunao hivyo sheria hii itakuwa ni ya kibaguzi" alisema.

Mkurugenzi wa Uenezi na Mahusiano na Umma wa Chama cha Wananchi (CUF), Salim Bimani, alisema kuwa, hatua ya serikali kutaka kuwabana mabalozi ni ya kidikteta na isiyofaa kutekelezwa katika nchi ya kidemorasia na kuendeshwa katika misingi ya haki.

"Kwanini wanataka kuwabana mabalozi, hawa jamaa hawaingilii mambo ovyo, wanajua wajibu wao, utakorofishana nao pale tu utakapokiuka haki za binadamu, kwenda kinyume cha misingi ya kidemokrasia na kuharibu uchaguzi, sasa serikali inaogopa nini? labda kama inajiandaa kufanyika kitu kibaya ambacho wanajua mabalozi wataingilia, kwa hiyo wanajihami kabisa", alisema.

Bimani, alisema anatafsiri onyo hilo la serikali kwa mabalozi kama njia ya kuvibana vyama vya upinzani visidai haki pale itakapokiukwa.

"CCM imeishiwa sasa inatumia nguvu kuvibana vyama vya upinzani ikihofu kuwa uchaguzi mkuu ujao unaweza kuwa mbaya kwa upande wake", alidai kiongozi huyo wa CUF.

Kama ilivyo kwa Mbatia, naye alitahadharisha kuwa endapo serikali itamtimua balozi yoyote kwa sababu tu amekemea uvunjaji wa haki za binadamu, uvurugaji wa uchaguzi, basi Tanzania inaweza kuingia katika mgogoro mkubwa wa kidiplomasia nchi fadhili ambalo zinaweza kusitisha misaada na watakaoathirika ni wananchi wa kawaida.

"Umeona Zimbabwe imewekewa vikwazo, wanaoteseka ni wananchi, kila kitu kimevurugika, hii yote ni kutokana na kiburi cha watawala wasiiongitia demokaria, haki za binadamu na kuvuruga uchaguzi, wametimua mabalozi wanaotaka kuona haki inatendeka sasa wanakiona" alisema.

Alitoa wito kwa wananchi, asasi zisizo za kiserikali na wapenda mageuzi wote, kukemea na kulaani onyo hilo la serikali kwa mabalozi, akisema kuwa endapo litatekelezwa linaweza kuleta madhara makubwa kwa nchi na wananchi wake.

Kauli hizo za wanasiasa wa vyama vya upinzani, zimekuja siku tatu tu, baada ya Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, kuonya kuwa serikali ya Tanzania itamfukuza nchini Balozi au ofisa yeyote wa kibalozi atakayebainika kushirikiana na vyama vya upinzani kuking’oa chama tawala madarakani.

Serikali pia imesema, nchi zinazotoa misaada kwa Tanzania hazina mamlaka ya kuingilia mambo ya ndani ya Tanzania.

Membe, alitoa msimamo bungeni ambapo alisema kwamba, mabalozi au ofisi za mabalozi wanaruhusiwa kushirikiana au kuvisaidia vyama vya siasa lakini si kwa lengo la kuking’oa chama tawala madarakani.

Alisema, Balozi au ofisa wa kibalozi atayeshirikiana na vyama vya siasa kuking’oa chama tawala madarakani watakuwa wanaingilia mambo ya ndani ya nchi mwenyeji, kuvunja itifaki na sheria za kimataifa.

Kwa mujibu wa Waziri Membe, kifungu cha tisa cha Mkataba wa Vienna kinairuhusu Serikali kuwafukuza nchini bila hata kutoa sababu yoyote ya kufanya hivyo.

CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

TANZANIA SI NCHI MASIKINI TENA? ha! ha! ha!

Subject: [tanzanet] Tanzania' si masikini' tena

Imeandikwa na Na Joseph Lugendo; Tarehe: 31st October 2009 Habari Leo


TANZANIA imeingia katika kundi la nchi zenye maendeleo ya watu ya kati kutoka katika kundi la nchi zenye maendeleo ya watu ya chini duniani, imebainishwa katika Ripoti ya Umoja wa Mataifa ya Maendeleo ya Binadamu.

Lakini wakati Tanzania ikiingia katika kundi hilo la nchi zenye maendeleo ya watu ya chini duniani ugumu wa maisha unaotokana na kuongezeka kwa mfumuko wa bei na njaa inayotokana na ukame uliolikumba taifa vikiendelea kuwa changamoto kwa jamii ya sasa.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo iliyotolewa Octoba 13 mwaka huu, Tanzania ambayo ilikuwa nchi ya 159 katika kundi la nchi zenye maendeleo ya chini kati ya nchi 177 zilizoorodheshwa na ripoti hiyo ya mwaka 2007/2008, mwaka huu imepanda na kuwa nchi ya 151 na kuondoka katika kundi hilo la nchi zenye maendeleo ya chini ambalo nchi ya Niger imeshika mkia.

Ripoti hiyo imeonesha nchi kumi kwa kuwa na maendeleo ya juu zaidi duniani kwa mwaka huu zimeongozwa na Norway na kufuatiwa na Australia, Iceland, Canada, Ireland, Uholanzi, Sweden, Ufaransa, Uswisi na Japan.

Mwaka 2008 nchi kumi kwa kuwa na maendeleo ya juu zaidi duniani ziliongozwa na Iceland na kufuatiwa na Australia, Norway, Canada, Ireland, Uholanzi, Sweden, Japan, Luxembourg na Uswisi.
Hata hivyo imefafanuliwa katika ripoti hiyo kuwa katika nchi hizo zenye maendeleo ya binadamu ya juu, kuna tofauti ndogo sana kati ya nchi moja na nyingine.

Vigezo vilivyotumika kupandisha nchi kutoka nafasi moja kwenda nyingine kwa mujibu wa ripoti hiyo ni kuongezeka kwa umri wa kuishi mwanadamu kwa afya njema, fursa ya kupata elimu na kupata maisha bora.

Vipimo vya vigezo hivyo ni umri wa wastani wa kuishi wa mwanadamu katika nchi husika, wastani wa watu wazima wanaojua kuandika na kusoma pamoja na kiwango cha uandikishaji wa wanafunzi wanaojiunga na darasa la kwanza na wastani wa kipato cha mtu mmoja mmoja kwa mwaka.

Katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Kenya imeongoza kwa kushika nafasi ya 147 duniani kwa mwaka huu kutoka nafasi ya 148 katika ripoti ya mwaka 2007/2008 na Tanzania kwa kushika nafasi hiyo ya 151 duniani, imekuwa ya pili katika nchi za EAC kutoka nafasi ya tatu mwaka 2007/2008.

Uganda imeshika nafasi ya tatu katika nchi wanachama wa EAC mwaka huu kwa kushika nafasi ya 157 duniani, hata hivyo imeporomoka nafasi tatu kwani mwaka 2007/2008 ilikuwa nafasi ya 154.

Rwanda na Burundi bado ziko katika kundi la nchi zenye maendeleo ya chini ambapo Rwanda ipo katika nafasi ya 167 mwaka huu na imeporomoka kutoka nafasi ya 161 mwaka 2007/2008 na Burundi imeshika nafasi ya 174 mwaka huu wakati katika ripoti ya 2007/2008, ilikuwa ya 167.

Tanzania imepiga hatua hiyo baada ya ripoti ya sasa kutumia takwimu za 2007 ambazo zimeonesha mafanikio katika sekta ya elimu na kuna uwezekano katika ripoti zijazo ikaendelea kupiga hatua kutokana na matarajio ya kuongezeka kwa umri wa wastani wa kuishi mwanadamu. Kwa sasa umri wa wastani wa kuishi mwanadamu Tanzania ni miaka 55.

Kwa mujibu wa Tarifa ya Takwimu za Tanzania (Tanzania in Figures) iliyotolewa mwaka huu na Ofisi ya Takwimu ya Taifa, umri wa wastani wa kuishi mwanadamu unatarajiwa kuongezeka kutokana matarajio ya kupungua vifo vya watoto walio chini ya miaka mitano na wajawazito vinavyosababishwa na malaria baada ya kufanikiwa kwa usambazaji wa vyandarua vyenye dawa kwa bei nafuu.

Hata hivyo kupiga hatua kwa Tanzania katika ripoti zijazo kutategemea upatikanaji wa takwimu halisi za nchi nyingine kwani ripoti hizo za UN zimebainisha kuwa orodha ya maendeleo ya watu katika nchi husika hutokana na takwimu walizopata kutoka katika nchi hizo kwa wakati huo na kwamba zinaweza zisitoe picha ya hali halisi ilivyo.

Kutokana na hali hiyo, upatikanaji wa takwimu kwa wakati katika nchi husika, unaweza kubadilisha matokeo ya nafasi ya nchi husika katika orodha hiyo ya maendeleo ya watu kwa mujibu wa nchi wanazoishi, lakini mabadiliko hayo yataonekana katika ripoti zijazo.

Wakati ripoti ya UN ikiwa na matokeo hayo, Ripoti ya Bajeti ya Kaya iliyotolewa Januari mwaka huu imeonesha kuwa Watanzania walio wengi bado wanaishi maisha ya chini ambapo wengi nyumba zao zina sakafu ya udongo, kuta za udongo na miti na kupauliwa kwa miti nyasi na udongo.

Ripoti hiyo ya Bajeti ya Kila Kaya pia imeweka bayana kuwa katika mali ambazo Watanzania wanazimiliki kwa wingi ni vifaa vya jikoni, vitanda, viti na meza huku kompyuta ikiwa mali inayomilikiwa na Watanzania wachache zaidi ikifuatiwa na redio za kisasa (Complete music system), magari, simu za mezani (land line) na pikipiki.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo ya kaya, asilimia 67 ya nyumba za Watanzania zina sakafu za udongo. Hata hivyo nyumba za aina hiyo zimeelezewa kupungua kutoka mwaka 2001 ambapo asilimia 74 ya nyumba za Watanzania zilikuwa na sakafu za udongo.

Pia nyumba nyingi kwa kiwango cha asilimia 68.1 kuta zake zimejengwa kwa fito, udongo na mawe ingawa zimepungua kutoka zilizokuwepo mwaka 2001 ambapo asilimia 74 za nyumba za Watanzania zilikuwa na kuta hizo.